Saturday, September 21, 2013

Alshabab wakiri kutekeleza utekaji Wa Westgate

Wapigani wa Somalia Alshabab wamekiri jioni hii kuwa wao ndio waliiohusika katika shambulizi lililotokea leo mapema hapa Nairobi saa 11:50.Wapiganaji hao waliandika katika mtandao wao wa Twitter kwamba wamefanya hivyo kwa sababu ya kulipisha kizazi ya majeshi ya Kenya kuingilia Somalia kuwathibiti wao.


Mujahideen waliingia ndani ya jengo hilo la kibiashara leo mchana na mpaka sasa bado wapo ndani ya jengo hilo la Westgate.na waliingia humo kupambana na ma-Kafiri wa Kenya ndani na waliingia ndani ya himaya yao walisema kundi hilo la Jihad Somalia

Wakenya kazi yao sasa ni kuwasubiri ama kuangalia nini kitafanywa na Majeshi yao ndani Westgate kwani mpaka sasa Majambazi hao bado wanasadikika kuwa wamo ndani ya Jengo hilo na kuna raia wanaoshikiliwa na kundi hilo baya kwa usalama.

Al-shabab pia wamejitapata kuwa watu waliowaua ni 100 na sio 30 kama ilivyoripotiwa na Kenya Red Cross lilisema kundi hilo.

Kwa upande wa shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya wao wamesema watu waliouwawa ni 30 na waliojeruhiwa ni 60 hadi kufikia muda huu.Ambapo bado watu wanaokolewa .

Ikumbukwe kwamba Majeshi ya Kenya yaliingia nchini Somalia miaka miwili iliyopita  kupambana na Al-shabab,na mpaka sasa majeshi hayo ya Kenya yamebaki katika nchi ya Somalia kama majeshi ya Umoja wa Afrika na ilihaidi kuisaidia Somalia, pia majeshi hayo yanaungwa mkono na Umoja wa Kimataifa.

Friday, September 20, 2013

Vyombo vya habari na Wanablogu Nchini Kenya Wapewa Onyo kali na ICC

Vyombo vya habari na wanablogu nchini Kenya wametaja utambulisho wa mwanamamke aliyejitokeza kama shahidi anayelindwa kwenye kesi ya uhalifu dhidi ya ubinadamu ya Naibu Rais wa Kenya, William Ruto, wakichochea onyo kali kutoka kwa Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa (ICC) na hasira kali kutoka kwa makundi ya haki za binadamu.

Mwanamke huyo alikuwa ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka katika kesi dhidi ya Ruto, na siku ya Jumanne (tarehe 17 Septemba) alitoa mbele ya mahakama hiyo ushahidi wa namna alivyopata mateso huku akilia alipokuwa akielezea alivyofungiwa ndani ya kanisa moja akiwa na watu wengine kiasi cha 2,000 na kumiminiwa mafuta na kuchomwa moto baada ya uchaguzi uliozozaniwa wa mwaka 2007.

Shahidi huyo alitajwa tu kama "Shahidi P0536", uso wake ulifichwa na sauti yake kugeuzwa. Lakini ndani ya kipindi ambacho mahakama ilikuwa ikiendelea na kikao chake, iliyorushwa moja kwa moja na vituo kadhaa vya televisheni nchini Kenya, watazamaji walianza kukisia jina lake halisi kwenye mtandao wa Twitter na mitandao mingine ya kijamii, liliripoti shirika la habari la AFP.

Kufikia Jumatano, taarifa kadhaa kwenye Twitter zilitoa lile linaloweza kuwa jina lake halisi, ambapo mwanablogu mmoja wa Kenya na mtandao wa gazeti moja walichapisha hata picha walizosema ni za shahidi huyo. Maoni kadhaa pia yalimtaja mwanamke huyo kama "muongo".

ICC ilisema inaweza kuchukua hatua za kisheria.

"Ubainishaji wowote wa utambulisho wa shahidi ambaye utambulisho wake umelindwa... ni sawa sawa na kosa la jinai," alisema jaji kiongozi wa ICC, Chile
Eboe-Osuji. "Mambo hayo yatachunguzwa na watuhumiwa watafunguliwa mashtaka."

