Friday, February 21, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013 YATANGAZWA.

Necta


Matokeo ya kidato cha 4 mwaka 2013 yametangazwa, ufaulu umeongezeka kwa asilimia kati ya 0.61 na 16.72 ukilinganisha na mwaka 2012.


 Jumla ya watahiniwa 427,679 waliandikishwa kufanya mtihani ila waliofanikiwa kufanya mtihani ni watahiniwa 404,083.

Jumla ya watahiniwa laki 235,227 sawa na asilimia 58.25 ya waliofanya mtihani wamefaulu.

Wasichana waliofaulu ni laki 106,792 na wavulana waliofaulu ni laki 128,435.

 Jumla ya wanafunzi laki 151,187 wamepata '0' (division ziro) . Wasichana ni 72,237 na wavulana ni 78,950.

Jumla ya wanafunzi waliopata daraja la 4 (division 4) ni laki 126,828, wasichana wakiwa 62,841 na wavulana 63,987.

Wavulana waliopata daraja la tatu (Division 3) ni 27,904 na wasichana ni 17,113.

Waliopata daraja la pili (Division 2) Wavulana ni 14,167 na wasichana ni 7,561.

Wavulana waliopata daraja la kwanza (division one) ni 5,030 na wasichana ni 2,549.

Shule 10 zilizoongoza ni: St.Francis Girls, Marian Boys, Feza Girls, Precious Blood, Canossa, Marian Girls, Abbey

Shule kumi zilizoongoza: Anwarite Girls, Rosmini, na DonBosco Seminary.

Zilizofanya vibaya ni: Kisima, Kitongoni, Tongani, Njechele, Lumemo, Mvuti, Tambani, Nasibugani, Ungulu, Kitonga, Singisa, Hurui, Barabarani, Nandanga, Vihokoli, Chongoleani, Likawage, Gwandi, Rungwa, Uchindile.

Watahiniwa kumi bora ni: 1. Robina S. Nicholaus (Marian Girls), 2. Magreth Kakoko (St.Francis Girls), 3. Joyceline Leornard Marealle (Canossa), 4. Sarafina W. Mariki (Marian Girls), 5. Abby T. Seembuche (Marian Girls), 6. Sunday Mrutu (Anne Marie), 7. Nelson Anthony (Kaizerege), 8.Emmanuel Gregory (Kaizerege), 9. Janeth Urassa (Marian Girls) na 10. Angel Ngulumbi (St Francis)

Baraza limefuta matokeo ya watahiniwa 272 waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani yao.

Bonyeza Linki hii Kuona Matokeo Yote
Matokeo Bonyeza Hapa

Mchimba Riziki

Wednesday, February 19, 2014

Pasta Afariki Dunia Kwenye Chumba Chaa Mwanamke.

Hali ya taharuki ilikumba mtaa wa Buruburu, Nairobi baada ya mwili wa kasisi kupatikana katika chumba cha kulala cha mwanamke aliyesemekana kuwa muumini wa kanisa la pasta huyo.

Estate Za Buruburu Nairobi
Kasisi huyo mwenye umri wa miaka 70 alisemekana kutembelea mwanamke huyo katika mtaa wa Buruburu Phase 1 mwendo wa saa tano asubuhi na kukaa ndani ya chumba hicho siku nzima.

Maafisa wa polisi walisema mwili wa kasisi Geoffrey Maingi ulipatikana bila majeraha yoyote.
Mkuu wa Polisi wa Buruburu Richard Kerich alisema kasisi huyo anayehudumu katika kanisa la Redeemed Gospel Buruburu aliliegesha gari lake katika duka la Tuskys mtaani humo kabla ya kuelekea kwa mwanamke huyo.

Mwanamke mwenye chumba hicho alisema kasisi huyo alikuwa ameenda kumuombea na kuongeza kuwa hakujua iwapo alikuwa mgonjwa.

“Si mara ya kwanza kwake kuja tushiriki maombi pamoja. Amekuwa akinitembelea mara kwa mara,” alisema mwanamke huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 40 aliwaambia polisi kuwa kasisi huyo alianguka ghafla na kufariki.
“Kando na kuwa pasta wangu yeye pia ni rafiki na ndio maana huwa tunashiriki maombi pamoja,” akasema

Jirani wa mwanamke huyo alithibitisha kuwa kasisi huyo amekuwa na ziara kadhaa chumbani humo.

Tukio hilo lilivutia umati mkubwa huku baadhi ya wakazi wa mtaa huo wakidokeza kuwa huenda kifo cha pasta huyo kilitokana na matumizi ya dawa za kuongeza hamu/ashiki za mapenzi.

“Hii ilikuwa adhabu ya Mungu kwa kasisi huyo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke huyo. Mungu alikuwa anataka kuleta vitendo vyake vya gizani hadharani,” jirani mmoja alinukuliwa.

Majirani walisema mwanamke mshukiwa alikosana na mumuwe mwaka uliyopita kufuatia mzozo wa kifamilia.

Waendesha teksi walisema kuwa mwanamke huyo aliwaomba msaada ampeleke hospitalini lakini tayari alikuwa amekufa.

