Friday, July 25, 2014

Viongozi Wa Sasa Bavicha Hawana Sifa Tena Ya Kugombea.

Dar es Salaam. 
John Heche Mwenyekiti Bavicha Taifa 
Viongozi wote wa juu wa sasa wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) hawatagombea nafasi yoyote katika baraza hilo kutokana na umri wao kuzidi miaka 30.
Kwa mujibu wa katiba ya Bavicha, mgombea wa nafasi yoyote anatakiwa asiwe na umri wa zaidi ya miaka 30.
Mwenyekiti wa Bavicha, John Heche alisema jana kuwa yeye, Katibu Mkuu wake, Deogratius Munishi na Naibu Katibu Mkuu, Ester Daffi hawatagombea nafasi yoyote kutokana na umri walionao... “Hii ina maana kuwa baada ya uchaguzi, tutaachia madaraka na kuendelea na shughuli nyingine za chama.”
Alisema ili kuepuka udanganyifu hususan wa umri miongoni mwa wagombea wengine katika nafasi mbalimbali za baraza hilo, watahakikisha wanasimamia suala hilo kwa umakini mkubwa.
Heche alisema uchaguzi wa Bavicha katika ngazi ya taifa utafanyika Septemba 10, mwaka huu na fomu zitaanza kutolewa kuanzia Agosti 10 hadi 25 mwaka huu.
Alisema nafasi zitakazogombewa katika uchaguzi huo ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti bara na Zanzibar na katibu mkuu.
Nyingine ni naibu katibu mkuu bara na Zanzibar, mratibu mhamasishaji taifa, mweka hazina na wajumbe watano wa kuwakilisha kwenye baraza kuu la chama na wajumbe 20 wa  kuwakilisha vijana kwenye mkutano kuu wa chama hicho.
Rushwa
Akizungumzia suala la rushwa katika uchaguzi, Heche alisema uongozi unaomaliza muda wake umejipanga kudhibiti vitendo hivyo ili kuzuia wasaliti kujipenyeza.
Alisema kuna baadhi ya watu wamejipanga kutoa rushwa ndani ya baraza hilo ili kushinda nafasi mbalimbali kwa lengo la kuivuruga Chadema baadaye na kuidhoofisha.
Alisema chama hicho kitawawinda wagombea hao na kuwafisha katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili wachukuliwe hatua za kisheria na baadaye kufutwa uanachama.
Mwaka 2011, Bavicha ilifanya uchaguzi ambao ulitawaliwa na mizengwe na vurugu hadi kusababisha kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea.
Mwananchi Source

Tuesday, July 22, 2014

Saratani Ya Koo Na Tumbo Husababishwa Na Pombe Za Kienyeji Kama Busaa.

Wazee wakifurahia Busaa Picha kwa Hisani Ya Nation Mediu Group
Wanasayansi wameitaka kuangazia unywaji busaa wakisema unachangia pakubwa ongezeko la visa vya saratani ya koo.
Ripoti hiyo inasema ingawa kinywaji hicho ni maarufu sana hapa nchini katika jamii mbalimbali utumiaji wa mahindi, mawele na mtama au mhogo ulioharibika kutengeneza busaa unachangia pakubwa katika kuwapa sumu wanywaji ambao mwishowe hupata magonjwa mbalimbali ukiwemo saratani ya tumbo na koo.

