Sunday, April 13, 2014

Ni Nini Maana Ya Neno: Ni Uwezo Gani Upo Katika Neno?

Neno ni nini?
Neno ni matamshi yenye maana yanayotoka kwenye kinywa cha mtu, au kitu !
Holy Bible
Kibiblia neno ni yale mambo yaliyojaza moyo wa mtu , biblia inasema “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake , hutoa yaliyo mema,na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoka yaliyo maovu; kwa kuwa mtu hunena yale yaujazayo moyo wake” Luka 6:45 amplified bible moyo umeandikwa kama (storehouse).

Neno la Mungu
Neno la Mungu ni yale maneno yanayotoka kwa Mungu, na ni makusudio ya somo hili kujifunza uweza ulio katika neno la Mungu ili yamkini tupate kujua msaada tutakao upata kwenye neno hilo! Mungu anaongea sana kupita unavyofikilia lakkini unawezaje kulipokea neno na kulitumia hapo ndo wengi wanaposhindwa.

UWEZA ULIO KATIKA NENO LA MUNGU
1) Uwezo wa kukuongoza katika njia sahihi.
“neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu” Zaburi 119:105 , neno linatuonyesha tunapoelekea, linatuongoza kutenda kwa usahihi kama vile nchi bila katiba inapotea, ndivyo mtu anayemwamini Yesu kutokuwa na neno la Mungu moyoni mwake! lazima atapotea! Mungu akamwambia Joshua “kitabu hiki cha torati kisitoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku…ndipo utakapoifanikisha njia yako…” Joshua 1:8. Ni kwa kufuata Neno la Mungu ndipo mtu anaweza ifanikisha njia yake!

2) Uwezo wa kutufanya hai.
“maana mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu” Mathayo 4:4, neno limejaa uwezo wa kutufanya hai, kama vile mwili bila chakula unakufa ndipo mtu aliye na Yesu bila neno lake lazima atakufa kiroho. Neno la Mungu linatupatia nguvu ya kuishi bila neno la Mungu maisha yetu ya kiroho yamo hatarini, Petro akamwambia Yesu “basi twende kwa nani wewe unayo maneno ya uzima” maneno ni uzima!

3) Uwezo wa ushindi dhidi ya shetani.
“tweni upanga wa roho ambao ni neno la Mungu” Waefeso 6:17b ,. Mkristo asiye na neno la Mungu ni sawa na mwanajeshi asiye na silaha alafu yuko vitani, neno la Mungu ni salaha kuu dhidi ya shetani “je, neno langu si kama moto, asema Bwana, na kama upanga ukatao kuwili?” neno la Mungu ni ushindi mkamilifu dhidi ya shetani! Tukijua kulitumia ni ushindi mkamilifu!

4) Uwezo wa kupokea kutoka kwa Bwana.
“…….na maneno yangu yakikaa ndani yenu , ombeni lolote mtalipata” Yohana 15:17. Neno likijaa ndani yetu tutajua jinsi ya kuomwomba Mungu sawa sawa. Ni muhimu kuishi kwa kusoma neno la mungu ili tuombe sawa na mapenzi yake .


5) Uwezo wa kuumba.
“kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa NENO LA MUNGU….” Waebrania 11:3. “maana yeye alisema ikawa,NA YEYE ALIAMURU IKASIMAMA” Zaburi 33:9 neno lina nguvu ya kuumba inategemea unaamuru nini na kwa uweza gani! Hivyo hata ukipita katika ugonjwa unaweza ukasimama mwenyewe ukaamuru kwa uweza wa kuumba na ugonjwa ukaondoka. Yesu alikuwa anatumia maneno kama haya kuponya watu “nataka takasika” uwe mzima” “mtoke mtu huyu” haya ni maneno ya kuumba kama Mungu alivyo tamka “iwe nuru ikawa n.k.” mwanzo 1:1-.. .

