Friday, December 27, 2013

NG'OMBE WA MAAJABU HUKO INDIA, WANAWAKE HUJIFUNGUA WATOTO WA KIUME KILA WAMSHIKAPO NG'OMBE HUYO MWENYE MIGUU MITANO.

Ng'ombe mwenye miguu mitano amekuwa akifanya miujiza nchini India, hii ni kutokana kila mwanamke mwenye mimba akishika mguu huo wa tano hujifungua mtoto wa kiume.

Raj Pratap's ndio jina alilopewa Ngombe  huyo, Raj mwenye miaka mitatu alianza kuonyesha maajabu baada ya mwanamke mwenye watoto wanne kuushika mguu wake watano na mwanamama huyo kujaliwa kupata watoto mapacha  wa kiume kwa mara ya kwanza.

Mwanamama huyo alipojifungua mapacha hao mapema mwezi wa pili mwaka huu,habari hizo zilizambaa kote India kuwa ngombe mwenye miguu mitano mwenye bahati apatikana,kwani katika dini ya Hindu wanaamini kuwa kati ya ngombe 5 millioni lazima mmoja mwenye bahati atapatikana.

Kuanzia siku habari za Ng'ombe mwenye miguu mitano kujulikana, Bwana Pratap amekuwa akijiingizia kipato kikubwa baada ya wanawake 30 kumtembelea Ng'ombe na kuushika mguu huo wa tano ili wapate watoto wa kiume. Bwana Pratap alijipatia  karibia Rupia 500 za India sawa na £5.

Cha kushangaza ni kwamba taarifa zinasema wanawake wote hao waliomshika Ng'ombe huyo waliweza kujifungua watoto wa kiume wote 30.Hii ilisababisha mmiliki wa Ng'ombe huyo kuwa na uhakika hata kukubali kumrudishia mtu pesa kama hatafanikiwa kumpata mtoto wa kiume.

Jumatatu ya 23 Dec mwaka huu, Ngombe huyo alisherekea maajabu yake ya watoto 33 kupatikana baana ya mwanamke aliyeshika mguu wake watano  kujifungua mapacha watatu wote wa kiume.

Bwana Pratap alisema, watoto wote waliokwisha kupatikana ni 33 na wote ni wakiume, mara ya mwisho ni mapacha watatu wamepatikana. Aliongeza "sijui kwanini haya yanatokea  lakini Raju anayo zawadi na ninataka tushiriki na ulimwengu mzima".

Kila siku ninafikiri kumpeleka Raju "Ulaya " ama "Amerika " na kufanya maajabu kule, alisema bwana Pratap.

Katka jamii ya Kihindi watoto wakiume wanapendwa sana kwani wao wanafaida kubwa na ni msaada kwa familia zao.

Mwanamke mmoja aliyepata mtoto wa kiume mwezi wa kumi mwaka huu ambae amekataa jina lake kutajwa amesema,Ni zawadi kutoka kwa Mungu kuushika mguu huu wa tano wa Raju ni bahati sana ,na umenizawadia mtoto wa kiume ninafuha sana.Pia familia yangu wanafuraha sana kwa kujua kuwa niko na kijana.

Ng'ombe wanaabudiwa sana na Wahindi wanaoamini katika dini ya Hindus kuwa Mungu wao Krishna alikuwa ni mchunga ng'ombe. 

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score