Thursday, September 5, 2013

Kenya kupigia kura kujitoa ICC kabla ya kesi

Bunge la Kenya liliitwa siku ya Jumanne (tarehe 3 Septemba) kuzungumzia juu ya kumaliza uwanachama wa nchi hiyo kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kabla ya kesi dhidi ya uhalifu wa kibinadamu inayomkabili Naibu Rais William Ruto kuanza mjini The Hague wiki ijayo, liliripoti shirika la habari la AFP.Naibu Spika Joyce Laboso alitoa agizo ya "kikao maalum cha bunge" kukutana siku ya Alhamisi.

Hata hivyo, hata kama Kenya itaamua kujitoa kwenye ICC - ambayo itakuwa ni nchi ya kwanza kufanya hivyo - hakutaathiri kesi hizo kwani taratibu za kisheria tayari zimeanza. Ombi maalum la kujitowa pia litahitaji kuwasilishwa, hatua ambayo inaweza kuchukua miezi kadhaa.

Wabunge wanatarajiwa kujadiliana na kupigia kura uwezekano wa kujitoa kwenye Mkataba wa Rome wa ICC, kufuatia ombi kutoka kwa kiongozi wa Jubilee katika baraza la Seneti, Kithure Kindiki.

"Sheria yoyote humu nchini au ya kimataifa inaweza kufutwa au kurekebishwa," alisema Asman Kamama, mmoja ya wabunge wapatao 30 wanaouunga mkono azimio la Kindiki. "Si jambo la laana na tunataka kuwa kigezo barani humu."

Kesi ya Ruto inakuja ikiwa ni miezi miwili mbele ya ile ya Rais Uhuru Kenyatta, ambaye anakabiliwa na mashitaka matano ya uhalifu dhidi ya ubinadamu, ikiwemo mauaji, ubakaji, ukatili, kuwalazimisha watu kuhama makaazi yao na matendo mengine yasiyo ya kiutu.

Wote wawili Kenyatta na Ruto wamesema watashirikiana kikamilifu na mahakama hiyo. Wanakana mashitaka dhidi yao.

Monday, September 2, 2013

Watu saba wauza madawa ya kulevya wakamatwa Nairobi Wamo Watanzania wawili,Wahindi Wawili Na Wakenya Watatu.



Polisi ya Kenya imewakamata Watanzania wawili, Wakenya watatu na Wahindi wawili kwa tuhuma ya kutengeneza madawa aina ya crystal methamphetamine jijini Nairobi,
 gazeti la The Standard la Kenya liliripoti Jumapili (tarehe 1 Septemba).

Watuhumiwa walikamatwa kwa kumiliki kilogramu 50 za madawa haramu na yanakadiriwa kuwa na thamani ya shilingi bilioni 2 (dola milioni 1.2),gazeti la The Citizen la Tanzania liliripoti.

Watanzania Rumishaeli Mamkuu Shoo, miaka 27, na January Gabriel Liundi, miaka 30, walikamatwa Alhamisi katika gari lililobeba kifaa cha kutengenezea madawa ya kulevya na malighafi za madawa.
 Washukiwa kutoka Kenya na India walikamatwa katika Eneo la Biashara la Cape, katika majengo ambayo yamebadilishwa kuwa maabara ya kutengeneza madawa ya kulevya, kwa mujibu wa Naibu mkurugenzi wa Uchunguzi wa Makosa ya Jinai Gideon Kimilu.

Inaaminika washukiwa hao ni sehemu ya ushirika ambao unatengeneza madawa ya kulevya nchini Kenya na kuyasafirisha kwenda Afrika Kusini.
Watuhumiwa Walifikishwa mahakamani leo Jumatatu.

Sunday, September 1, 2013

MECHI ZA CHAMPION LEAGUE ZITAKANZO ANZA SEPTEMBER 17 WENSDAY 2013 NA SEP 18


Champions League: FIXTURE 17 VS 18 SEPTEMBER 2013

Group A September 17

SAA    WENYEJI                WAGENI

11:45    Manchester U     VS    Bayer Leverkusen
11:45    Real Sociedad    VS    Shakhtar Donetsk

Group B September 17

11:45    FC København    VS    Juventus
11:45    Galatasaray    VS    Real Madrid

Group C September 17

11:45    Benfica        VS    Anderlecht
11:45    Olympiakos    VS    Paris Saint Germain

Group D September 17

11:45    Bayern Munich    VS    CSKA Moscow
11:45    Viktoria Plzen    VS    Manchester City

Group E September 18

11:45    Chelsea        VS    Basel
11:45    Schalke 04    VS    Steaua Bucuresti

Group F September 18

11:45    Marseille    VS    Arsenal
11:45    SSC Napoli    vs    Borussia Dortmund

Group G September 18

11:45    Atletico Madrid    VS    Zenit Petersburg
11:45    Austria Wien    VS    FC Porto

Group H September 18

11:45    AC Milan    VS    Celtic
11:45    Barcelona    VS    Ajax

HAPA CHINI INAONYESHA MAKUNDI YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE KAMA ILIVYOPANGWA


GROUP A


Man Utd
Shakhtar Donetsk
Bayer Leverkusen
 Real Sociedad

   
GROUP B


Real Madrid
Juventus
Galatasaray
Copenhagen

GROUP C


Benfica
Paris Saint-Germain
Olympiakos
Anderlecht

   
GROUP D


Bayern Munich
 CSKA Moscow
 Manchester City
Viktoria Plzen

GROUP E


Chelsea
 Schalke
 Basel
Steaua Bucharest

   
GROUP F


Arsenal
Olympique de Marseille
 Borussia Dortmund
Napoli

GROUP G


Porto
 Atletico Madrid
Zenit St Petersburg
Austria Wien
   
GROUP H


Barcelona
AC Milan
Ajax
Celtic






Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score