Wanasayasi watatu kutoka Chuo Kikuu cha Kiteknolojia cha Jomo Kenyatta(JKUAT), mmoja kutoka Chuo Kikuu cha Chiba kule Japan na mwingine kutoka Kituo cha Utafiti wa Maswala ya Afya (KEMRI) wanasema udadisi umeonyesha kemikali zinazochangia usambazaji wa saratani zinapatikana katika pombe iliyonunuliwa katika vituo mbali mbali vya vileo kule Bomet.
Wadadisi waligundua kuwa wagema wana mazoea ya kutumia mahindi yaliyooza ambayo huuzwa kwa bei ya chini na wauzaji na hivyo kufanya wanywaji pombe kupata sumu iliyo ya hali ya juu.
“Kuna haja ya kutumia mahindi masafi na bidhaa nyingine katika kutengeneza pombe lakini mambo yalivyo, tunaona wagema wakipendelea kutumia mahindi yaliyooza na kutengeneza busaa ambayo baadaye hupewa wanywaji katika sherehe za mazishi, harusi, ulipaji mahari na wakati wa kutahiriwa kwa wavulana,” ikasema ripoti hiyo.
“Kemikali hizi humfanya mnywaji kupoteza uzito, kutapika mara kwa mara na pia kuhara. Lakini baada ya muda mrefu, mwili hupoteza uwezo wake wa kuzuia magonjwa na mtu akapata saratani ya koo au matumbo,” ikasema ripoti hiyo.

Hali ya wabugiaji pombe huwa mbaya zaidi kwani wao hunywa hapa na kisha kunywa pale na hii inawafanya kuwa hatarini ya kunywa sumu aina mbalimbali na hivyo kuhatarisha maisha yao zaidi.
Inaonya kuwa wagema wengine sasa wameanza kutumia chakula ya mifugo ambacho kina sumu kali na hivyo kufanya wanywaji kunywa mvinyo wenye sumu aina mbali mbali.
Wanasayansi hao, Mary Kirui, Amos Alakonya na Keith Talam-wote kutoka Chuo cha JKUAT ,Bi Christine Bii(KEMRI) na Gonoi Tohru wa Chiba wanaamini kuna haja ya serikali kuangalia ubora wa Busaa mara kwa mara ili kuinua hali ya wabobeaji pombe.

Mourinho Anena Juu Ya Ujio Wa Van Gaal Manchester United. Amwambia............



Kushoto Ni Jose Mourinho akimtania Kocha Man U Van Gaal Kulia.
Kocha wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho, amejitanua kifua kwamba hamwogopi  mkufunzi mpya wa Manchester United, Louis Van Gaal wakati msimu mpya unapozidi kukaribia kuanza.
Wawili hao ambao ni marafiki wakubwa waliwahi kufanya kazi pamoja katika klabu ya Barcelona, Mourinho akiwa mkalimani na mwenzake kocha.

Makocha hawa wawili wana mafanikio makubwa kwenye taaluma yao ya ukufunzi  japo hawajawahi kujipata katika ushindani zaidi ya mwaka wa 2010 walipokutana kwenye fainali ya dimba la klabu bingwa Ulaya.
Wakati huo Mourinho alikuwa akiifunza Inter Milan ya Italia naye Van Gaal akinoa Bayern Munich ya Ujerumani. Timu hizo zilikutana kwenye fainali hizo na  Mourinho akaibuka kidedea kwa kutwaa ubingwa.
Mwaka huu, watagongana vichwa kwenye Ligi Kuu ya Uingereza ambapo Van Gaal ameapa kujaribu kushinda taji katika msimu wake wa kwanza akiwa uongozini huku naye mwenzake akisisitiza wazo sawa na hilo.
“Sina wasiwasi kwamba kwa sasa yupo hapa. Mwanzo ninatamani sana kukutana na United na wala sioni cha kunipa hofu. Hii ni kwa sababu sisi sote ni makocha wazuri na ninachojua ni kuwa ataisaidi Manchester United,” Mourinho alisema.
“Van Gaal kwa mtazamo wangu ndiye aliyekuwa kocha bora wa dimba la dunia na ni mtu ninayemheshimu sana kutokana na urafiki wetu mkubwa wa siku nyingi. Ila pamoja na yote, katika ushindani kila mmoja atajisimamia,” aliongeza.
Van Gaal alianza majukumu yake mapya klabuni humo juma lililopita na tayari ameapa kuirejesha United kwenye hadhi yake ya ushindani ligini baada ya kumaliza ya saba msimu uliopita chini ya ualimu wa David Moyes aliyepigwa kalamu.
Kwa sasa Van Gaal yuko na kikosi hicho jijini Miami, Marekani anakokitayarisha kwa mechi kadhaa za kirafiki. Kwa wakati huo huo anaendelea kufanya usajili ili kukirutubisha kikosi hicho hata zaidi.

