Friday, December 27, 2013

NG'OMBE WA MAAJABU HUKO INDIA, WANAWAKE HUJIFUNGUA WATOTO WA KIUME KILA WAMSHIKAPO NG'OMBE HUYO MWENYE MIGUU MITANO.

Ng'ombe mwenye miguu mitano amekuwa akifanya miujiza nchini India, hii ni kutokana kila mwanamke mwenye mimba akishika mguu huo wa tano hujifungua mtoto wa kiume.

Raj Pratap's ndio jina alilopewa Ngombe  huyo, Raj mwenye miaka mitatu alianza kuonyesha maajabu baada ya mwanamke mwenye watoto wanne kuushika mguu wake watano na mwanamama huyo kujaliwa kupata watoto mapacha  wa kiume kwa mara ya kwanza.

Mwanamama huyo alipojifungua mapacha hao mapema mwezi wa pili mwaka huu,habari hizo zilizambaa kote India kuwa ngombe mwenye miguu mitano mwenye bahati apatikana,kwani katika dini ya Hindu wanaamini kuwa kati ya ngombe 5 millioni lazima mmoja mwenye bahati atapatikana.

Kuanzia siku habari za Ng'ombe mwenye miguu mitano kujulikana, Bwana Pratap amekuwa akijiingizia kipato kikubwa baada ya wanawake 30 kumtembelea Ng'ombe na kuushika mguu huo wa tano ili wapate watoto wa kiume. Bwana Pratap alijipatia  karibia Rupia 500 za India sawa na £5.

Cha kushangaza ni kwamba taarifa zinasema wanawake wote hao waliomshika Ng'ombe huyo waliweza kujifungua watoto wa kiume wote 30.Hii ilisababisha mmiliki wa Ng'ombe huyo kuwa na uhakika hata kukubali kumrudishia mtu pesa kama hatafanikiwa kumpata mtoto wa kiume.

Jumatatu ya 23 Dec mwaka huu, Ngombe huyo alisherekea maajabu yake ya watoto 33 kupatikana baana ya mwanamke aliyeshika mguu wake watano  kujifungua mapacha watatu wote wa kiume.

Bwana Pratap alisema, watoto wote waliokwisha kupatikana ni 33 na wote ni wakiume, mara ya mwisho ni mapacha watatu wamepatikana. Aliongeza "sijui kwanini haya yanatokea  lakini Raju anayo zawadi na ninataka tushiriki na ulimwengu mzima".

Kila siku ninafikiri kumpeleka Raju "Ulaya " ama "Amerika " na kufanya maajabu kule, alisema bwana Pratap.

Katka jamii ya Kihindi watoto wakiume wanapendwa sana kwani wao wanafaida kubwa na ni msaada kwa familia zao.

Mwanamke mmoja aliyepata mtoto wa kiume mwezi wa kumi mwaka huu ambae amekataa jina lake kutajwa amesema,Ni zawadi kutoka kwa Mungu kuushika mguu huu wa tano wa Raju ni bahati sana ,na umenizawadia mtoto wa kiume ninafuha sana.Pia familia yangu wanafuraha sana kwa kujua kuwa niko na kijana.

Ng'ombe wanaabudiwa sana na Wahindi wanaoamini katika dini ya Hindus kuwa Mungu wao Krishna alikuwa ni mchunga ng'ombe. 

Mchimba Riziki

KENYA KUHAMA KUTOKA ANOLOJIA KWENDA DIJITALI VITUO VYA TELEVISION KUFUNGWA.

Kenya ilifunga ishara zote za matangazo ya
analojia saa sita ya usiku wa Alhamisi usiku wa jana (tarehe 26
Desemba) kufuatia uamuzi wa mahakama
mapema wiki hii, The Standard la Kenya liliripoti.

Nation Media Group, Standard Media Group na
Royal Media Services zilizima matangazo yao siku
ya Jumatatu katika kupinga kupuuzwa na
Mahakama Kuu kwa ombi lao la kucheleweshwa
kwa uhamaji kwenda dijitali.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia
Fred Matiang'i alisema kaya nyingi zilikuwa
zimejiandaa kuhamia huko dijitali.

"Kati ya TV zipatazo milioni 1.5 million ndani ya
eneo la awamu yetu ya kwanza kuzima, kiasi cha watu
500,000 tayari zimeshahama kwenda dijitali kwa
sababu wamejiunga na ama DSTV au GoTV,"
alisema. "Hilo linatuacha na kiasi cha watu  milioni na
wale wapatao 700,000 ambao tayari
wameshanunua vigamuzi."

