Friday, April 18, 2014

Kurasa Za Magazeti Leo Ijumaa 18/04/2014

Tanzania Daima

Habari Leo

Mwananchi

Nipashe

Majira

Mtanzania

Raia

The Citizen

Kisiwa

Bingwa

Mwanaspoti

Spoti

Msimbazi

Bingwa

Nipashe Michezo

Msimbazi

Michezo

Mwanasporti


Mwananchi Michezo

Majira

Championi

Championi

Habari leo

Daily Sport

Daily News


Kisiwa

AN-NUUR

Ijumaa

Ijumaa

Kiu

Kiu

Mchimba Riziki
Sauti Ya Waislamu

Tuesday, April 15, 2014

Wakenya Kupata Vitambulisho Vipya Vya Kiraia.... Kuanzia Miaka 12 Watapata Vitambulisho..

Serikali imesema usajili mpya unaotarajiwa kufanywa utahusisha Wakenya wote wenye umri wa miaka 12 na zaidi. Usajili huo utakaogharimu Sh8 bilioni hautaanza kwa kutolewa kwa vitambulisho vya kitataifa  lakini utanakili habari zote zitakazohitajika kutoa vitambulisho.
Naibu Wa Rais Kenya Willium Ruto.
SERIKALI imesema usajili mpya unaotarajiwa kufanywa utahusisha Wakenya wote wenye umri wa miaka 12 na zaidi.
Katibu katika Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia Joseph Tiampati alisema usajili huo hautaanza kwa kutolewa kwa vitambulisho vya kitataifa  lakini utanakili habari zote zitakazohitajika kutoa vitambulisho..

Kuanzia miaka 12 mtu huwa na alama wazi za vidole hivyo  tayari kuwa na kitambulisho cha kitaifa,” alisema Bw Tiampati.
Kulingana na Bw Tiampati wale wako chini ya umri wa miaka 12 watatambuliwa kupitia vyeti vya kuzaliwa vyenye majina ya wazazi wao.
Katibu huyo aliongeza kuwa kando na alama za vidole, serikali itatumia macho kama sehemu za kujitambulisha hasa kwa walemavu.

Wakazi wengi wa maeneo yayochunwa chai hawana alama wazi za vidole hivyo tutawatambua kupitia macho,” alisema Bw Tiampati.
Vilevile serikali ilitangaza kuwa itakuwa na hifadhi spesheli ya habari za wageni walio nchini kihalali.
“Tutakuwa na sajili ya wale wanaoishi nchini kwa sababu zinazokubalika kisheria.” 
Akizungumza Jumanne wakati wa kongamano la Connected Kenya 2014 mjini Mombasa, Bw Tiampati alisema mchakato huo utagharimu serikali Sh8 bilioni.
“Tunataka kwanza kutengeneza mfumo mwafaka wa kuweka habari na baadaye Wizara ya Usalama wa Ndani itaendeleza mchakato wa kutoa vitambulisho upya kwa Wakenya wote,” alisema Katibu huyo.
Jumatatu Naibu wa Rais William Ruto alisema hatua hiyo ya kuwasajili Wakenya upya ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama nchini.
“Tutaanzisha mpango wa kuwapa Wakenya vitambulisho vya kidigitali vitakavyorahisisha kutambua wanaojisajili na kuingia humu nchini kinyume na sheria,” alisema Bw Ruto.
Bw Ruto alifichua kuwa mpango huo unaopaniwa kukamilika katika kipindi cha miezi sita ijayo, unatarajiwa kupunguza visa vya ugaidi na utovu wa usalama nchini unaosababishwa na watu ambao uraia wao unatiliwa shaka.

Aidha chama cha ODM Jumanne kilitilia shaka mpango huo na kuitaka serikali kueleza kwa kina jinsi mchakato huo utakavyofadhiliwa.
Katika taarifa iliosomwa na Mwakilishi wa Wanawake kaunti ya Taita Taveta Joyce Lay,viongozi wa ODM  walishangaa vipi serikali itamudu kufadhili mpango huo ilhali miradi mingine kama vile reli na vipatakilishi imekwama.
“Serikali itatoa fedha za huu mradi wapi na tayari imeshindwa kukamilisha miradi mingine. Hatuwezi kubali Wakenya kuumizwa zaidi kulipa ushuru ili kufadhili miradi ambayo haitawahi kukamilika,” alisema Bi Lay.
Bi Lay ambaye alikuwa ameandamana na mbunge wa Ugunja Opiyo Wandai na mwenzake wa Busia Florence Mutua, alisema hatua hio haina manufaa yoyote hadi serikali kwanza ikabiliane na kukomesha ufisadi miongoni mwa maafisa wake.
Serikali tayari imeunda vikundi kutoka wizara kadhaa ili kutathmini jinsi mpango huo utakavyoendeshwa kabla ya kuzinduliwa rasmi.

