Thursday, January 30, 2014

Yaliyomo Magazetini Asubuhi Ya Leo Alhamisi Ya tarehe 30/01/2014..

Yaliyomo Magazetini Asubuhi Ya Leo Alhamisi Ya tarehe 30/01/2014..


Majira

Habari Leo

Mwananchi

Tanzania Daima

The Citizen

Daily News

Sport Starehe
Mchimba Riziki Magazetini 

Wednesday, January 29, 2014

Magazetini Leo 29/01/2014

Yaliyomo Magazetini Leo 29/01/2014
Majira
Uhuru
Nipashe
Tanzania Daima
Mwananchi
Guardian
Daily Nation
The Citizen
Habari Leo
MCHIMBA RIZIKI

Matokeo Yote Ya England Premier League Iko Hapa

Manchester united 2:0 Cardiff city
6' Van Parsie
59' Young
Nowrich 0:0 Newcastle united
Southampton 2:2 Arsenal
21' J.Fonte
48' Giroud
52' Carzola
54' Lallana
80' Red card Flamin
Swansea 2:0 Fullham
61' Chelvey
76' Chico
Crystal Palace 1:0 Hullcity
16' Punchion
90' Speron Red card
90' Mcgregor
Liverpool 4:0 Everton
21' Steven Gerrad
33' Sturridge
35' Sturridge
50' Luis Suarez.
MCHIMBA RIZIKI MICHEZO

Tuesday, January 28, 2014

Kenya si Kama Tanzania "Adhabu Kali Kwa Mchina Kenya".


Mahakama nchini Kenya imemtoza faini ya shilingi milioni 20 au dola laki mbili na thelathini raia mmoja mchina kwa kuhusika na biashara haramu ya pembe za ndovu.

Tang Yong Jian ametozwa faini ya dola laki mbili na thelathini
Adhabu hii inatokana na sheria kali za kudhibiti uwindaji wa wanyama pori.
Tang Yong Jian alikamatwa wiki jana akiwa na Pembe za Ndovu zenye kilo 3.4 katika sanduku lake katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Ikiwa atashindwa kulipa faini hiyo huenda akafungwa miaka saba gerezani.
Kenya iliharamisha biashara ya pembe za Ndovu mwaka 1989, lakini kumekuwa na ongezeko la biashara hiyo haramu katika miaka ya hivi karibuni.

Kuna hitaji kubwa la pembe hizo barani Asia kwa matumizi ya mapambo huku wahifadhi wa mazingira wakishuku kuwa pembe za Vifaru hutumiwa kama dawa Mashariki mwa Bara Asia.

Kenya inakabiliwa na changamoto ya kuwindwa kiharamu kwa Ndovu zake
Nchini Kenya kilo moja ya Pembe za Ndovu, inaweza kukugharimu kati ya shilingi 12,000-18,000.
Uwindaji haramu umetajwa kama bishara haramu ya kimataifa ambapo wawindaji hasa huwawinda ndovu na vifaru kwa wingi. Ni hapo jana tu ambapo kifaru mmoja aliyetambulika kwa jina Josephina, aliuawa katika mbuga ya wanyama ya Nairobi.

Kenya inakabiliwa na changamoto ya kuwindwa kiharamu kwa Ndovu zake
Alikuwa kifaru wa kike mwenye umri wa miaka minne. Maafisa wa kulinda wanyama pori wanasema kuwa, kuuawa kwa Joeshina ni mfano mbaya kwani Vifaru wa kike wana umuhimu mkubwa katika kuongeza idadi ya wanyama hao wanapozaana.

Kwa muda wa wiki moja nchini Kenya, kimeripotiwa matukio manne ya uwindaji haramu katika mbuga tofauti tofauti.
Mkuu wa shirika la kulinda wanyama pori nchini Kenya, bwana William Kipsang, anasema kuwa tatizo la uwindaji linachangiwa na maswala ambayo hawawezi kudhibiti kama shirika.