Mkataba Wa Vana Gaal
Mkufunzi huyo alitia saini kandarasi ya miaka mitatu na United na mechi yake ya kwanza ya Ligi inayoanza Agosti 16, itakuwa dhidi ya Swansea siku mbili kabla ya Chelsea kuanza kampeni yao vile vile dhidi ya Burnley iliyopandishwa daraja.
Tetesi Za Usajili
Boss wa Manchester City Manuel Pellegrini anapanga kumchukua Didier Drogba, 36, ambaye pia anasakwa na klabu yake ya zamani Chelsea (Daily Star), meneja wa Manchester United Louis van Gaal anataka kutoa pauni milioni 17 kumchukua beki mkabaji wa Ajax Daley Blind, 24 (Daily Express), United pia wameripotiwa kuwa karibu kumsajili beki wa kati wa Borussia Dortmund Mats Hummels, 25, kwa pauni milioni 16 (Daily Mail), Tottenham wameambiwa watoe pauni milioni 25 kama wanamtaka kiungo wa Real Sociedad Antoine Griezmann, 23, ambaye pia anafuatiliwa na Chelsea na Monaco (Daily Telegraph), boss wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hatosajili mshambuliaji msimu huu na hivyo kufuta tetesi zinazomhusisha na Mario Balotelli wa AC Milan (Daily Mirror), kiungo wa Ureno Thiago Mendes, 23, ametupilia mbali uwezekano wa kurejea Chelsea na angependa kusalia Atletico Madrid miaka miaka mingine miwili (Daily Express), PSG watakwepa sheria za Fifa za fedha kwa kumchukua Angel Di Maria, kwa mkopo kwa mwaka mmoja kutoka Real Madrid. Di Maria anasakwa pia na Man United (Daily Express), Arsenal, Chelsea na Man United wanamtaka beki Reece Oxford, 15, baada ya kinda huyo kuonesha kipaji msimu uliopita akiwa na West Ham ya vijana (Daily Star), Arsene Wenger atamruhusu Thomas Vermaelen kwenda Manchester United, ikiwa tu atarhusiwa kumchukua Phil Jones au Chris Smalling (Daily Mirror), Chelsea watampa Didier Drogba mkataba wa miezi 12 wa kucheza ambao hautakuwa na kipengele cha kuwa kocha, ingawa Chelsea wapo tayari kuzungumzia hilo (Daily Telegraph), mshambuliaji wa Lille Divock Origi anakwenda Boston Marekani kuungana na Liverpool ambao wapo katika ziara ya mechi za kabla ya msimu. Atafanyika vipimo kabla ya kukamilisha uhamisho wake wa pauni milioni 10. Huenda pia akarejeshwa Lille kwa mkopo (Daily Star).



Monday, July 21, 2014

Mkenya Aliyecheza World Cup Kutua Liverpool

Liverpool inakaribia kufikia maafikiano na klabu za Southampton kumnunua beki Dejan Lovren na klabu ya Lille ili kupata saini ya mshambuliaji Mkenya Divock Origi.
Divorck Origi

Kulinganana BBC, The Reds ambao kwa wakati huu wako ziarani nchini Marekani wameripotiwa kufikia makubaliano na Lille kumsajili Origi raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Kenya kwa dau la Sh1.5 bilioni. Kwa wiki kadhaa sasa Liverpool imekuwa ikimsaka mshambuliaji huyo huku kukichapishwa ripoti kadhaa za maafikiano baina ya pande zote ila taarifa hizo hazijawahi kuwa rasmi.
Kumhusu mlinzi Lovren mwenye umri wa miaka 25, Liverpool waliwasilisha ofa ya Sh3 bilioni juma lililopita ila ilikakataliwa. Hata hivyo Lovren raia wa Croatia ameelezea nia yake ya kutaka kuhamia Liverpool hatua ambayo imeanza kuwafanya Southampton kuwaza mara mbili.
Mlinzi huyo amewasilisha barua kwa klabu hiyo ya kuwataka wamruhusu aondoke ikiwa ni baada ya kutumikia mwaka mmoja wa mkataba wake wa miaka minne nao.
Liverpool ambao watashiriki Ligi ya mabingwa msimu ujao kwa mara ya kwanza tangu 2009, wamekuwa wakikirutubisha kikosi chao na hadi kufikia sasa baada ya kuondoka kwa nyota wao Luis Suarez aliyetua Barcelona, wamefanikiwa kuwasajili wachezaji sita.