Monday, April 14, 2014

Chuo Kikuu Nairobi Mtihani Wafurugwa Na Kuchanwa Mbele Ya Wahadhiri Waliokuwa Wasimamizi.

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Nairobi Jumatatu walirarua karatasi za mitihani wakitaka waongezewe wiki moja zaidi ili kujiandaa vyema kwa ajili ya mtihani huo.
Chuo Kikuu Nairobi
Kundi la wanafunzi waliokuwa wakiongozwa na kiongozi wa wanafunzi, Paul Ongili maarufu Babu Owino, lilienda katika kila darasa ambamo mitihani ilikuwa ikifanyika na kurarua karatasi za maswali na vijitabu vya kuandikia majibu.

Mtihani wa somo la hisabati wa wanafunzi wa mwaka wa tatu na nne ambao tayari ulikuwa karibu kukamilika, ulikatizwa ghafla na wanafunzi hao ambao waliwataka wenzao kuondoka katika chumba cha mtihani.
Baadhi ya wanafunzi walilalamika walipoteza mali zao zikiwemo kadi za mtihani wakati wa rabsha hizo.
“Nimepoteza kadi yangu ya kufanyia mtihani, sijui nitapata wapi nyingine,” akasema Kennedy Nzioka, mwanafunzi wa uhandisi wa mwaka wa tatu.

Wahadhiri waliokuwa wakisimamia mitihani hiyo waliachwa mdomo wazi huku wakiwa wamejawa ghadhabu.
“Sina jambo la kuwambia wanahabari,” akasema Dkt Jeremiah Musuva ambaye alikuwa akisimamia mtihani wa somo la hisabati wa wanafunzi wa mwaka wa tatu.
“Mimi nilikuwa nimejiandaa vyema kwa ajili ya mtihani huu. Hata maswali yalikuwa rahisi,” akasema Edward Mailu, mwanafunzi wa Uhandisi mwaka wa tatu.
  Kulingana na Bw Ongili, wanafunzi hao wanataka uongozi wa chuo hicho kuwapatia wanafunzi muda zaidi ili kufidia wiki mbili ambazo wahadhiri walipoteza walipokuwa wamegoma.
“Tunataka wiki moja zaidi ya kujiandaa kwa ajili ya mtihani huo ili kufidia wiki mbili za mgomo wa wahadhiri,” akasema kiongozi huyo wa wanafunzi wakati wa mahojiano na waandishi wa habari
Bw Ongili ambaye alichaguliwa kuongoza wanafunzi wa chuo hicho, alidai kuwa wanafunzi hawakuwa wamejiandaa vyema kwa ajili ya mtihani huo baada ya kutatizwa na mgomo.
Alidai kuwa wiki iliyopita, wanafunzi waliwasilisha maombi yao kwa utawala wa chuo hicho wakitaka kuongezewa muda wa wiki moja kuwapatia wakati wa kutosha kusomea mtihani huo.

Maombi Rasmi
Hata hivyo, utawala wa chuo hicho ulikanusha madai hayo na kusema kuwa viongozi wa wanafunzi hawakuwasilisha maombi rasmi wakitaka kuongezewa muda.
“Uongozi wa chuo unapenda kushutumu kitendo hicho cha wanafunzi wachache kutatiza mtihani kwa madai kuwa hawajajiandaa vyema. Seneti ya chuo ndiyo ina mamlaka ya kusitisha mtihani ,” akasema afisa ambaye hakutaka kutajwa kwa sababu za kiusalama. 
“Kiongozi wa wanafunzi ni wanafunzi kama wengine na kulingana na sheria hakuna mwanafunzi ambaye ana mamlaka ya kuahirisha tarehe ya mtihani bila kupitia kwa seneti,” akaongezea.
Alisema kuwa tayari uongozi wa chuo umeanzisha mazungumzo na viongozi ili kutafutia suala hilo ufumbuzi.
Mitihani ilivurugwa ndani ya bewa kuu pekee lakini inaendelea vyema katika mabewa mengineyo tisa ya chuo kikuu cha Nairobi.