''Serikali ya Kenya imetumia mamilioni ya fedha kuhifadhi wanyama pori , lakini nchini Kenya na kwingineko barani Afrika raia wengi wangependa kuona usalama wa binadamu ukishughulikiwa kwanza badala ya wanyama pori. Vile vile watu wengi huishi katika miji iliyo mbali na misitu na wanyama hao,'' alisema Kipsang

Mashirika ya kulinda wanyama wanasema ikiwa tatizo la uwindaji haramu halitatatuliwa, basi kwa muda wa miaka ishirini, ndovu na vifaru barani Afrika hawatokuwepo tena.
Asilimia kumi ya uchumi wa Kenya hutegemea utalii, ikiwa Kenya itapoteza Ndovu na vifaru wake, basi sekta ya utalii itaathirika pakubwa.

Chanzo BBC Swahili
Mchimba Riziki

Sunday, January 26, 2014

Droo Ya FA Imepangwa Dakika Chache Zilizo Pita

Droo ya michuano ya kombe la FA imefanywa punde kwa mechi za mchujo wa raundi ya tano.

Kombe la FA 
Chelsea wamepangiwa kucheza na Manchester City katika mchezo unaotazimiwa na ushindani wa hali ya juu.
Chelsea ambao wamefuzu kwenye raundi ya tano kwa kuiondosha Stoke City katika mchezo ambao ulimalizika kwa ushindi wa bao moja kwa bila.

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho akizungumza punde baada ya droo hii amesema, "Iwapo unataka kuwa bora lazima ucheze na timu bora."

Nao Manchester City wao walijikatia tiketi ya kufuzu michuano hiyo hatua ya tano kwa kuiadhibu Watford kwa mabao 4-2.

Liverpool wao watakuwa wageni wa Arsenal kwenye mchezo wa raundi ya tano.

Roberto Martinez ataiongoza Everton kukutana na timu yake ya zamani ya Swansea, ilihali Sunderland wao watacheza na Southampton ikiwa ni mechi liyokutanisha timu zote za ligi ya England.

Cardiff watakuwa nyumbani kuwakaribisha Wigan na Hull watacheza na Brighton. Sheffield Wednesday watapamabana na wenzao walioko kwenye ligi ya Championship, Charlton FC.

Mechi zote zitachezwa jumamosi na jumapili ya tarehe 15 na 16 mwezi wa pili.

Mshindi wa mechi kati ya Fulham ama Sheffield United atapambana na mshindi kati ya Nottingham Forest au Preston kwenye hatua ya raundi ya tano ya kombe hilo ambalo fainal yake itachezwa kwenye uwanja wa Wembley.

Droo kamili ni kama ifuatavyo;
Manchester City v Chelsea
Sheffield United au Fulham v Nottingham Forest au Preston North End
Arsenal v Liverpool
Brighton & Hove Albion v Hull City
Cardiff City v Wigan Athletic
Sheffield Wednesday v Charlton Athletic
Sunderland v Southampton
Everton v Swansea City.

Chanzo BBC 
Mchimba Riziki Michezo

Huyu Ndie Diamond Mwanamuziki Gali Afrika Mashariki Kote


Diamond Platinumz ndiye msanii kipenzi cha Afrika Mashariki kwa sasa ambaye kwa maneno matatu ya Kiingereza unaweza kumtaja kama; 'Hitmaker’, 'Heart Breaker’ na 'Moneymaker'.
Diamond Platinums Akiwa Kazini

Kwa ufupi ni mwanamuziki mwenye uwezo wa kuachia fataki wakati wowote kutokana na ubunifu mkubwa alionao, mzuri inapokuja katika suala la mauzo na mtundu inapofikia hatua ya kuwabadili vichuna.

Sifa hizo tatu zimemfanya kuwa msanii kichwa kwenye Ukanda huu akitajwa kuwa mwanamuziki ghali katika eneo hili.Ukweli ulipo ni kwamba umchukie au umkubali, Naseeb Abdul, ni msanii anayeshiriki ligi tofauti kabisa na wengine na wala hana mpinzani kwa wakati huu.
Lakini kama wasemavyo waswahili, safari ndefu huanza kwa hatua moja na licha ya umaarufu pamoja na utajiri mkubwa aliojipatia kwa kipindi kidogo, kuna alikoanzia Diamond Platinumz 'Rais wa wasafi.’

