Saturday, April 26, 2014

Tani Moja Ya Heroin Yakamatwa Na Wanajeshi Wa Austrilia Katika Pwani Ya ....................


Madaya Ya Heroin Yaliyokamatwa. Inasemekana ni zaidi ya Tani moja.
Jeshi la Wanamaji la Australia lilikamata magunia 46 ya heroin yenye thamani ya dola milioni 290 (shilingi bilioni 25 za Kenya Sh) kutoka kwenye meli iliyokuwa ikisafiri katika Upwa ya Kenya, lilitangaza Shirika la Habari la Australia jana siku ya Ijumaa (tarehe 25 Aprili).


Mabaharia wa meli ya HMAS Darwin waliingia kwenye boti walioishuku na kugundua madawa yaliyofichwa kwenye mifuko ya saruji.

"Madawa haya sasa yameshikiliwa na na yameharibiwa hapo jana na wanajeshi wa Australia," alisema kamanda Terry Morrison. "Inafahamika vyema kwamba madawa haya yanayasaidia makundi ya kigaidi kifedha ili waweze kufanya matendo yao ya kigaidi."

 Meli hiyo ya Darwin imetumwa kwenye Pembe ya Afrika kama sehemu ya Operesheni Slipper, mchango wa Australia kwenye juhudi za kimataifa za kupambana na ugaidi, ulanguzi na uharamia kwenye eneo la bahari la Mashariki ya Kati.
Meli Iliyokuwa Imebeba Madawa Hayo. HMAS

Thursday, April 24, 2014

Mourinho achanganyikiwa Ni kutokana na mechi mbili ngumu mbele yake.. Kikosi chake kinamajeruhi wengi..Tizama alichokisema Mreno huyo.


KOCHA wa Chelsea Jose Mourinho yuko kwenye njia panda kuhusu wachezaji atakaotumia kwa mechi dhidi ya Liverpool Jumapili na Atletico Madrid Jumatano ijayo.
Kocha Wa Chelsea
Jose Mourinho
Hii ni kutokana na kuwa wanasoka wanne watakosa mechi ya marudiano dhidi ya Atletico Madrid juma lijalo ya kufuzu kwa fainali ya Uefa. Baada ya kutoka sare 0-0 nchini Uhispania Jumanne ni lazima Chelsea washinde uwanjani Stamford Bridge katika mechi ya marudiano la sivyo ikose kufuzu kwa fainali.

Hata hivyo jitihada hizo huenda zikavurugwa na hatua ambako kipa nambari moja Petr Cech na difenda John Terry waliumia katika mechi ya Jumanne na watakosa mechi ya marudiano. Nao Frank Lampard na John Obi Mikel walipata kadi za manjano na vile vile watakosa mechi hiyo.
Kocha Mourinho ametisha kuchezesha timu dhaifu dhidi ya Liverpool Jumapili ijayo ili kuokoa nafasi zake kufika fainali ya Uefa.
Mbali na wanne hao, Chelsea pia itakosa huduma za straika Samuel Eto’o na kiungo shupavu Eden Hazard ambao pia wana majeraha.
“Msimu wa Cech umeisha kwani atachukua muda mrefu kupona na kwa Terry, itatulazimu tucheze hadi fainali ili apate nafasi nyingine ya kuonja soka ya Uefa,” Mourinho alisema baada ya mechi hiyo.
Vijana hao watakutana na Liverpool yenye ari kuu ya kushinda taji kwa mara ya kwanza tangu 1990.
Chelsea inashikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa alama 75, tano nyuma ya Liverpool ambayo ina alama 80 huku zikiwa zimesalia mechi tatu pekee msimu kumalizika.

Msimamo Wa Ligi kuu England Ulivyo kwa sasa.

  1. English Premier League
    Standings
    #
    Team
    GP
    W
    D
    L
    GF
    GA
    GD
    PTS
    1
    35
    25
    5
    5
    96
    44
    52
    80
    2
    35
    23
    6
    6
    67
    26
    41
    75
    3
    34
    23
    5
    6
    91
    35
    56
    74
    4
    35
    21
    7
    7
    62
    41
    21
    70
    5
    35
    20
    9
    6
    57
    34
    23
    69
    6
    35
    19
    6
    10
    51
    49
    2
    63
    7
    34
    17
    6
    11
    56
    40
    16
    57
    8
    35
    13
    10
    12
    50
    45
    5
    49
    9
    35
    14
    4
    17
    39
    54
    -15
    46
    10
    35
    11
    11
    13
    39
    49
    -10
    44
    11
    35
    13
    4
    18
    28
    41
    -13
    43
    12
    35
    10
    7
    18
    38
    48
    -10
    37
    13
    35
    9
    9
    17
    47
    51
    -4
    36
    14
    34
    10
    6
    18
    34
    43
    -9
    36
    15
    34
    9
    8
    17
    35
    49
    -14
    35
    16
    34
    6
    15
    13
    41
    54
    -13
    33
    17
    35
    8
    8
    19
    28
    56
    -28
    32
    18
    35
    7
    9
    19
    31
    65
    -34
    30
    19
    35
    9
    3
    23
    35
    77
    -42
    30
    20
    34
    7
    8
    19
    33
    57
    -24
    29