Sunday, April 13, 2014

Ni Nini Maana Ya Neno: Ni Uwezo Gani Upo Katika Neno?

Neno ni nini?
Neno ni matamshi yenye maana yanayotoka kwenye kinywa cha mtu, au kitu !
Holy Bible
Kibiblia neno ni yale mambo yaliyojaza moyo wa mtu , biblia inasema “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake , hutoa yaliyo mema,na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoka yaliyo maovu; kwa kuwa mtu hunena yale yaujazayo moyo wake” Luka 6:45 amplified bible moyo umeandikwa kama (storehouse).

Neno la Mungu
Neno la Mungu ni yale maneno yanayotoka kwa Mungu, na ni makusudio ya somo hili kujifunza uweza ulio katika neno la Mungu ili yamkini tupate kujua msaada tutakao upata kwenye neno hilo! Mungu anaongea sana kupita unavyofikilia lakkini unawezaje kulipokea neno na kulitumia hapo ndo wengi wanaposhindwa.

UWEZA ULIO KATIKA NENO LA MUNGU
1) Uwezo wa kukuongoza katika njia sahihi.
“neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu” Zaburi 119:105 , neno linatuonyesha tunapoelekea, linatuongoza kutenda kwa usahihi kama vile nchi bila katiba inapotea, ndivyo mtu anayemwamini Yesu kutokuwa na neno la Mungu moyoni mwake! lazima atapotea! Mungu akamwambia Joshua “kitabu hiki cha torati kisitoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku…ndipo utakapoifanikisha njia yako…” Joshua 1:8. Ni kwa kufuata Neno la Mungu ndipo mtu anaweza ifanikisha njia yake!

2) Uwezo wa kutufanya hai.
“maana mtu hatoishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu” Mathayo 4:4, neno limejaa uwezo wa kutufanya hai, kama vile mwili bila chakula unakufa ndipo mtu aliye na Yesu bila neno lake lazima atakufa kiroho. Neno la Mungu linatupatia nguvu ya kuishi bila neno la Mungu maisha yetu ya kiroho yamo hatarini, Petro akamwambia Yesu “basi twende kwa nani wewe unayo maneno ya uzima” maneno ni uzima!

3) Uwezo wa ushindi dhidi ya shetani.
“tweni upanga wa roho ambao ni neno la Mungu” Waefeso 6:17b ,. Mkristo asiye na neno la Mungu ni sawa na mwanajeshi asiye na silaha alafu yuko vitani, neno la Mungu ni salaha kuu dhidi ya shetani “je, neno langu si kama moto, asema Bwana, na kama upanga ukatao kuwili?” neno la Mungu ni ushindi mkamilifu dhidi ya shetani! Tukijua kulitumia ni ushindi mkamilifu!

4) Uwezo wa kupokea kutoka kwa Bwana.
“…….na maneno yangu yakikaa ndani yenu , ombeni lolote mtalipata” Yohana 15:17. Neno likijaa ndani yetu tutajua jinsi ya kuomwomba Mungu sawa sawa. Ni muhimu kuishi kwa kusoma neno la mungu ili tuombe sawa na mapenzi yake .


5) Uwezo wa kuumba.
“kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa NENO LA MUNGU….” Waebrania 11:3. “maana yeye alisema ikawa,NA YEYE ALIAMURU IKASIMAMA” Zaburi 33:9 neno lina nguvu ya kuumba inategemea unaamuru nini na kwa uweza gani! Hivyo hata ukipita katika ugonjwa unaweza ukasimama mwenyewe ukaamuru kwa uweza wa kuumba na ugonjwa ukaondoka. Yesu alikuwa anatumia maneno kama haya kuponya watu “nataka takasika” uwe mzima” “mtoke mtu huyu” haya ni maneno ya kuumba kama Mungu alivyo tamka “iwe nuru ikawa n.k.” mwanzo 1:1-.. .