Rufaa ya vikundi vya vyombo vya habari
inatarajiwa kusikilizwa mahakamani siku ya leo
Ijumaa.

Mchimba Riziki

UHURU KENYATTA NA WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA HAILEMARIAM DESALEGN WAIZURU SUDAN YA KUSINI KUTAFUTA AMANI

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Waziri Mkuu
wa Ethiopia Hailemariam Desalegn waliwasili
huko Juba Alhamisi hapo jana (tarehe 26 Disemba) kwa ajili
ya mazungumzo na rais wa Sudani Kusini Salva
Kiir yanayolenga kutatua hali ya kukosekana kwa
utulivu kunakoongezeka katika nchi hiyo,Afp iliripoti.

Viongozi hao walipigwa picha kabla ya kuingia
kwenye mazungumzo ya siri.

Ziara hiyo imekuja
katikati ya jitihada zinazoendelea zinazofanywa
na mataifa yenye nguvu ya kanda hiyo kuzuia
hali isiyo na utulivu kwa takribani wiki mbili.

Wajumbe kutoka Kenya na Ethiopia tayari
walishirikishwa katika jitihada za usuluhishi wiki
iliyopita, wakati mawaziri wa mambo ya nje wa
nchi husika walikuwa mojawapo wa ujumbe wa
kanda huko Juba.

Waziri wa nje wa Kenya Amina Mohammed
ameambatana na Kenyatta kwenda Juba, ofisi
yake ilisema.

Kenya imekuwa ikituma ndege kuhamisha raia
wake kutoka Sudani Kusini , ambapo wengi wana
biashara.

Watu elfu kadhaa wanaaminika waliuawa
tangumapambano yalipozuka Sudani ya Kusini ,
baina ya vikosi vinavyomtii Kiir dhidi ya wale
wanaomunga mkono mpinzani wake Riek
Machar, aliyekuwa makamu wa rais ambaye
alifukuzwa mwezi Julai.

Hali ya kukosekana kwa utulivu imechukua sura
ya kikabila, ikilenga kabila la Dinka la Kiir dhidi
ya Nuer la Machar.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga
kura Jumanne kutuma askari wa ziada karibia
6,000 na polisi kwenda Sudani Kusini, karibia
mara mbili ya kikosi cha Misheni ya Umoja wa
Mataifa huko Jamhuri ya Sudani Kusini hadi
vikosi 12,500 na polisi wa kiraia 1,323.

Umoja wa Afrika (AU) na Mamlaka baina ya
serikali za Maendeleo (IGAD) imeelezea kwa
uwazi wasiwasi juu ya kuongezeka kwa vurugu.

"AU na IGAD zimekuwa na wasiwasi mkubwa
kutokana na ripoti ya uhamasishaji wa
wanamgambo wa kikabila huko Sudani Kusini,
jambo ambalo linatishia kuongezeka zaidi kwa
mzozo na kuingia kwenye vurugu baina ya
kikabila zitakazosababisha uharibifu mkubwa
ambazo zingeweza kuhatarisha taifa liliundwa
hivi karibuni la Sudani Kusini," vikundi hivyo
vilisema katika taarifa.

IGAD inatarajia kufanya mkutano wa wakuu wa
nchi kuhusu mzozo wa Sudani Kusini hapa
Nairobi siku ya leo (ijumaa)

By Mchimba Riziki

MWALIMU WA DINI APIGWA RISASI MOMBASA

Ulamaa wa Kiislamu alipigwa risasi na kufariki
dunia na wanaume wenye silaha ambao
hawajafahamika usiku wa Jumatano (tarehe 25
Disemba) huko Ukunda, moja ya eneo muhimu
ya utalii nchini Kenya kandokando ya Bahari ya
Hindi, kusini mwa Mombasa, AFP iliripoti.

"Halikuonekana kuwa tukio la kawaida la
ujambazi," Jack Ekakoro, kamanda wa eneo hilo
alisema Alhamisi.
"Alionekana kuwa mlengwa wa
washambuliaji."

Salim Mwasalim, alivyokuwaa akijulikana
mwalimu huyo wa dini mwenye umri wa miaka
60, "alipigwa risasi wakati akitembea kurudi
nyumbani akitokea kwenye msikiti ulio karibu,"
Ekakoro alisema.

"Tunachunguza kujua sababu na kuwapata
washambuliaji," aliongezea, akisema wauaji
walitoroka kwa pikipiki.

