Saturday, May 31, 2014

Mapokezi Ya Railla Odinga Yalikuwa Ya Kutisha... Maelfu Wajitokeza Kumpokea kinara Wao

Na Mathayo Ngotee

Aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Mh.Raila Amollo Odinga aliwasili leo hii 31/05/2014 akitokea nchini Marekeni alipokuwa ziarani yapata miezi mitatu.
Wafuasi wa Railla Asubuhi ya leo

Mapokezi yalikuwa makubwa na yaliandaliwa na wanachama na wafuasi wa mrengo wa CORD, ukifanyika jijini Nairobi katika bustani za Uhuru park. Mkutano huo wa kumpoke Mh.Raila ulihudhuriwa na maelfu ya wananchi kutoka pande zote Kenya.

Wakati akiongea na wananchi Mh. Railla aliyazungumzia mambo mengi yaliyotokea nchini Kenya

Hotuba Ya Mh.Railla Odinga 
Mh.Raila Odinga
"Niko na furaha kubwa sana kurudi nyumbani,kwani nilikuwa Marekani yapata miezi mitatu.Nilipata nafasi kuhutubia katika Vyuo vikuu mbalimbali pia vyuo vya ufundi tofauti tofauti nchini humo.

Nimewaleteeni salamu kutoka katika nchi ya Barack Obama mdogo na nimeifikisha katika nchi ya Barack Obama mkubwa.

Nawashukuru sana watu wote walioacha kazi zao na kuja kunikaribisha nyumbani, sita wahi kuisahau hii siku katika maisha yangu. Nawashuku Stephen Kalonzo,Mosess Wetengula,Anyang' Nyogo na timu nzima ya uwongozi kwa kuiongoza upinzani vyema wakati wote nilipokuwa nje, na waliweza kuwanganisha wanaCORD na tukabaki na mungano imara.

Katika Miezi yote mitatu niliyokuwa nje Wakenya walikuwa wakiwasiliana nami wakinieleza kero zao, wengine walinipigia simu,wengine waliniandikia barua, pia wengine walitumia Twitter kunielezea kero zao.
Mtoto aliyepigwa risasi Mombasa na mama yake kuuwawa niliskia, suala la kuongezeka kwa utovu wa usalama ambao unamhadhiri mdogo na mkubwa niliskia pia. Wakenya wamekuwa wakibaguliwa kwa dini zao kama vile waislamu wa Mombasa wanavyo nyanyaswa kuitwa magaidi.

Pia kama nilipokuwa nje Pesa za wananchi ziliibwa kulipwa kampuni hewa za marafiki wa rais kwa njia ya digitali, Watalii pia waliikimbia Kenya,pia watu wengi maelfu walipoteza kazi zao.

Pia bwana Raila Odinga aliweza kuiambia serikali kuwa iandae mkutano wa mapema iliwaweze kuongelea hali ya sasa ya nchi hiyo ya Kenya. Viongozi waote wa Cord waliweza kusema kwa pamoja kuwa siku ya saba saba itakuwa ndio siku yenyewe ya mkutano huo.

Wafuasi wa Cord Katika Uwanja Wa Uhuru Park

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score