Wednesday, July 9, 2014

Brazili Wanyolewa Bila Maji Wembe Uliotumika Ni Chuma Cha Ujerumani.

Brazili Imeondolewa Hapo jana Katika Mechi Ya Nusu Fainali Kwa Kichapo Cha Mbwa Wa Sokoni Pale Ilipokandamizwa Mabao 7:1.
Timu Hiyo Iliyoandaa Kombe La Dunia Kwa Mbwembwe Nyingi Iliweza Kubanduliwa Na Wajerumani Usiku Wa Jana.

Umakini wa vijana wa Joachim Low ulikuwa wa kupigiwa mfano walipoiadhibu Brazil na kuwa timu ya kwanza kuwahi kushindwa kwa mabao mengi zaidi katika hatua hiyo ya nusu fainali ya kombe la dunia.
Kabla ya mechi hiyo vyombo vya habari vilikuwa vimemulika mfumo wake Luiz Felipe Scolari vikidai alikuwa ameumba timu yake kumtegemea Neymar.
Kujeruhiwa kwa Neymar Ijumaa iliyopita ilimlazimu Scolari kubadili mfumo ambao sasa haukuwa na nyota huyo.

Hebu Fuatilia Linki Ifuaatayo Kuweza Kutazama Magoli Yalivyokuwa Yakiminika.
http://www.fifa.com/worldcup/videos/highlights/match=300186474/index.html

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score