Wednesday, February 19, 2014

Kuchinja Punda Halali Kenya... Bucha Ya Kwanza Kuzinduliwa Karibuni


VIONGOZI mjini Nakuru wameteta vikali baada ya kichinjio cha nyama ya punda kujengwa huko Naivasha. Hata hivyo, kunao waliosifu hatua ya kujenga kichinjio hicho wakisema ni biashara mwafaka.

Punda

Naibu Gavana wa Nakuru John Ruto alipinga vikali uwepo wa kichinjio hicho huko Maraigushu.
Mbunge wa Naivasha John Kihagi naye alisema hatua hiyo chafulia Naivasha jina.
Bw Ruto alisema mkutano wa washika dau akiwemo Mkuu wa Bora Afya wilayani Naivasha na Mkuu wa Idara ya Matibabu ya Mifugo wataitwa ili kuelezea ni kwa nini walikubali ombi la kujengwa kwa kiwanda hicho ambacho kitagharimu Sh15 milioni.


Kichinjio hicho ambacho kinamilikiwa na wawekezaji kutoka China na Kenya kiko tayari kufunguliwa baada ya wiki mbili zijazo mara tu serikali itakapotoa vibali vya kusafirisha nyama hiyo kwenda Uchina.
Nyama Ya Punda

“Hii itachangia wizi wa punda na kisha kuuzwa hapo huku wasafirishaji nyama wakibeba mizoga ya punda bila kujali kwani sasa itakuwa halali,” alilalamika mbunge wa Naivasha John Kihagi.


Lakini Mkurugenzi wa kiwanda hicho John Kariuki alipinga madai hayo akisema tayari wameweka makubaliano na wafugaji wa punda huko Baringo, Nakuru, Laikipia na Samburu na hivyo basi wako tayari kuanza kazi hiyo ambayo itawapa watu 30 kazi huku wengine 100 wakiajiriwa kama wafanya kazi na madereva humo.

Mbunge wa Molo Jacob Macharia alifurahia biashara hiyo akisema sasa Wakenya watapata nafasi ya kubadili mawazo potovu kuhusu nyama ya punda ambayo imekuwa ikiuzwa kisirisiri katika maduka mbali mbali ya nyama, hasa ile ya nyama choma na chemsha.

Bw Kihagi alisema huenda akaelekea mahakamani kupinga ufunguzi rasmi wa kiwanda hicho akisema kinaharibia wananchi na wanabiashara wa nyama jina huko Naivasha na hivyo hakifai kufunguliwa kamwe.



Nafasi za kazi:
Lakini kiwanda kimepata idhini kutoka kwa serikali huku nia yake ikiwa ni kuchinja punda na hatimaye kusafirisha nyama hiyo hadi Uchina ambako ulaji wa punda ni kawaida.

Nyama Ya Punda
Bw Macharia alisema kiwanda hicho kitaongeza nafasi zaidi za kazi huku wakulima wakianza kufuga punda wa nyama na kuwauzia Wachina kwa njia iliyo halali.

Wazo hilo pia lilipata kuungwa mkono na Mwakilishi wa Chama cha Wanabiashara Bw Njuguna Kamau  ambaye alisema Kenya inahitaji viwanda vingi ili kuongeza nafasi za kazi kote nchini.




Mchimba Riziki

  

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score