Thursday, July 31, 2014

Gaza On Fire: Ghaza Katika Lindi La Moto Na Damu

Gaza On Fire
Utawala wa Kizayuni wa Israel leo umeendelea kudhihirisha sura yake halisi ya ugaidi, ukatili na unyama baada ya kushambulia shule nyingine ya Umoja wa Mataifa katika eneo la Jabali huko katika Ukanda wa Ghaza na kuua raia wasiopungua 20 wa Kipalestina.

 Familia nyingi za Kipalestina zimekimbilia katika shule hizo za Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kulinda maisha yao mbele ya mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na jeshi la Israel dhidi ya watu wa Ghaza. Shule hiyo ni ya tatu ya Umoja wa Mataifa kushambuliwa na jeshi la Israel katika mashambulizi ya sasa ya utawala huo haramu katika Ukanda wa Ghaza. Makumi ya wengine wamejeruhiwa.



Habari zinasema kuwa zaidi ya Wapalestina 150 wameuawa shahidi katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza katika mashambulizi ya jana ya jeshi za Israel. Jeshi la Israel linashambulia kwa makombora taasisi za kiraia na kijamii kama shule na vituo vya elimu, misikiti na makanisa, hospitali, vituo vya umeme na maji na kadhalika.


Gaza On Fire
Ni wiki tatu sasa ambapo wakazi wa Ghaza wanakabiliwa na mashambulizi makali ya nchi kavu, baharini na angani ya jeshi la Israel ambalo halikuwaonea huruma hata watoto wadogo, wanawake wajawazito, wazee na vikongwe. 

Ndege za kivita za Israel na walenga shabaha wa utawala huo ghasibu wamekuwa wakiwashambulia watoto wadogo wa Palestina wanaoonekana wakicheza mitaani. Matukio haya, kama yanavyosisitisza mashirika ya kutetea haki za binadamu, ni kielelezo cha jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu. 

Hadi kufikia leo Wapalestina karibu 1290 wameuawa shahidi na wengine zaidi ya 7115 wamejeruhiwa katika siku 23 za mashambulizi ya kinyama ya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.

Raia wa Ghaza ambao wako katika mzingiro wa pande zote wa Israel kwa kipindi cha miaka saba sasa wanakabiliana na utawala huo katili kwa kila walichonacho huku silaha ya watoto wadogo na wanawake ikiwa ni machozi na mayowe. Maeneo yote ya Ghaza yamejaa damu za mashahidi wanaouawa huku karibu kila nyumba ikiwa katika maombolezo ya ndugu, jamaa au rafiki.


Jambo la kusikitisha zaidi kuhusu matukio ya sasa ya Ghaza ni kimya cha jamii ya kimataifa hususan nchi za Ulaya na Marekani ambazo zimekuwa zikijigamba kuwa wabeba bendera ya kutetea haki za binadamu. Nchi za Magharibi hazikuishia katika kunyamaza kimya mbele ya mauaji hayo ya kutisha yanayofanywa na utawala katili wa Israel huko katika Ukanda wa Ghaza, bali zinausaidia utawala huo wa kigaidi kwa silaha zaidi. Kwa kweli yanayotokea Ghaza ni maafa makubwa ya binadamu ambayo doa lake jeusi litabakia milele katika uso wa historia ya mwanadamu.


Ghaza ya leo ni mtihani mgumu kwa Umoja wa Mataifa, Baraza la Usalama, taasisi za kimataifa na nchi zote zinazodai kutetea haki za binadamu zinazoendelea kunyamaza kimya na kushuhudia kwa macho tu jinsi watu wa Ghaza wanavyochinjwa na mashine ya vita ya Israel.


Katika mazingira hayo linajitokeza swali kwamba je, raia wa Ghaza si wanadamu kama wengine wanaopaswa kudhaminiwa usalama na amani? Je, ni jumuiya na taasisi gani zinazopaswa kuwadhaminia usalama na amani? Ni nini majukumu ya wajibu wa Umoja wa Mataifa la Baraza lake la Usalama katika hali ya sasa ambapo watoto wadogo wasio na dhambi na wanawake wa Ghaza wanaendelea kuchinjwa na kuuawa kama wadudu wasio na thamani?  


Wednesday, July 30, 2014

Hatimaye Mkenya Wa Pili Atua Ligi Kuu England.... Atashiriki Michuano Mikubwa Ya UEFA

Divork Origi Na Sakfu Ya Liverpool.

London: Hatimaye, klabu ya Liverpool imemsajili mshambuliaji wa chipukizi, Divock Origi Mkenya/Mbelgiji akitokea Klabu yake ya Lille aliyojiunga nayo akiwa na miaka 15.