Ulamaa mwingine wa Kiislamu Hassan Mwayuyu
alipigwa risasi kwenye mazingira kama hayo, pia
na wanaume wenye silaha waliokuwa kwenye
pikipiki, katika eneo hilo tarehe 6 Disemba.

Mwasalim alikuwa chini ya uchunguzi wa polisi
katika orodha ya wanaodaiwa kutoa mafunzo
kwa vijana kupambana pamoja na al-Shabaab,
chanzo cha polisi kiliiambia AFP.

By Mchimba Riziki

Wednesday, December 25, 2013

MSIMU HUU WA SIKUKUU ULINZI WAIMARISHWA MARA DUFU KUEPUKANA NA MATUKIO HATARI ZANZIBAR:

MSIMU HUU WA SIKUKUU ULINZI WAIMARISHWA MARA DUFU KUEPUKANA NA MATUKIO HATARI ZANZIBAR:

 Wakati sikukuu ya krismasi inakaribia, ikitoa nafasi ya kuanza kwa kilele cha msimu wa krismasi, polisi wamewaomba wakaazi kuwa waangalifu na kushirikiana na uongozi ili kuhakikisha usalama kwa wote.

"Hali ya sasa ni nzuri, lakini tumeongeza ulinzi katika maeneo yote ya Zanzibar ikiwa ni pamoja na maeneo ya makanisa," Kamishna wa Polisi wa Zanzibar Hamdan Omar Makame aliwaambia waandishi wa habari. "Tumewaomba viongozi wa makanisa kuripoti kwa polisi nyendo na matukio yoyote wanayoyatilia shaka."

Makame pia alikutana na viongozi wa Chama cha Wawekezaji wa Utalii Zanzibar katika makao makuu ya polisi siku ya Jumanne (tarehe 24 Desemba) ili kuwahakikishia kuwa polisi wamechukua hatua zote za lazima kuhakikisha usalama wa watalii na raia.

Aliwashukuru kwa kuendeleza ushirikiano wao na viongozi wa usalama na kuomba kwamba wamiliki wa hoteli wote kufunga kamera za usalama katika majengo yao.

"Kila mtu ana jukumu la kutimiza katika kuiweka Zanzibar salama, ikiwa ni pamoja na [kuifanya] mahali salama kwa watalii," alisema.


Matukio ya mashambulizi:
Katika mwaka mmoja na nusu uliopita, mfululizo wa mashambulizi ya tindikali yakiwalenga viongozi wa dini na wageni kutoka nje yaliharibu sifa ya Zanzibar.

Mwezi Novemba 2012, Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Suleiman Soraga alijeruhiwa katika shambulizi la tindikali wakati akifanya mazoezi ya kukimbia karibu na nyumbani kwake.

Mwaka jana siku ya Krismasi, mtu mwenye silaha alimpiga risasi na kumjeruhi vibaya Padri Ambrose Mkenda, padri wa kikatoliki katika mji wa Zanzibar. Kisha mwezi Februari 2013, mtu asiyejulikana mwenye silaha alimuua padri wa Kikatoliki Evarist Mushi nje ya kanisa lake Zanzibar.

Mapema mwezi Agosti, washambulizi wasiojulikana waliwamwagia tindikali usoni wanawake wawili wa Uingereza wenye umri wa miaka 18 waliokuwa wakiishi Zanzibar na kufanya kazi kama walimu wa kujitolea.

Tarehe 13 Septemba, padri wa Kikatoliki wa Zanzibari Joseph Anselm Mwangamba aliharibiwa sura na washambulizi wasiojulikana ambao walimmwagia tindikali alipokuwa akitoka kwenye mgahawa wa intaneti Mji Mkongwe. Siku kumi baadaye, kundi la washambuliaji wasiojulikana katika gari la pikapu walitupa guruneti kuelekea kwenye eneo lenye maduka mengi katika Mtaa wa Darajani katika mji wa Zanzibar, lakini lilishindwa kulipuka.

Wakristo na Waislamu wa visiwani walio wengi kihistoria wamekuwa wakiishi kwa amani, Makame alisema, hata hivyo uhalifu huo wa kikatili unauchochea umma na kuipa Zanzibar sifa mbaya nchi za nje.

Ili kusaidia kuhakikisha usalama na kuongeza ushirikiano, Makame alisema ofisi yake imekuwa ikihamasisha mikutano na mijadala baina ya dini mbalimbali ili uhusiano mzuri kati ya Waislamu na Wakristo uimarishwe.