Rais wa Wasafi Diamond Na Timu Yake
HISTORIA
Sababu ya kuwa ghali kwa huduma zake, Diamond hakosi shoo zaidi ya mbili wiki baada ya nyingine, kwani mapromota kila uchao humpapatikia.
Akianza hakuna aliyemwandama kwani alionekana kuwa mbwa wa kubweka tu, ila sasa anang’ata kiasi cha kuhitaji walinzi wa kutosha kuhakikisha kwamba yupo salama.
Wengi hawafahamu alikochimbukia kijana huyu mzaliwa wa Kigoma, aliye na historia ndefu iliyokumbwa na umaskini wa kuogopesha enzi za utoto na ujana wake.
Diamond Na Timu Yake Ya Nyumbani Kigoma All Stars

UTAJIRI
Fataki ya 'Kamwambie’ aliyoifanya 2009 ndiyo iliyomfungulia milango ya rehema na kumwezesha kuwa nyota akiwafukuzia Lady Jay D na Jose Chameleone kwa ukwasi.
Tangu mwisho wa 2011, kwa mujibu wa blogu kadhaa ya Tanzania, akaunti yake ya benki haijawahi kushuka chini ya Ksh5.3 milioni (Tsh100 milioni). Na mali yake kwa ujumla inakadiriwa kuwa yenye thamani ya KSh64 milioni (Tsh1.2 bilioni).
Kutokana na kipato chake kizuri cha muziki, Diamond ameishia kuwa mjasiriamali mzuri akimiliki nyumba kadhaa za kupangisha, maduka ya nguo, vipande vya mashamba na magari makubwa.
Mtaani Tegeta, Dar-es-salaam, msanii huyo anaendelea kujenga jumba lake la kifahari ambalo linakaribia kumalizika na tayari yupo kwenye mchakato wa kujenga hoteli yenye hadhi ya 4-Star.
Aidha ana simu nne za rununu moja ikiwa na laini mbili hivyo basi kumaanisha ana nambari tano za simu. Hivyo wakati mwingi yeye hulazimika kuziweka kwenye milio ya chini kutokana na simu nyingi ambazo hupokea kwa siku.
Kando na hayo, makampuni mengi yanamlipa mamilioni ya pesa ili kutangaza bidhaa zao. Kampuni ya soda, Coca Cola na ile ya huduma za simu nchini Tanzania, Vodacom ni kati ya nembo kubwa zilizoko na mikataba minono naye.

MAISHA YA MUZIKI
Diamond Juu Ya Mchuma Moja ya Mali zake
Ndiyo kazi yake inayompa riziki na vile vile kumfanya kutoa ajira kwa timu yake kubwa ya zaidi ya watu 12, inayojumulisha madansa wake, msaidizi wa kibinasfi, wapiga picha na wapambaji.
Kila juma Diamond hupata shoo mbili hadi nne ambazo huhakikisha anakusanya ujumla wa zaidi ya KSh2 milioni ndani ya Tanzania hesabu za haraka zikionyesha kuwa kwa shoo moja huwagharimu mapromota Ksh350,000.
Anapoalikwa kutumbuiza nje, malipo yake kwa shoo moja huwa haipungui dola 25,000 (Ksh2 milioni). Miaka miwili iliyopita, alitumbuiza nchini Rwanda kwenye tamasha kubwa la uwanjani na kupokea Ksh10 milioni.
Katika taaluma ya muziki, amerekodi zaidi ya nyimbo 133 na mwanamuziki anayemuhusudu sana ni Usher Raymond wa Marekani.
Baada ya kutumbuiza kwenye ufunguzi wa shindano la Big Brother Africa 2012, wakati huo akitamba na 'Mbagala’, msanii huyo alitangaza ada mpya ya kufanya kazi naye.
Kupitia Facebook yake alisema mwanamuziki yeyote ambaye angetaka kumshirikisha katika wimbo wake, angelazimika kumlipa Ksh265,000 kwa audio na ikiwa ni video, ada hiyo inakuwa maradufu.
“Nimefanya colabo nyingi ila nyimbo hizo huwa hazitokei katika albamu yangu na wala hazininufaishi kwa lolote. Sasa hivi muziki una maana ya biashara na ndio maana najipa thamani hii. Ikiwa wasanii wa mbele wanalipisha kwa collabo kwa nini mimi nisifanye hivyo,” alisema.
Diamond alianza muziki kwa kujaribu kuwa rapa lakini marafikize wakamshauri ajaribu mtindo mwingine kwani huo wa kufoka hakuwa akiumudu.
Nguli huyo humtaja mamake kuwa kigezo cha mafanikio yake kwani aliishi kuandamana naye kwenye tamasha nyingi za kusaka vipaji na talanta na angemsubiri muda wote.
Wimbo wa 'Mawazo’ alimwandikia mwigizaji wa filamu za bongo Jacqueline Wolper aliyewahi kuwa mpenzi wake. Ule wa 'Kamwabie’ na 'Mbagala’ alimtungia mpenziwe kwa jina Sarah, aliyemkataa sababu hakuwa na uwezo. 'Ukimwona’ alimwimbia mchumba wake Wema Sepetu waliyerudiana, baada ya kumsaliti.