Mchezaji huyo mwenye miaka 19 ameukubali mkataba wa miaka mitano lakini ataendelea kubaki kwenye klabu yake huko Ufaransa kwa mkopo katika msimu ujao kabla ya kuhamia Anfield mwaka ujao 2015.

“Ninayo furaha kwa klabu kubwa kama Liverpool imenisajili,” Origi alisema.
Origi alicheza mechi zote tano za Ubegiji katika fainali za Kombe la Dunia la mwaka huu wakati wakipigana kuelekea robo-fainali na kuifungia timu yake bao dhidi ya Urusi.
Mbali na Origi, Liverpool pia imewanunua Rickie Lambert, 32, akitokea Southamptom na kiungo wa wa kati Adam Lallana, 25,  kutoka Southampton.
Kadhalika imewanasa Emre Can, 20 akitokea Bayer Leverkusen na winga Lazar Markovic, 20, akitokea Benfica.
Mlinzi Dejan Lovren, 25 akitokea Southamptom pia amehamia Anfield.
“Najua hii ni klabu yenye historia kubwa, wachezaji wakubwa  na mashabiki wengi,” aliongeza.
“Kwangu Liverpoool ni moja ya vilabu bora kabisa duniani na ninayo furaha sana kuwa sehemu ya historia hii.
Origi ambaye asili yake ni Kenya alianzia katika klabu ya Genk alichochezea babake, Mike Okoth kabla ya kuhamia Lille.


TETESI ZA SOKA ULAYA

Beki was Aston Villa Ron Vlaar, 29, atakuwa
 na mazungumzo na meneja wake Paul Lambert kuhusiana na hatma yake licha ya Southampton kumwania (Daily Mirror), QPR wanafikiria kumchukua kiungo wa Colombia Carlos Sanchez, 28, kwa pauni milioni 4 kutoka Elche (Daily Mirror), West Ham na QPR wamepanda dau kwa Marseille kumchukua Matheiu Valbuena baada ya kiungo huyo Mfaransa kukataa kuhamia Dynamo Moscow (L'Equipe), Manchester United na Barcelona bado wanamfuatilia Juan Cuadrado, 26, wa Fiorentina lakini huenda wakatishwa na bei ya pauni milioni, 32, ya kiungo huyo kutoka Colombia (Marca), Manchester United wamefikia makubaliano "ya mdomo" na kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, ya uhamisho wa pauni milioni 47 (Tuttosport), matumaini ya Manchester City kumsajili beki kutoka Morocco Mehdi Benatia, 27, yamefifia baada ya Roma kusema hakuna dalili za mchezaji huyo kuondoka (Le Figaro), meneja mpya wa Manchester United amewaonya mashabiki wake kuwa timu hiyo huenda ikasuasua katika miezi mitatu ya mwanzo wa msimu wakati wachezaji wakianza kuzoea mbinu zake (Times), Van Gaal amesema iwapo watashinda Ligi Kuu msimu ujao na kuwapiku majirani zao Manchester City, utakuwa ushindi "mtamu" zaidi (Manchester Evening News), kiungo wa Manchester City Yaya Toure, 31, amesema huenda akasalia katika timu hiyo hadi atakapoacha kucheza soka (Guardian), mshambuliaji mpya wa Barcelona Luis Suarez, 27, ambaye anatumikia adhabu ya miezi minne, amehamia katika mji wa Pyrenees kuanza mazoezi ya msimu mpya akiwa na mwalimu binafsi (Daily Mail), Didier Drogba, 36, amesema Diego Costa, 25, atakuwa mchezaji "mkali" katika Ligi Kuu ya England (Sun), AC Milan wanafanya mazungumzo wa mshambuliaji kutoka Brazil Robinho, 30 (Le Figaro), kiungo wa Arsenal Santi Cazorla,29, bado anasakwa na Atlètico Madrid. Atlètico pia wanamfuatilia Fernando Torres, 30, na winga wa PSV Eindhoven Zakaria Bakkali, 18 (AS.com), kiungo anayefuatiliwa na Liverpool, Xeridan Shaqiri, 22, huenda akaamua kubakia na klabu yake ya Bayern Munich (Tuttosport), Borussia Dortmund na Schalke wanamtaka mshambuliaji kutoka Serbia, Aden Ljajic, 22, kutoka AS Roma (Bild), Barcelona wametangaza kumsajili kiungo kutoka Brazil, Alex Varoneze Dione anayejulikana kama "Betri" kwa miaka mitatu (Mundodeportivo), Manchester United wameanza tena kumfuatilia beki wa kati wa Atletico Madrid Miranda, baada ya Atlètico kusema wapo tayari kupokea dau la pauni milioni 23 (Metro), AC Milan wanamtaka winga wa Newcastle Hatem Ben Arfa na huenda akauzwa kwa pauni milioni 12 (Daily Star), Bayern Munich wapo tayari kusubiri hadi Oktoba kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdez ambaye anauguza jeraha la goti, ingawa anaweza kusita kwenda kugombea namba na Manuel Neuer (Mundo Deportivo), QPR wanataka kumchukua Ronaldinho ambaye amemaliza mkataba wake na Atletico Mineiro (Globoesporte) na Chelsea wanakataa kutengeneza jezi zenye jina la kipa Thibaut Courtois, 22 na Romelu Lukaku, 22, kwa sababu wachezaji hao bado hawajapewa namba (Daily Star).