Wakristo wanafikia asilimia 3 ya watu milioni 1.2 wa Zanzibar, walio wengi kati ya hao ni Waislamu.


Wajibu wa Uamsho wachunguzwa:
Bado haieleweki kama mashambulizi ya tindikali na matukio mengine yanachochewa kidini, lakini vurugu za hapa na pale zilianza baada ya kukamatwa kwa kiongozi wa Uamsho Sheikh Farid Hadi Ahmed mwezi Oktoba 2012.

Uamsho, ulitokana na shirika la hisani la dini kuwa chama cha waliojitenga wakidai uhuru kutoka Tanzania.

Ahmed ana viongozi wengine tisa wa Uamsho bado wanashikiliwa, wakishtakiwa Mahakama Kuu ya Zanzibar kwa kuchochea vurugu na fujo, na njama za kuhatarisha amani na utulivu, miongoni mwa makosa mengine. Walikuwa hawajashitakiwa na walikataliwa dhamana chini ya Sheria ya Usalama wa Taifa. Walikuwa wanasubiri rufaa katika Mhakama Kuu ili kubatilisha uamuzi wa dhamana.

Viongozi wa Uamsho na wafuasi mara kwa mara wamekuwa wakileta wasiwasi wa kidini katika visiwa, lakini taasisi wakati wote imekuwa ikikanusha kuhusika.

Katika mikusanyiko kadhaa mwaka jana, viongozi wa Uamsho walitetea uhuru wa Zanzibar kutoka katika muungano wa sasa na Tanzania ili kutekeleza sheria za Kiislamu.

"Viongozi wa Uamsho wanaamini kwamba uhuru wa Zanzibar utasaidia kutunza utamaduni wa Kiislamu ambao umeharibiwa na mwingiliano wa mtindo wa maisha wa kigeni unaoletwa na wageni na kuigwa na vijana wa nchini," Ahmed aliwaambia waliohudhuria katika mkusanyiko kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari ya Lumumba mwezi Mei 2012.

Hassan Khatib, mwenye umro wa miaka 32, mwalimu katika shule ya dini na mfuasi wa Uamsho anayeishi Zanzibar, alisisitiza kusema kauli yake na kupuuza tuhuma kwamba kikundi kinachochea vurugu.

"Tunataka nguo za heshima hatutaki sketi fupi," Khatib aliwambia waandishi wa habari. "Tunapinga kuongezeka kwa baa, na tunadai uhuru wa Zanzibar ili tuweze kujenga uchumi wetu na kulinda utamaduni wetu."


Vurugu zatishia tasnia muhimu ya utalii:
Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar Saidi Ali Mbarouk alisema kwamba mwaka jana tasnia ya utalii, ambayo inachangia asilimia 27 ya pato ghafi la ndani la Zanzibar, iliathiriwa vibaya sana na vurugu.

Tasnia inaajiri moja kwa moja watu 15,000, wakati zaidi ya kazi nyingine 35,000 zinatokana moja kwa moja na utalii, alisema.

"Machafuko yaliyochochewa na kikundi cha Uamsho cha Waislamu mwezi Oktoba mwaka jana, yakifuatiwa na mashambulizi ya viongozi wa dini yameharibu sifa ya Zanzibar," aliiambia Sabahi, akiongeza kwamba kutokuwa na utulivu kumesababisha kushuka kwa utalii, ambako serikali inajaribu kuzuia katika msimu mkuu wa mwaka huu.

Kipindi cha watalii wengi Zanzibar ni kuanzia katikati ya mwezi Juni hadi Septemba na katikati ya Desemba na Februari.

Kutokana na hatua za kukinga zilizochukuliwa kuhakikisha usalama, Mbarouk alisema mamlaka zilikuwa zikitarajia kila kitu kuendeshwa kwa amani kuzunguka katika maeneo ya utalii wakati wa sikukuu.

"Hatutarajii tukio lolote wakati wa sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya," alisema. "Tunawaomba wananchi kuwakaribisha wageni."

Mwenyekiti wa Chama cha Wawekezaji wa Utalii Zanzibar Abdulsamad Ahmed Saidi alikiri kwamba hadi sasa mambo yanaonekana kuwa mazuri.

"Utafiti tulioufanya wiki iliyopita unaonyesha kwamba kuna uthabiti wa biashara katika utalii na ushikaji mzuri wa nafasi kwani katika baadhi ya hoteli nafasi zimejaa," aliwaambia waandishi wa habari.

