Thursday, May 8, 2014

Abdulfatah al Sisi mwanajeshi Anayetaka Urais Misri.

Abdulfatah al Sisi mwanajeshi anayegombea katika uchaguzi wa rais wa Misri na ambaye siku hizi ndio gumzo la siku katika vyombo vya habari, amesema katika mahojiano na kanali ya CBC kwamba nchini Misri hakuna tena kitu kinachojulikana kama Ikhwanul Muslimin.

Al Sisi pia amejiarifisha kuwa ndiye mwakilishi wa wananchi wa Misri, na kwamba yeye si mgombea wa jeshi.

Wakati huo huo amesisitiza kuwa iwapo atashinda urais, Misri itashuhudia matukio mazuri.

Ingawa matamshi hayo yanaweza kutafsiriwa kuwa ya kampeni, lakini kutamka wazi jenerali huyo wa zamani wa jeshi kwamba harakati ya Ikhwanul Muslimin haina tena nafasi nchini Misri, kunaonesha kuwa atakabiliana vikali na wapinzani, suala linalokinzana na misingi ya demokrasia na uhuru wa kujieleza.

Wakati huo huo, makundi ya kutetea haki za binadamu nchini humou sambamba na kusema kuwa al Sisi anaungwa mkono na wanajeshi, yamesisitiza kuwa jeshi linazuia uhuru wa vyombo vya habari na wapinzani wa kisiasa.

Wananchi wa Misri bado hawajasahau kipindi cha miaka 30 ya kutekelezwa sheria ya hali ya hatari, iliyouwezesha utawala wa dikteta Hosni Mubarak kuwanyanyasa na kuwatia mbaroni wapinzani.

Pia tangu jeshi lilipompindua Rais Muhammad Mursi aliyechaguliwa na wananchi,

serikali ya mpito inayoungwa mkono kwa kiasi kikubwa na jeshi nayo pia inaendeleza mwenendo huo huo.  Serikali ya Misri kwa kuitangaza harakati ya Ikhwanul Muslim kuwa ni kundi la kigaidi,

harakati ambayo kwa muda wa mwaka mmoja ilitawala Misri, kivitendo imeonesha kuwa siasa zake ni kama za  utawala wa kijeshi wa Hosni Mubarak.

Moja ya sifa za watawala wa kijeshi wa Misri zilikuwa ni ukandamizaji na hivi sasa pia serikali ya mpito ya Cairo inaendeleza mwendo huo.

Jambo la kuzingatia hapa ni kuwa, al Sisi anajiona kuwa mwakilishi wa wananchi na sio jeshi.

Lakini kwa karibu miezi 10 iliyopita jeshi ndilo limekuwa likisimamia masuala ya Misri.

Kwa maelezo hayo ni wazi kuwa, hata kama Adil Mansour ndiye rais wa serikali ya mpito  lakini kivitendo nchi imekuwa ikiongozwa na jeshi.

Jenerali Abdulfatah al Sisi aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Misri ameingia katika kinyang'anyiro cha kugombea urais kwa kujivika vazi la kiraia, ili kwa mara nyingine aweze kuihusisha utawala wa kijeshi katika muundo wa kisiasa wa nchi hiyo.

Mwaka mmoja ambao Muhammad Musri aliongoza serikali ya Misri, ulikuwa ni wakati mgumu mno kwa wanajeshi waliokuwa wamezoea kudhibiti nguzo zote za kisiasa, kiuchumi na kiusalama.

Hata utawala wa Kizayuni, Marekani na madola ya Kiarabu ya pembezoni mwa Ghuba ya Uajemi pia yalionesha wasiwasi kutokana na Misri kuongozwa na utawala wa kiraia ulioletwa na kundi la Ikhwanul Muslimin.

Lakini baada ya jeshi kuipindua serikali ya Misri, wimbi la misaada ya kifedha na kisiasa ya Wamagharibi na serikali za Kiarabu lilianza kumiminika kwa serikali ya mpito ya wanajeshi.

Suala hilo linabainisha wazi kuwa, ushindi wa wanajeshi nchini Misri una umuhimu mkubwa  kwa nchi hizo za Magharibi na Kiarabu.