Mshambuliaji Loic Remy alijiunga nao Jumapili baada ya klbu ya QPR kukubali ofa yao ya Sh1.2 bilioni. Kando na mchezaji huyo, kocha Berndan Rodger ameanunua Adam Lallan, Rickie Lambert, Lazar Markovic na Emre Can...

Kwa tetezi nyingi za soka usikose kujiunga nasi kila mara....

Nilijaribu Kutoa Mimba Ya Ronaldo "Maria Dolores Dos Santos Averiro" Ni Mama Wa Cristiano Aliyasema Hayo Katika Uzinduzi Wa Kitabu Cha Historia Yake.


LISBON, Ureno

Maria Dolores Dos Santos Averiro Mama Yake Ronaldo

Mama yake mchezaji bora duniani Cristiano Ronaldo, amefichua siri kwamba alijaribu kuavya/Kutoa mimba alipokuwa akitarajia kujifungua mwanasoka huyo miaka 29 iliyopita.

Katika kitabu chake kilichozindulia siku za hivi karibuni, Dolores Aveiro anaeleza kuwa daktari wake aliyekuwa akimshughulikia wakati wa ujauzito huo, aligoma kumsaidia katika jitihada zake za kutoa mimba.

Kuona hivyo, Dolores aliamua kuifanya mwenyewe nyumbani alipoanza tabia ya kunywa pombe yenye joto na kisha kushiriki mazoezi makali kupita kiasi akiwa na wazo kwamba hatua hiyo ingepelekea mimba ya Cristiano kucharuka


“Nilitaka kutoa mimba lakini daktari hakuniunga mkono kabisa. Hivyo nilianza kunywa pombe yenye uvuguvugu na kisha kukimbia mpaka pale nilipozirai ila jitihada zote hizo za kutoa ujauzito ule haukufua dafu,” Dolores anaeleza kwenye kitabu hicho cha wasifu wake.

Pamoja na yote mama huyo anakiri kwamba baadaye mwanawe alikuja kubaini ukweli wa mambo na badala ya kuwa na machungu naye, amekuwa akimfanyia utani tu kwa tendo lake hilo ambalo huenda lingemnyima nafasi ya kuwa mwanasoka maarufu zaidi Duniani jinsi alivyo sasa.

“Alipogundua nilichojaribu kufanya, alikuja na kunieleza haya, 'mama hebu tazama, ulitaka kuniavya ila sasa ni mimi ndiye ninayekimu familia nyumbani”. Ronaldo alimwambia mama yake

Mbali Na Hayo 


Kwa wakati huo straika wa zamani wa klabu ya Arsenal na taifa la Ufaransa, Thiery Henry ameibua mjadala ambao umekuwepo kwa siku nyingi wa ni nani mkali zaidi kati ya Lionel Messi na Cristiano.
Wachezaji wote hawa ambao wameshinda mataji ya wachezaji bora duniani Ballon d’Or, Messi anayeisakatia klabu ya Barcelona akiibeba mara nne naye Cristiano akitawazwa mara mbili, wamekuwa wakiwagawanya wadau wengi.
Kulingana na Henry, kando na mambo mengine uwanjani hasa ufungaji mabao, Cristiano hana talanta na kipaji cha kweli kinachoweza kulinganishwa na kile cha Messi.

Cristiano Ronaldo



Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score