Friday, August 16, 2013

MBINU MPYA ZA WASICHANA WA VYUO KUJILEWESHA KWA DAWA ZAZ KULEVYA


Katika uchunguzi uliovyanywa na shirika moja nchini Kenya linaonyesha kwamba kwa sasa wasichana wa vyuoni na shule za upili wamepata mbinu mpya za kuwalevya.
Haya yanavanywa na wanafunzi hao ili kusudi kukwepa adhabu za walimu wawapo mashuleni.

Kinyume na hapo mwanzo ambapo watumiaji wa mihadarati walikuwa wakijidunga au kumeza vidonge, wasichana hao sasa wamegundua mbinu mpya ya kupaka madawa hayo kwenye sodo, dawa hizo hupenya polepole kwenye mwili kwa kutumia vitobo/vitundu  vidogo vilivyoko mwilini.

Kwa mujibu wa shirika hilo la kurekebisha tabia, limearifu kuwa idadi kubwa ya wasichana waliogeukia uraibu huo imeongezeka maradufu.
Kwa mujibu wa Bi Cecil Njuguna anaesimamia kituo cha Asumbi, amesema idadi ya wasichana hasa walio Katika shule za mabweni wanaofanya hivyo inazidi kupanda.
"Wanaita 'tampon shot' ambapo wanakwaruza sehemu zao nyeti huku wamevaa SODO hizo, na kuendelea na shughuli zao za kawaida. Lakini baada ya muda, yeyote aliemakini atagundua wanaonekana kulewa kiasi', alisema Bi Njuguna
Katika kituo cha kurekebisha tabia cha Asumbi Limuru wamesha pokea wasichana 20 waliokuwa wamenaswa na tabia hiyo.
"Wasichana hao hawawezi kuwa makini darasani na wametekwa na dawa za KULEVYA kwa kunajisi miili yao"
Bi Njuguna aliendelea kusema huenda hicho ni kionjo tu, na kwamba na huenda wasichana wengi nchini na kwingineko wamekumbatia mbinu hii ya kiajabu.

Nae Mbunge wa jimbo la Molo Bi Mary Mbugua, aliomba kuwepo kwa juhudi za pamoja kukatiza tabia hiyo haraka iwezekanavyo.
Mbugua alisema amefahamishwa kuwepo kwa mtindo huo ulioibuka
Unaolenga kuwaibua wasichana wadogo kutumia dawa za kulevya.
Uraibu huo umechangia kudorora kwa maadili Katika jamii na ndio kizingiti kikuu katika kukabiliana na utovu wa nidhamu shuleni .
"Tunaomba waalimu waangalifu zaidi wanapowashughulikia wanafunzi. Na wafahamishe wazazi mara tuu wanapodadisi mabadiliko yoyote kwa wasichana ili hatua za haraka zichukuliwe " alisema mbunge Mbugua.
Vile vile aliewahimiza wazazi kuwapa watoto kazi za nyumbani ili wanaoikuwa likizoni kwani hii itawafanya wawe watu wanaowajibika katika jamii

Naye mhudumu wa kijamii Bi Mary Marachia  alithibitisha kuwepo na kutumika  kwa njia hiyo maarufu kama SODO, alisema kuwa wasichana wengi wanaogopa kujidunga kwa sindano za kushiriki wanatumia njia hiyo hatari kutokana na kuogopa magonjwa ya kuambukiza.
Ndio maana wamegeukia dawa za kulevya kwa njia ya sodo na hivyo imewafanya vigumu sana kutambuliwa.
Bi Karachia akitoa wito hasa kwa walimu na wazazi wa wanafunzi hasa waliokatika mabweni  kufuatilia kwa uangalifu mienendo ya na masomo ya wasichana  hao kwani itasaidia kugundua na kukatiza uovu huo.
"Wasicwalioathirika wanaonyesha ishara zote za mhathiriwa akiyetekwa na uarabu wa dawa za za kulevya, ikiwemo kushindwa kuwa makini darasani, kuzinzia na kisha kutapika,"
Pia alitahadharisha "walimu kuwa makini na majeraha ya ghafla ya wasichana, yalifungwa kwa bendejiakisema kitambaa hicho chaweza kuwa kimepakwa ama kufungiwa dawa za kulevya.


 Vijana wenzangu jihathirini sana na dawa hizi za kulevya kwani litatuangamiza vijana..ushari kutoka kwa
MCHIMBA RIZIKI (Mathayo Ngotee)  "NDANI YA TAIFA LEO" KENYA 
ASANTE SANA

Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score