Lakini jambo lililo wazi ni kuwa, nchini Misri kila siku zinavyozidi kusonga mbele ndivyo malengo ya wanapambinduzi yanavyozidi kupewa mgongo huku jeshi likipiga hatua za kushika madaraka.

Hali hiyo ina maana kuwa, utawala wa kijeshi unakaribia tena kuasisiwa nchini humo suala linaloashiria uwezekano wa kuanza tena uasi, upinzani na machafuko mapya katika nchi hiyo ya Kiarabu ya kaskazini mwa Afrika.

Watu Waliofariki Wazidi Kuongezeka Wafikia Watu 78 Ni kutokana na kunywa pombe yenye sumu

IDADI ya watu waliokufa
kutokana na pombe
haramu katika mtaa wa
mabanda wa Shauri Yako,
Embu mjini imepanda na
kufikia watu 39 baada ya
waathiriwa zaidi ambao
walikuwa wamelazwa
katika Hospitali ya Embu
Level Five kuaga dunia.

Meneja wa mawasiliano wa St John Ambulance Bw
Fred Majiwa alisema kuwa miili miwili bado
haijatambuliwa, na kwamba wakazi wa Embu
wamehimizwa kuwaripoti watu wote waliotoweka
katika dawati la St John Ambulance hospitalini
humo ambalo liliwekwa mahususi kushughulikia
mkasa huo.

Wagonjwa 73 wametengwa katika hospitali hiyo hadi
sumu iliyokuwa ndani ya pombe waliyokunywa
itakapojulikana.

“St John Ambulance ikishirikiana na Idara ya
Huduma za Jamii wameunda dawati la kutoa
msaada kuwatafuta watu waliotoweka na ule wa
kisaikolojia wa kuzipatia familia na manusura
ushauri nasaha,” alisema Bw Majiwa.

Sampuli za
pombe hiyo pamoja na mkojo na damu ya
waathiriwa imepelekwa maabara ya serikali
kwa ukaguzi.

Afisa mkuu wa matibabu hospitalini humo Dkt
Gerald Ndiritu alisema kwamba wanatarajia
kupokea matokeo kamili katika muda wa siku mbili.

Kufikia sasa, pombe hiyo haramu imepelekea vifo
vya angalau watu 78 katika kaunti tano.

Kaunti ya Embu ambapo watu 39 wamepoteza
maisha yao, ndiyo yenye idadi kubwa ya vifo.

Katika kaunti ya Makueni, takriban watu 18
wamekufa, ilihali wengine 10 wamethibitishwa kufa
mjini Limuru, kaunti ya Kiambu.

Kaunti za Kitui na
Murang’a zimerekodi vifo tisa na viwili mtawalia.

MURANG’A
WATU watano zaidi walifariki Jumatano baada ya
kubugia pombe yenye sumu katika kaunti ya
Murang’a, hivyo kufanya idadi ya walioangamia
katika eneo hilo kufika watu saba.

Wawili walifariki katika soko la Kirere, eneo bunge
la Kigumo baada ya kunywa pombe inayofahamika
kama 'Sacramento’.

Pombe hiyo ambayo imekuwa
maarufu miongoni mwa watumiaji wake kimetiwa
kwenye chupa za milimita 500.

Watu Wengine watatu
walifariki eneo la Kamucii.

Madaktari walikuwa na kibarua kigumu cha kutibu
idadi kubwa ya waathiriwa ambao walikuwa
wakisombwa na ambulansi huku wengine wakiletwa
na jamaa zao.

Magari ya ambulensi yalikuwa yakizuru kila kijiji
kubeba waathiriwa wa pombe hiyo.

Kamishna wa kaunti hiyo Bi Kula Hache alisema
maafisa wa polisi tayari wamekusanya sampuli za
pombe hiyo katika baa mbalimbali za Kigumo na
Maragua na kupelekwa katika kituo cha polisi cha
Kigumo ambapo inafanyiwa uchunguzi na maafisa
wa Shirika la Takwimu nchini na Mamlaka ya
Ukusanyaji Ushuru (KRA).