SHUJAA ALIYEAMBUKIZWA UKIMWI KULIPWA KSH MILLIONI 653........

Mwathiriwa mmoja wa bomu la 1998 atapata Sh652.5 milioni kama fidia baada ya kuambukizwa virusi vya HIV akijaribu kuwaokoa manusura katika shambulizi hilo la kigaidi.

William Maina alikuwa akichokoa vifusi vya jengo la Ubalozi wa Amerika, ambalo liliharibiwa kabisa na shambulizi hilo.


Alishuhudia mbele ya mahakama moja ya Amerika kwamba alikuwa akifanya kazi kando na ubalozi huo wakati wa shambulizi, na alikimbia eneo la mkasa kusaidia katika juhudi za uokoaji.
Ni katika shughuli hizo za kuwasaidia wahasiriwa ambapo alipata majeraha na mikwaruzo iliyofanya damu yake kuchanganyika na ya wahasiriwa.
Bw Maina baadaye alipatikana kuwa na virusi vya HIV ambavyo husababisha ugonjwa wa Ukimwi. Alitoa ushahidi mahakamani kuonyesha hakupata ugonjwa huo kwingine.
“Ingawa alikuwa na majeraha madogo tu ya kimwili wakati wa juhudi za uokoaji, HIV ni ugonjwa sugu, hatari na wenye kusababishia mtu fedheha unaohitaji matibabu ya maisha,” Jaji wa Amerika John Bates alisema katika uamuzi wake.
Mwathiriwa mwengine Jael Oyoo pia alifidiwa. Bi Oyoo alitolewa kwenye vifusi na waokoaji na alipata majeraha mabaya ya moto usoni na kichwani. Waokoaji walidhania alikuwa amefariki.
Kadhalika, alipoteza uwezo wa kuona katika jicho lake la kushoto na kuathiri mno kuona katika jicho la kulia. Alikuwa hospitalini kwa miaka miwili.
Wawili hao ni miongoni mwa waathiriwa wa shambulizi hilo la bomu dhidi ya ubalozi wa Amerika mjini Nairobi, waliofidiwa baada ya kupata majeraha mabaya.
Waliopoteza waume au wake zao watapata kiasi cha hadi Sh696 milioni. Wengine watapewa Sh609 milioni.

Katika uamuzi wake, Bw Bates alitoa Sh435 milioni kwa waathiriwa wa majeraha mabaya ya kimwili, kwa mfano kuvunjika sehemu za mwili, maumivu ya nyama na makovu pamoja na waaathiriwa wa kisaikolojia.

Iwapo uchungu wa kimwili na kisaikolojia ni mwingi sana – kama waathiriwa waliopata majeraha mengi na mabaya na waliopoteza uwezo wa kuona na kusikia ama waliodhaniwa kuwa wamefariki – mahakama imetoa hadi dola milioni saba (Sh609 milioni) na zaidi,” Bw Bates alisema katika kesi iliyowasilishwa na Milly Mikali na wengine.
Walikuwa wameshtaki Jamhuri ya Sudan kwa shambulizi hilo la kigaidi.
Lakini kwa waliopoteza wake au waume zao, Jaji alisema watapewa Sh696 milioni kama fidia ya wapenzi wao waliopoteza maisha.
Aidha, kwa waathiriwa waliopata majeraha ya kiakili kuandamana na majeraha madogo ya kimwili, Jaji aliamua watalipwa kati ya Sh130 milioni na Sh261 milioni. Kwa waliokuwa na majeraha kwa saa kadha, watapata fidia ya Sh87 milioni.
Iwapo kipindi cha maumivu ni kidogo atapata pesa kidogo. Kwa mfano, aeleza jaji, waliokuwa na majeraha kwa dakika 10 watapata Sh43 milioni.

Source Taifa Leo

Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score