"Tumelalamika kuhusu usalama, lakini serikali ilijibu vizuri kwa kuongeza maofisa usalama zaidi na pia kuhamasisha polisi jamii, hususani kuzunguka maeneo ya vivutio vya utalii kama vile Mji Mkongwe wa Zanzibar," alisema Saidi.


Hofu inaendelea kuwa kubwa:
Pamoja na uhakika kutoka kwa viongozi wa serikali, hofu inaendelea kuwa kubwa miongoni mwa jamii ya Kikristo.

"Tuko imara na tunaamini yote yataendelea vizuri, lakini jamii ya Kikristo ina wasiwasi," alisema Michael Hafidh, mhubiri katika Kanisa la Anglikani la Zanzibar. "Tumekuwa tukiishi [pamoja] kwa amani kwa miaka mingi, lakini baadhi ya watu wanatugawanya."

Aliwaomba polisi kuendelea kufanya jitihada za kuwasaka watu wanaosababisha hofu na wasiwasi wa kidini visiwani hapo.

Dickson Kaganga, askofu wa Kanisa la Assemblies of God huko Zanzibar, mojawapo kati ya makanisa yaliyolengwa wakati wa maandamano mwaka jana, alisema waumini wake walikuwa na wasiwasi lakini wana matumaini.

"Wote tuna haki ya kushiriki katika dini zetu huko Zanzibar," aliwaaambia waandishi wa habari, akitoa wito kwa polisi kuhakikisha kila mmoja anakuwa salama.

Sheikh Soraga pia alitoa wito wa waamini kuwa na uvumilivu na kushirikiana kwa amani huko Zanzibar, akisema kisiwa hakiwezi kuendelea kama hali ya wasiwasi wa kidini na kisiasa iliopo sasa itaendelea.

"Tuepuke migogoro isiyo ya lazima. Kuna baadhi ya watu wenye ndoto za kisiasa, wanatumia dini kuligawa taifa.

Mchimba Riziki
Tunakutakia X-Mass Njema Na Heri Kwa Mwaka Mpya.

Sunday, December 22, 2013

HAWAJALI GHARAMA KUBWA ZA SMARTPHONE BALI WANACHOJALI NI MAWASILIANO

Licha ya gharama kubwa za awali za kununua smartphone, Wasomali wanaongezeka katika kulipia kutokana na faida za kuunganishwa papo hapo na intaneti, kunakorahisisha mawasiliano na wanafamilia walio nje ya nchi na kupata habari na taarifa kwa urahisi na kwa gharama nafuu kuliko njia iliyokuwa imezoeleka ya kupata intaneti.

"iPhones ya gharama kubwa kabisa ni dola 800, wakati [simu] Samsung ziliuzwa kwa dola 500, ingawaje zipo baadhi ambazo zinagharimu zaidi," alisema Faisal Abdullahi mwenye umri wa miaka 34 ambaye anamiliki duka la kuuza simu za mkononi katika soko la Hamar Weyne huko Mogadishu. Smartphone ya gharama ndogo kabisa iliuzwa kwa dola 250, alisema.

Uuzaji wa smartphone umeongezeka kwa haraka, Abdullahi alisema, akinukuu kwamba duka lake liliuza smartphone 12 mwaka 2012, na takriban 100 mwaka huu.

Abdullahi alisema wateja wake wengi wanaulizia smartphone, hususani simu za mkono za Samsung, ambazo zinafahamika sana kwa sababu ni bei rahisi kuliko iPhone na zina programu za bure zaidi.

"Baadhi ya simu hizi ni ghali sana ingawaje kwa sasa zinauzwa kwa gharama nafuu kidogo kuliko zilipokuja kwa mara ya kwanza ," alisema. "Unaweza kuona nyingine ni ghali sana, lakini tunaziuza kila mara."

Gharama ndogo za matumizi ya data:

Abdisalam Warsame, mwenye miaka 20 mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Djibouti katika wilaya ya Wadajir, alisema alimshukuru dada yake aliyeko Saudi Arabia ambaye alimtumia fedha kununua smartphone miezi nne iliyopita.

"Nilizoea kwenda katika mgahawa wa intaneti ambao unatoza shilingi 18,000 za Somalia kwa saa wakati nilipohitaji kutumia intaneti, na inawezekana kuihitaji mara kadhaa kwa siku,. "Sasa ninalipa dola 1 (shilingi 20,000) kwa zaidi ya saa 24 katika smartphone yangu."

