Tuesday, December 10, 2013

Tanzania Yaadhimisha siku Ya Uhuru: Vita Kubwa Yatangazwa.

Tanzania yaadhimisha
siku ya uhuru huku
kukiwa na miito ya vita
kubwa zaidi dhidi ya
umasikini:

Tanzania iliadhimisha miaka 52 ya uhuru wake
siku ya Jumatatu (tarehe 9 Disemba) lakini
wasomi wengi wameikosoa serikali kwa
kutokufanya jitahada za kutosha katika kuondoa
umasikini miongoni mwa raia.

Kwa mujibu wa Honest Ngowi, profesa wa
uchumi kwenye Chuo Kikuu cha Mzumbe, pato
la jumla la Tanzania linakua kwa asilimia 7 kwa
mwaka, lakini hali ya uchumi kwa Watanzania
wengi inazorota.

"Tunapaswa kuhakikisha ukuaji wa uchumi wetu
unapunguza umasikini wa watu, na hasa
Watanzania wa kawaida,"

Aliongeza kwamba Tanzania ina uhuru wa
kisiasa lakini si uhuru wa kiuchumi, ambao ni
muhimu kwa maendeleo ya kijamii

Gaudence Mpangala, profesa wa sayansi ya
siasa kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
alikubaliana na hoja hiyo.

Alisema kwamba takwimu ambazo
Tanzania inaonesha kwa washirika na wafadhili
wa kimataifa zinaonesha kwamba uchumi wa
nchi hiyo unakuwa kwa kasi, lakini kiuhalisia
wananchi masikini hawaoni manufaa yake.

Benson Banna, profesa wa sayansi ya jamii
kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, aliisifu
serikali kwa kudumisha amani na utulivu ndani
ya miaka 52 iliyopita, lakini uwekezaji zaidi
unahitajika kwenye elimu na viongozi lazima
wabadilike kutoka kuwa wapangaji na kuwa
watekelezaji.

"Viongozi wetu wanaongea sana," Bana aliiambia Chanzo cha habari.

"Wakati umefika sasa kwa viongozi wetu wawe
watu wa vitendo zaidi badala ya kupiga soga.

Hii ndiyo njia pekee ya kufikia maendeleo
yanayoonekana kwa nchi yetu."

Tanzania ilipata uhuru kutoka kwa Uingereza
tarehe 9 Disemba 1961.
Wakati huo huo, Benki ya Dunia ilikubali
kuendelea upya na msaada wake kwa Mfuko wa
Jamii wa Tanzania (TASAF) baada ya kutathmini
vyema maendeleo yake ya siku za karibuni chini
ya mpango wa TASAF-III, liliripoti gazeti la Daily
News la Tanzania.

"Benki ya Dunia itaendelea kuisadia serikali ya
Tanzania katika kuhakikisha malengo ya kuondoa
umasikini yanafikiwa," alisema afisa wa Benki ya
Dunia Denny Kalyalya wakati wa ziara yake
kwenye kijiji cha Fukayosi siku ya Jumamosi
(tarehe 7 Disemba).

Mchimba Riziki.


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score