MAKUENI
Idadi ya watu waliofariki kutokana na pombe
haramu katika kata ya Kitise, Kaunti ya Makueni
imeongezeka kutoka 12 hadi 16 na waliolazwa
hospitalini kutoka 67 hadi 75.
Akizungumza na mwandishi wa Taifa Leo
Mkurungezi Mkuu wa afya Kaunti ya Makueni Dkt
David Kiuluku alisema kuwa idadi hiyo iliongezeka
baada ya maiti zao kupatika katika kijiji cha Kitise.

Kiuluku alisema kuwa waathiriwa wanane walifariki
wakitibiwa katika hospitali ya Makueni ilhali wengine
wanane walipatikana wamefariki katika vijiji vya
Kitise na Kanzokea.

Kiuluku alisema kuwa hospitali ya Makueni ilikuwa
na waathiriwa 75 na mmoja katika hali maututi na
watatu wakiwa vipofu.

Mmoja wa waliolazwa alikuwa mhudumu katika baa
ya Kasovo iliyo eneo la Kitise.

Mbithe Muthoka ambaye ndugu zake walikuwa
miongoni mwa waathiriwa alisema kuwa mamake
alikuwa amempigia simu baada ya watatu hao
kutoamka Jumatatu asubuhi.

Mmoja wa ndugu zake Munyao Muthoka alifariki
na wengine watatu wanapokea matibabu katika
hospitali ya Makueni.

Haya ndio madhara makubwa yaliyotokana na pombe yenye sumu iliyotengenezwa Nairobi katika mtaa wa Kariobangi North.

Swali ni jee kilipata wapi kibali cha kuingia sokoni? Je KRA hawakudhibitisha ubora ama kulikuwa na Ukora?

Mchimba Riziki itaendelea kuchunguza hayo yote na utayapata hapa hapa.

Wednesday, May 7, 2014

Uchaguzi mkuu Afrika Ya Kusini.

Uchaguzi mkuu nchini Afrika Kusini, utafanyika leo Jumatano.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni, ushindani mkali utakuwa kati ya wagombea watatu kutoka vyama vya ANC, chama cha upinzani cha muungano wa kidemokrasia na chama cha wapigania uhuru na uchumi.

Kuna jumla ya wagombea elfu nane na 651, ambao wanatoka katika vyama 45 vya kisiasa, watakaochuana katika uchaguzi huo.

Uchaguzi mkuu nchini Afrika Kusini hufanyika kila baada ya miaka mitano.

Mbali na Rais, katika uchaguzi huo huchaguliwa pia wawakilishi wa wananchi katika bunge linaloundwa na wajumbe 400 na wawakilishi 90 wa baraza la kitaifa la mikoa tisa ya nchi hiyo.

Zaidi ya watu milioni 25 yaani karibu nusu nzima ya wananchi wa Afrika Kusini, wamejiandika kushiriki katika uchaguzi huo.

Afrika Kusini ina jumla ya watu milioni 53 ambapo asilimia 80 kati yao ni watu weusi, na asilimia 9 pekee ikiwa inaundwa na watu weupe.

Hii ni katika hali ambayo matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanyika nchini humo yanaonyesha kuwa, chama tawala cha ANC kitashinda katika uchaguzi mkuu huo utakaofanyika hivi leo, kwa kujipatia asilimia 63 ya kura zote kiwango ambacho kiko chini ya asilimia tatu ikilinganishwa na kura za uchaguzi wa mwaka 2009..

Endelea kufuatilia Mchimba Riziki itakuletea matokeo hayo.

Tuesday, May 6, 2014

Kutana Na Mapacha Waliozaliwa Na Baba Tofauti.

Twins Marcus and Lucas arrived in the world just
48 minutes apart... yet they have two different
fathers.

Mum Charlotte Hilbrandt became pregnant by ex-
husband Michael AND new boyfriend Tommy when
she slept with both men within 48 hours.

It means the boys, who turned six last week, are
one of only three known sets of twins in the world
who are genetic half-brothers, beating odds of a
billion to one.

“You have a bigger chance of winning the lottery
than something like this happening,” said 38-year-
old Charlotte.

She is the first to admit her boys are like chalk and
cheese. Cheeky Marcus, her son by Michael, is
short and stout, red-haired with bundles of energy.

His twin Lucas, her son by Tommy, is taller, blonde
and has a more gentle, calm manner.

Even more surprisingly, both dads are very much a
part of their lives and Charlotte says they are one
big happy family.


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score