Kwa upatikanaji wa intaneti katika simu yake ya mkononi, Warsame alisema sasa anaweza kuwasiliana na nchi nyingine duniani wakati wote.

Vivyo hivyo, mkaazi wa Mogadishu mwenye miaka 32 Yusuf Ibrahim alisema amekuwa mtumiaji wa mara kwa mara wa intaneti katika simu ya mkononi kwa miezi mitano iliyopita.

Alisema huduma hii imefanya iwe rahisi kwake kuendelea kuwasiliana na wanafamilia wake wanaoishi Finland.

"Ninawasiliana na mke wangu na watoto katika WhatsApp kila siku," Ibrahim alisema . "[Ninahisi] kama vile niko pamoja na wao, na ni nafuu kuliko kuongea nao moja kwa moja. Nilikuwa nalipa zaidi ya dola 50 hapo kabla kuongea nao tu, lakini sasa ninatumia chini ya dola 10 kwa mwezi, ingawa nawasiliana nao kila saa."

Abdirashid Hussein mwenye umri wa miaka 35, mfanyakazi wa kampuni ya intaneti na simu za mkononi ya Hormuud Telecom, alisema 1 gigabyte (GB) ya data ya intaneti inagharimu dola 25, na muda itakayodumu inategemea matumizi ya mtu.

Licha ya Hormuud, Somtel iliyoko Hargeisa ni kampuni nyingine pekee inayotoa huduma ya intaneti kupitia simu za mkononi huko kusini mwa Somalia.

Aweys Abdirahman, mwenye umri wa miaka 23 mwanafunzi katika Shule ya al-Imra katika wilaya ya Hodan Mogadishu, alisema simu za kisasa zinarahisisha kwa Wasomali kuwa wameunganishwa, ingawaje wakosoaji wanasema kwamba vijana wanatumia muda wao mwingi kwenye smartphone zao.

Somalia iko nyuma sana katika suala la upatikanaji wa intaneti, hata hivyo, ongezeko la matumizi ya intaneti ya simu ya mkononi ya gharama nafuu inasaidia kuziba pengo mwaka baada ya mwaka, alisema.

"Kwa upande mmoja sio ghali sana kwa sababu kiasi cha fedha ninachotumia kupata intaneti sasa ni [chini ya] kile nilichokuwa nikitumia kwa kupiga simu [pekee yake]," alisema Abdirahman, akiongeza kwamba anahifadhi fedha kwa kutuma ujumbe mfupi kwa marafiki zake na familia badala ya kupiga simu.

Faisal Muse Mohamed, mwandishi wa habari mwenye umri wa miaka 24 anayefanya kazi katika Redio Mogadishu, amekuwa akipata intaneti kupitia smartphone yake kwa mwaka sasa.

Hususan, anasema anatumia simu yake ya aina ya Samsung Galaxy kupata mitandao ya kijamii kama vile Facebook, ambako huingia kuwasiliana na kupata habari.

"Ninatumia Facebook zaidi kwa sababu unaweza kuwasiliana na marafiki na kupata taarifa na picha zinazokwenda na wakati ambazo zimetumwa," . Alisema anatumia pia Whatsapp kuwasiliana na marafiki kwa sababu sio gharama kubwa na haihitaji matumizi makubwa ya data.




Kuchukua nafasi ya mikahawa ya intaneti
Hassan Mohamed, mkazi wa Mogadishu mwenye umri wa miaka 30 ambaye anasoma sosholojia katika Chuo Kikuu cha Somalia, alisema smartphone ni njia binafsi zaidi ya kupata intaneti, kuunganishwa na watu na kuwa na taarifa wakati wote.

"Sasa ninajisikia kwamba nina uwezo wa kupata intaneti wakati wote ninapoihitaji badala ya kuwategemea [watoa huduma wengine] wa intaneti kama zamani," alisema Mohamed, ambaye amekuwa akitumia simu aina ya Samsung Galaxy kwa karibia miezi saba sasa.

"Ninaitumia kutuma baruapepe, kupata taarifa kuhusu habari, na pia ninatumia kupata tarifa zinazohusiana na masomo na taarifa kutoka katika Google na kupata mitandao ya kijamii," .
"Ninaweza pia kusoma au kutazama chochote ambacho ni faragha kivyangu. Kwa kuwa maeneo ya huduma za intaneti ni maeneo ya umma, huwezi kupata au kutazama kila kitu unachokitaka," alisema.


Mchimba Riziki

Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score