Kuachiliwa:
“Alikuja hapa akitaka tumpeleke marehemu hospitalini lakini baada ya kufika kwake tulipata mwili wake ukiwa baridi kumaanisha alikuwa ashakufa,” alisema mhudumu wa teksi ambaye alisema baadaye waliwajulisha maafisa wa polisi.

Polisi walimzuilia mwanamke huyo kwa saa kadhaa ili kutoa habari kuhusu kisa hicho lakini wakamwachilia baadaye.
“Tutabaini chanzo cha kifo cha kasisi baada ya mwili wake kufanyiwa upasuaji, kwa sasa hauwezi kutoa taarifa yoyote,” alisema Bw Kerich .

Bw Kerich alisema kuwa polisi wamekusanya bidhaa katika chumba hicho ambazo zitatumiwa katika uchunguzi.

Mwili wa marehemu ambao polisi walisema haukuwa na majeraha yoyote ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City kufanyiwa upasuaji.

Waumini wa kanisa la Redeemed Gospel Buruburu walifika katika eneo hilo na kuondoa gari la pasta huyo ili kuzuia wanahabari kulipiga picha.

Mchimba Riziki

Kuchinja Punda Halali Kenya... Bucha Ya Kwanza Kuzinduliwa Karibuni


VIONGOZI mjini Nakuru wameteta vikali baada ya kichinjio cha nyama ya punda kujengwa huko Naivasha. Hata hivyo, kunao waliosifu hatua ya kujenga kichinjio hicho wakisema ni biashara mwafaka.

Punda

Naibu Gavana wa Nakuru John Ruto alipinga vikali uwepo wa kichinjio hicho huko Maraigushu.
Mbunge wa Naivasha John Kihagi naye alisema hatua hiyo chafulia Naivasha jina.
Bw Ruto alisema mkutano wa washika dau akiwemo Mkuu wa Bora Afya wilayani Naivasha na Mkuu wa Idara ya Matibabu ya Mifugo wataitwa ili kuelezea ni kwa nini walikubali ombi la kujengwa kwa kiwanda hicho ambacho kitagharimu Sh15 milioni.


Kichinjio hicho ambacho kinamilikiwa na wawekezaji kutoka China na Kenya kiko tayari kufunguliwa baada ya wiki mbili zijazo mara tu serikali itakapotoa vibali vya kusafirisha nyama hiyo kwenda Uchina.
Nyama Ya Punda

“Hii itachangia wizi wa punda na kisha kuuzwa hapo huku wasafirishaji nyama wakibeba mizoga ya punda bila kujali kwani sasa itakuwa halali,” alilalamika mbunge wa Naivasha John Kihagi.


Lakini Mkurugenzi wa kiwanda hicho John Kariuki alipinga madai hayo akisema tayari wameweka makubaliano na wafugaji wa punda huko Baringo, Nakuru, Laikipia na Samburu na hivyo basi wako tayari kuanza kazi hiyo ambayo itawapa watu 30 kazi huku wengine 100 wakiajiriwa kama wafanya kazi na madereva humo.

Mbunge wa Molo Jacob Macharia alifurahia biashara hiyo akisema sasa Wakenya watapata nafasi ya kubadili mawazo potovu kuhusu nyama ya punda ambayo imekuwa ikiuzwa kisirisiri katika maduka mbali mbali ya nyama, hasa ile ya nyama choma na chemsha.

Bw Kihagi alisema huenda akaelekea mahakamani kupinga ufunguzi rasmi wa kiwanda hicho akisema kinaharibia wananchi na wanabiashara wa nyama jina huko Naivasha na hivyo hakifai kufunguliwa kamwe.



Nafasi za kazi:
Lakini kiwanda kimepata idhini kutoka kwa serikali huku nia yake ikiwa ni kuchinja punda na hatimaye kusafirisha nyama hiyo hadi Uchina ambako ulaji wa punda ni kawaida.

Nyama Ya Punda
Bw Macharia alisema kiwanda hicho kitaongeza nafasi zaidi za kazi huku wakulima wakianza kufuga punda wa nyama na kuwauzia Wachina kwa njia iliyo halali.

Wazo hilo pia lilipata kuungwa mkono na Mwakilishi wa Chama cha Wanabiashara Bw Njuguna Kamau  ambaye alisema Kenya inahitaji viwanda vingi ili kuongeza nafasi za kazi kote nchini.




Mchimba Riziki

  

Monday, February 17, 2014

Rubani Mzaidizi Aiteka Nyara Ndege Ya Ethiopia.


Assistant pilot of the passenger jet airline of Ethiopia WHO spoiled.

Passenger jet Ethiopia
Geneva officials say the Deputy's pilot Took control of the aircraft pilot When he went into the bathroom to the his need.
The event will reportedly not happen the aircraft type Boeing 767-300 became ikipaa in the atmosphere of Sudan.
Pilot's assistant changed the course of the aircraft bound for Rome That frame Italy, and Switzerland kuipaa Until he poitua in Geneva airport.
In a statement to the media That The Organization says all 200 Passengers are safe.
Report departments managing air traffic in Switzerland says That the pilot's assistant asked for Citizenship before the aircraft landing and he surrendered to security Officers surrounded WHO Had the aircraft.
Police immediately arrested arrested.

Provision miner

Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score