Ukabila Huu Utaisha Lini Afrika? Cheki Kiongozi Mkubwa AliyeKataa Kujibu Swali La Mwanahabari kisa Ukabila...

Kiongozi wa chama cha Wiper aliye pia mmoja wa vinara wa Cord Kalonzo Musyoka alichemka na kukataa kujibu swali la mwanahabari kwa misingi ya jina lake la ukoo.
Kalonzo Musyoka Akimwomba Murethi Mwaandishi Wa
 Habari Msamaha baada ya kukataa kulijibu swali lake
Bw Musyoka alilazimika kutuma taarifa baadaye kuomba msamaha kwa kutoa matamshi hayo.

“Ilikuwa utani lakini nigependa kumwomba msamaha, pamoja na wanahabari wengine wote na mtu yeyote yule aliyeudhika na matamshi hayo,” taarifa hiyo iliyotumwa na msaidizi wake Dennis Kavisu ilisema.
Tukio hilo lililoshangaza wengi wakati wa kikao cha wanahabari kilichoandaliwa na muungano huo Nairobi kilipelekea Wakenya wa tabaka mbalimbali kueleza hasira yao katika mtandao wa kijamii wa Twitter.
Wakati wa mahojiano baada ya Cord kutoa ripoti yake kuhusu utawala wa mwaka mmoja wa Serikali ya Jubilee, mwanahabari wa runinga ya Q TV inayomilikiwa na Nation Media Group, Bw Kennedy Mureithi aliuliza ni kipi ambacho upande wa upinzani umefanya hadi sasa kushauri Serikali.
Mureithi: Yale ambayo mumekuwa mkisema ni kuhusu makosa ya Serikali ingawa hamjatoa mwongozo mbadala kama Cord. Hamsemi ‘hili ni baya, hili ndilo linafaa kufanywa’.  

Video Ndio Hii Hapa Chini


Musyoka: Kwanza sikupata jina lako.
Mureithi: Jina langu ni Kennedy Mureithi kutoka Nation Media, QTV.
Musyoka: Asante Kennedy…hilo jina limekusaliti kabisa…
Ingawa aliendelea kuongea, matamshi yake hayakusikika kutokana na kicheko cha baadhi ya waliokuwepo, pamoja na jinsi kaimu kiongozi wa ODM Anyang’ Nyong’o na mbunge wa Budalangi Ababu Namwamba walivyoingilia kati kwa haraka na kueleza swali hilo lilikuwa limeangaziwa tayari.
Hisia tofauti zilitolewa na Wakenya wa tabaka mbalimbali katika Twitter, ambapo wengi walimshutumu Bw Musyoka huku wengine wakionekana kutetea matamshi yake.
“Kwa kweli sina la kusema. Sijui hata nianzie wapi,” alisema mwanahabari mashuhuri wa runinga ya Citizen, Bi Julie Gichuru.
Mwanahabari mwingine, Bi Isha Chidzuga wa runinga KTN alisema, “Kuna sababu ya kuwepo kwa msemo ‘No comment’. Imenuiwa kukuokoa. Jikwae dole wala sio ulimi.”


Waliomtetea walisema Wakenya hujifanya tu kukemea ukabila ilhali wao wenyewe ni wakabila.
“Amen. Wanahabari pia walihusika kugawanya Kenya kikabila mbali na kuwa walituuza kwa chai na mandazi,” alisema Bi Noreen Auma kwenye Twitter.
Kwa upande wake, Geoffrey Nyambane alitaja yaliyokuwa yakiendelea mtandaoni kama kutotaka kutambua ukweli na akasema cha muhimu ni “kukabiliana na tatizo halisi ambalo ni ukabila Kenya.”
Kwenye kikao hicho, Bw Musyoka alitoa wito kwa Serikali ikabiliane na ukabila ambao ni tishio kwa umoja wa kitaifa.



Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score