MAISHA NA VICHUNA
Diamond Vs Wema
Pamoja na sifa nzuri za kuwa 'hitmaker’ maisha yake upande wa pili yamekuwa yakiandamwa na kashfa nyingi za kimapenzi kwa tabia yake ya kuwabadilisha wanawake kila anapohisi kufanya hivyo.
Japo aliwahi kudai kuumizwa sana na Wema aliyemtuhumu kwa kutokuwa mwaminifu kwenye uhisiano wao, kisura huyo ambaye ni staa wa filamu za bongo pia aliwahi kudai kulizwa na Diamond kwa maana moja wanafanana inapokuja kwani wanawezwa kutajwa kuwa 'heartbreakers’.
Uhusiano wao umekuwa wa kukosana na kurudiana na hata wakati ambapo walikuwa njia panda, mara kwa mara waliripotiwa kutafutana na kuendelea na usuhuba.
“Mimi na Naseeb tuliachana baada ya yeye kunidanganyia na Jokate (Mwegelo) baada ya mimi kuwafumania wakipigana busu wakati huo tukiishi pamoja. Muda wote nimekuwa naye sikuwahi kumsaliti na nilijichunga sana kwa ajili yake maana nilikuwa nisharidhika naye licha ya ugomvi wetu wa kila mara,” Wema alinukuliwa na gazeti la Mzuka walipotemana mara ya kwanza.
Kwa sasa wawili hao wamerudiana na uhusiano wao ni wa mtu na mchumbake na wala sio mpenzi tena.
Wakati ambapo Diamond anakutana na mtangazaji Jokate, mrembo huyo alikuwa tayari yupo kwenye uhusiano na mwanavikapu wa NBA, Hasheem Thabeet uliodumu kwa miaka miwili na Jokate alikiri kuwa alikuwa akimpenda sana mchezaji huyo.
Hata hivyo kutokana na uhusiano huo wa mbali Jokate akiwa Tanzania na mwenzake Marekani, kichuna huyo alijipata kwenye hali ya upweke na hivyo kumpa nafasi Diamond.
“Ilitokea tu kwani nilikuwa kwenye hali fulani akatumia nafasi au fursa hiyo lakini angenitongoza mwaka huu (2013) nisingemkubali,” gazeti la Ijumaa lilimnukuu Jokate, Oktoba mwaka jana.
Ni uhusiano ambao Diamond alikiri kuwepo katika mojawepo ya mahojiano na Clouds TV, kitu ambacho alionekana kujutia.
Kuachana huko kukawa ndio mwisho wao licha ya mwanamuziki huyo kumnunulia gari la thamini ya Ksh800,000. Ukaribu kati ya Diamond na Wema uliendelea licha ya tofauti zao.
Ni ukaribu ambao kwa kiasi kikubwa uliwaumiza wengi, muhusika mkubwa akiwa mtangazaji Penny Mungilwa ambaye kwake msanii huyo alikuwa mwanaume wa kipekee.
Penny aliishi kusikia uvumi akawa anaupuuzia kutokana na jinsi alivyomwamini Diamond lakini picha za mwanamuziki huyo wakiwa na Wema, Hong Kong zilipovuja, zilivunja moyo wa hidaya huyo ambaye tayari alikuwa kahamia nyumbani kwake.

Diamond Kazini 

Mchimba Riziki Makala




Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score