Tuesday, July 15, 2014

Huku kombe La Dunia Likiwa Limefika tamati Basi Usikose siri Hii Aliyoambiwa Gotze Kabla ya Kuingia Kwenye Mechi Yao Ya Fainali. Ambapo Gotze Alikuwa Shujaa Wa Ujerumani.

Ujerumani Katika Picha Moja 
Kocha wa Ujerumani, Joachim Loew ametoboa siri kwamba alimwambia shujaa wa fainali ya Kombe la Dunia 2014 Mario Gotze aidhihirishie dunia kuwa ni bora kuliko Lionel Messi. 


Goli moja la Gotze la dakika za nyongeza ndio lilipeleka kilio Argentina huku kombe hilo likitua Ujerumani.
Na baada ya sherehe za ubingwa wa  Dunia 2014, kocha wa Ujerumani, Joachim Loew alisema kuwa alimpa  nasaha moja Gotze kabla ya kumuingiza uwanjani akitokea benchi.  
Captain Wa Ujerumani Akishangilia kombe la Dunia
Law alimwambia mchezaji huyo kuwa aingie uwanjani na kuionyesha dunia kwamba ana kiwango kikubwa kuliko mshambuliaji huyo wa Argentina.  “Nilimwambia Gotze baada ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza cha muda wa zia


Timu Ya Ujerumani Ikipokelewa Nyumbani Ujerumani



da, 'dhihirisha kwamba wewe ni mchezaji bora kuliko Messi, onyesha kuwa una kiwango kumpiku yeye, kiwango ambacho kinaweza kushinda Kombe la Dunia,” Loew aliwaambia wanahabari baada ya mechi.
mashabiki Wa Ujerumani Wakiwashangilia Mashujaa Wao 
Baada ya kazi kuwa ngumu hadi dakika za mwisho  huku  mchezo ukionekana ungeamuliwa na penalti, wachezaji wawili ambao waliingizwa kama nguvu mpya ndio walioishia kuikomboa Ujerumani.
Andre Schurrle alipokea mpira wa pembeni mwa uwanja upande wa kushoto kutoka katikati na kutimka nao huku akiandamwa na mabeki wawili wa Argentina.
Lakini maarifa yake ya kuzalisha krosi ya haraka iliyowapenya katikati madifenda, yalimfikia vyema Gotze kwenye eneo la hatari. Naye hakusita kuutuliza kwa kifua kabla ya kupiga kiki kali lililojaa katika wavu wa kipa Romero Rodriguez huku ikiwa imesalia dakika tatu pekee kabla ya mchezo kwenda hatua ya penalti.
Gari Walilotumia Timu Ya Ujerumani Wakiwa Munich
Bao hilo lilitosha kuwapa Ujerumani taji hilo kwa mara ya nne, makombe ya awali wakishinda 1954, 1974  na 1990.
Huku Ujerumani wakisherehekea ufanisi wao, Messi ambaye alituzwa kuwa mchezaji bora wa dimba hilo amewalaumu mafowadi kwa kupoteza nafasi nyingi za wazi ambazo zingewapa ubingwa badala ya wapinzani wao.

Baadhi Ya Wachezaji Wa Ujerumani Wakishangilia 
“Hatukustahili tuliyoyapata na ukweli ni kuwa mastraika walipoteza nafasi za kufunga tulizopata. Hilo linauma sana sababu si jambo rahisi kupoteza pembamba namna ile,” Messi alisema.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score