6)Ni Mungu mwenyewe.
“hapo mwanzo kulikuwa na neno , naye neno alikuwako kwa Mungu naye neno alikuwa Mungu” Yohana 1:1 ,. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe, kwasababu huwezi kumtofautisha mtu na neno lake , Mungu ni neno na ndio maana sisi tukilishika neno lake tunakuwa washiriki wa tabia ya kiungu “…tupate kuwa washiriki wa tabia ya kiMungu…” 2Petro 1:4,. The Amplified Bible says that “ sharer (per-takers) of divine nature” na kwa namna hiyo tunaitwa miungu “mimi nimesema ndinyi miungu,na wana waa aliye juu wote pia..” Zaburi 82:6. Kumbe tunapata uwezo wa kuumba kwasababu na sisi ni mi ungu kwa kulishika neno lake!

Tunapataje uwezo wa Neno la Mungu!
“hapo mwanzo kulikuwa na neno, naye neno alikuwako kwa Mungu naye neno alikuwa Mungu, . Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa yeye; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima , nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo yang’aa gizani wala giza halikuiweza!” Yohana 1:1-5 ,.


Mambo ya kujifunza kutoka kwenye hilo andiko!
1.) Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe hivyo si la kulifanyia mzaha, kamwe huwezi kumtenganisha mtu na neno lake , ndiyo maana hata Mafalisayo walimtega Yesu kwenye maneno yake ili wamkamate “wakamviziavizia …ili wamnase kwenye maneno yake, wapate kumtia kwenye enzi ya mamlaka ya liwali” Luka 20:20. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe.

2.) Tunajifunza jinsi ya kulitumia neno la Mungu , biblia inasema “ ndani yake ndimo ulimokuwa uzima” ni muhimu kujua kusikia neno tu haitoshi bali kujua kilichoko ndani ya neno hilo, Neno la Mungu lina uzima ndani yake ambao huwezi kuupata kwa kusikia peke yake! Ni kweli kusikia neno la Mungu kunaleta imani(warumi 10:17) lakini imani inatakiwa kuwekwa kimatendo hapo inamaanisha udhihirisho wa neno ulilolipokea na hapa ndipo wakristo wengi wanashindwa kujua na kubaki kumlaumu MUNGU!

3.) Tunaweza kuupokea ule uzima ulio katika neno , kwa kutafakari neno, kivipi basi? Tuchukue mfano wa tundo kama chungwa huwezi kula pamoja na maganda yake ni lazima kumenya maganda kwanza ndipo ule , sasa chungwa ni kama neno la Mungu na maganda ni tafsiri za kibinadamu, Kutafakari neno ni kumruhusu Roho mtakatifu akufundishe kama tulivyoona hapo juu kuwa NENO NI MUNGU, na hakuna anayejua mafumbo ya Mungu isipokuwa Roho mtakatifu, (1wakorintho2:10-11) hivyo Roho hutufunulia kwa kutafakari neno la Mungu Daud akasema “na sheri huitafakari mchana na usiku”

4.) Je wajua kuto kutafakari neno la Mungu ni kumzimisha Roho wa Bwana?
Biblia inasema “ tusimzimishe Roho wa Bwana” 1Thesalonike 5:19 ,. Kuto kutafakari neno la Mungu ni kumzimisha Roho wa Bwana, kwa sababu haumruhusu yeye kukufundisha na huku biblia inasema “Roho atatufundisha kuyashika yote” sasa ni Muhimu kutafakari neno la Mungu kwa kufanya hivyo tunaruhusu uwezo wa Neno la Mungu kutenda kazi katika maisha yetu!

5.) Sasa kwa kutafakari ndipo unapo ingiza uzima kwenye maisha yako, kwenye kazi yako , mafanikio yako (Joshua 1:8) n.k. iyo ndiyo Nuru inayo ng’aa gizani hata giza na wakuu wake hawataiweza kabisa! Jifunze kujiwekea Ratiba ya kusoma neno la Mungu kila siku na kutafakari(meditation) unahusianisha na maisha na kumwomba Roho mtakatifu akufundishe !............................

Shukrani na sifa ni kwa bwana kwa neno lake lipate kupenya ndani ya moyo wako na kuweza kubadilisha maisha ya wengi...
Pia Shukrani za dhati zimfikie mtumishi wa Bwana:

David Mgongolwa Wa New Hope Ministry
E-mail : davidmgongolwa@ymail.com

Imechapishwa Na Kuletwa Kwenu na 
Mathayo Tajiri Ngotee Mchimba Riziki Blog Ceo&Director
lebangotee@yahoo.com

 MAY GOD BLESS YOU


0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score