Sunday, March 24, 2013

KENYA YAFANYA KWELI YAIBANA NAIGERIA NYUMBANI

Kenya yaibana Nigeria nyumbani kwao

Harambee Stars ya Kenya licha ya kupata mateso tangu wawasili nchini Nigeria kucheza na Super eagles katika mechi ya kutafuta kuingia katika kombe la dunia Jumamosi nusura wawaaibishe mabingwa wa Afrika kwa kutoka sare ya 1-1 huko mjini Calabar , Nigeria.
Timu ya Harambee Stars
Kenya ndio iliyokuwa ya kwanza kufunga kupitia mchezaji Francis Kahata katika dakika ya 36 kipindi cha kwanza.
Licha ya Sduper Eagles kuwateremsha miamba yake yote kama vile John Obi Mikel na Victor Moses wa Timu ya Chalsea ya Uingereza lakini hawakufua dafu kwa kenya hadi katika dakika za majeruhi ya kipindi cha pili.
Katika dakika hizo za majeruhi mcherzaji Nnamdi Oduamadi aliiondolea Super Eagles aibu kwa kufunga bao na punde tu firimbi yamwisho kumaliza mechi ikapulizwa.
Mara ya mwisho kwa timu hizo kukutana ni katika mechi ya kirafiki mwezi Machi ,2011 Mjini Abuja ambapo Super Eagles ilifunga 3-0.
Wakati ambapo harambee Stars ya Kenya ilikuwa karibu sana kuifunga Nigeria ni katika mechi iliyochezwa Januari 12, 1997 wakati timu zote mbili zilitoka sare ya 1-1 mjini Nairobi. Lakini katika mechi ya marudio iliyochezwa Nigeria Juni 7 .1997 Nigeria iliizaba Harambee Stars 3-0. Hii vile vile ilikuwa ni mecchi ya kutafuta nafasi ya kucheza Kombe la Dunia la mwaka 1998.
Miaka iliyopita Nigeria imekuwa ikiipepeta Kenya . Katika mechi ya kutafuta nafasi ya kucheza kombe la dunia mwaka 1986, Harambee Stars walifungwa na Super Eagles 3-0 hii ilikuwa Juni 7, 1985 na baadae kukamilishi kibarua chao na kufaulu kuingia kombe la dunia kwa kuichapa Kenya 1-3
Wachezaji Harambee Stars: Arnold Origi, David Owino, Mulinge Munandi, David Ochieng, Brian Mandela, Victor Wanyama, David Gateri, Johanna Omollo, Jamal Mohammed, Dennis Oliech and Francis Kahata. Coach Adel Amrouche
Wachezaji wa Super Eagles: Vincent Enyeama, Solomon Kwambe, Godfrey Oboabona, Kenneth Omeruo, Elderson Echejile, Sunday Mba, Mikel Obi, Eddy Onazi, Obafemi Martins, Victor Moses and Brown Ideye

Waamuzi

Referee: Joshua BONDO (BOT)
Assistant Referee 1: Meshack MEDUPI (BOT)
Assistant Referee 2: Moemedi MONAKWANE (BOT)
Fourth official: Kutlwano LESO (BOT

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score