6)Ni Mungu mwenyewe.
“hapo mwanzo kulikuwa na neno , naye neno alikuwako kwa Mungu naye neno alikuwa Mungu” Yohana 1:1 ,. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe, kwasababu huwezi kumtofautisha mtu na neno lake , Mungu ni neno na ndio maana sisi tukilishika neno lake tunakuwa washiriki wa tabia ya kiungu “…tupate kuwa washiriki wa tabia ya kiMungu…” 2Petro 1:4,. The Amplified Bible says that “ sharer (per-takers) of divine nature” na kwa namna hiyo tunaitwa miungu “mimi nimesema ndinyi miungu,na wana waa aliye juu wote pia..” Zaburi 82:6. Kumbe tunapata uwezo wa kuumba kwasababu na sisi ni mi ungu kwa kulishika neno lake!

Tunapataje uwezo wa Neno la Mungu!
“hapo mwanzo kulikuwa na neno, naye neno alikuwako kwa Mungu naye neno alikuwa Mungu, . Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa yeye; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima , nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo yang’aa gizani wala giza halikuiweza!” Yohana 1:1-5 ,.


Mambo ya kujifunza kutoka kwenye hilo andiko!
1.) Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe hivyo si la kulifanyia mzaha, kamwe huwezi kumtenganisha mtu na neno lake , ndiyo maana hata Mafalisayo walimtega Yesu kwenye maneno yake ili wamkamate “wakamviziavizia …ili wamnase kwenye maneno yake, wapate kumtia kwenye enzi ya mamlaka ya liwali” Luka 20:20. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe.

2.) Tunajifunza jinsi ya kulitumia neno la Mungu , biblia inasema “ ndani yake ndimo ulimokuwa uzima” ni muhimu kujua kusikia neno tu haitoshi bali kujua kilichoko ndani ya neno hilo, Neno la Mungu lina uzima ndani yake ambao huwezi kuupata kwa kusikia peke yake! Ni kweli kusikia neno la Mungu kunaleta imani(warumi 10:17) lakini imani inatakiwa kuwekwa kimatendo hapo inamaanisha udhihirisho wa neno ulilolipokea na hapa ndipo wakristo wengi wanashindwa kujua na kubaki kumlaumu MUNGU!

3.) Tunaweza kuupokea ule uzima ulio katika neno , kwa kutafakari neno, kivipi basi? Tuchukue mfano wa tundo kama chungwa huwezi kula pamoja na maganda yake ni lazima kumenya maganda kwanza ndipo ule , sasa chungwa ni kama neno la Mungu na maganda ni tafsiri za kibinadamu, Kutafakari neno ni kumruhusu Roho mtakatifu akufundishe kama tulivyoona hapo juu kuwa NENO NI MUNGU, na hakuna anayejua mafumbo ya Mungu isipokuwa Roho mtakatifu, (1wakorintho2:10-11) hivyo Roho hutufunulia kwa kutafakari neno la Mungu Daud akasema “na sheri huitafakari mchana na usiku”

4.) Je wajua kuto kutafakari neno la Mungu ni kumzimisha Roho wa Bwana?
Biblia inasema “ tusimzimishe Roho wa Bwana” 1Thesalonike 5:19 ,. Kuto kutafakari neno la Mungu ni kumzimisha Roho wa Bwana, kwa sababu haumruhusu yeye kukufundisha na huku biblia inasema “Roho atatufundisha kuyashika yote” sasa ni Muhimu kutafakari neno la Mungu kwa kufanya hivyo tunaruhusu uwezo wa Neno la Mungu kutenda kazi katika maisha yetu!

5.) Sasa kwa kutafakari ndipo unapo ingiza uzima kwenye maisha yako, kwenye kazi yako , mafanikio yako (Joshua 1:8) n.k. iyo ndiyo Nuru inayo ng’aa gizani hata giza na wakuu wake hawataiweza kabisa! Jifunze kujiwekea Ratiba ya kusoma neno la Mungu kila siku na kutafakari(meditation) unahusianisha na maisha na kumwomba Roho mtakatifu akufundishe !............................

Shukrani na sifa ni kwa bwana kwa neno lake lipate kupenya ndani ya moyo wako na kuweza kubadilisha maisha ya wengi...
Pia Shukrani za dhati zimfikie mtumishi wa Bwana:

David Mgongolwa Wa New Hope Ministry
E-mail : davidmgongolwa@ymail.com

Imechapishwa Na Kuletwa Kwenu na 
Mathayo Tajiri Ngotee Mchimba Riziki Blog Ceo&Director
lebangotee@yahoo.com

 MAY GOD BLESS YOU



Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score