Jaji huyo alisema onyo hilo linamuhusu "kila mtu ndani ya chumba cha mahakama, kwenye eneo la umma, nchini Kenya, na kwengineko kote duniani", na kuwatolea wito "wanahabari, wanablogu, watumiaji wa mitandao ya kijamii au washiriki na wenye mitandao... kujitenga na lolote linaloweza kubainisha au kujaribu kubainisha utambulisho wa mashahidi wanaolindwa."

Shirika la haki za binadamu la Amnesty International lilisema "limetiwa wasiwasi sana" na kutoa wito kwa "ICC na mamlaka nchini Kenya kuchukua hatua madhubuti za kulinda usalama na afya ya shahidi huyu na familia yake."

Tume ya Haki za Binadamu ya Kenya, jumuiya huru isiyo ya kiserikali, ilisema mashahidi wengine sasa wanaweza kujitoa kwenye kesi hiyo.

"Kwa kuwa sasa shahidi huyu ametambuliwa, itakuwa ni shida kuwahakikishia wengine kwamba wao na familia zao watakuwa salama. Na nchini Kenya, hakuna familia ndogo tu: kuna mashangazi, mama wadogo na wakubwa, wajomba na baba wadogo na wakubwa, binami na wapwa," alisema msemaji wa Kamisheni hiyo, Beryl Aidi.

"Mashahidi wana haki ya kuhisi kwamba familia na jamaa zao wanaweza kuwa hatarini na wakataka kujitoa," alisema.

Endelea kuperuz ndani ya Mchimba riziki kwani baadaye kidogo tutawaletea maoni ya Wakenya kuhusu "Nini maoni yao kuhusiana na majina ama bahasha aliyonayo jaji Philip Wako ya watu wengine wanaotajwa kuhusika katika ghasia ya mwaka 2007/2008 Je kuna umuhimu wa majina hayo kuwekwa hadharani kabla ya kufika The Hegue {ICC}.


By Mchimba Riziki

Wednesday, September 18, 2013

Wabunge walimana makonde Nigeria kuhusu siasa za chama cha PDP Kujigawa





LAGOS, Nigeria

WABUNGE katika bunge la Nigeria Jumanne walilimana mangumi na mateke baada ya kundi moja lililojitenga kutoka kwa chama kinachotawala kuruhusiwa kuingia bungeni.

Kituo cha kibinafsi cha runinga cha African Independent Television pamoja na Channels TV vilionyesha picha za mbunge mwanamke aliyejawa na hasira akimchapa mwenzike usoni huku mbunge mwingine mwanamume akionekana akichukua kiti na kumchapa mwenzake.

Wabunge wengine walionekana wakiwapiga wenzao ngumi. Vurugu hizo zilianza baada ya kuwasili kwa Kawu Baraje, mwenyekiti wa kikundi kilichojitenga kutoka kwa Chama cha Peoples Democratic Party (PDP) ambaye aliambatana na magavana wanaomuunga mkono.

Spika wa bunge la wawakilishi, Aminu Tambuwal, aliwaambia wabunge kwamba Baraje alikuwa ameomba ruhusa kuwahutubia wafuasi wake katika hafla ya ufunguzi wa bunge.

Lakini kuwasili kwa kundi hilo kuliwakasirisha wabunge wa chama halisi cha PDP. Kelele zilianza, Baraje alipokuwa akiwahutubia wabunge. Chama cha PDP kina viti 23 kati ya 36 katika bunge hilo.

Chama hicho ambacho kimekuwa mamlakani tangu 1999, kimejipata pabaya katika siku za hivi majuzi. Kimekumbwa na mgawanyiko na upinzani mkubwa.

Chama hicho kinatazamwa kama kitaweza kukabiliana na tofauti zilizoko na kuchukua tena urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanywa 2015.

Mgawanyiko umedumu kwa miaka kadha huku wanachama wengine wakipinga ushindi wa Rais Goodluck Jonathan.

By Mchimba Riziki

Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score