Thursday, October 31, 2013

Kitengo cha kupambana na ujangili Tanzania chatuhumiwa kwa kukiuka haki za binadamu

Kampeni ya kupambana na ujangili Tanzania
imeingia matatani baada ya tuhuma za ukiukaji
wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na
kuteka nyara na kuua mwanamke, gazeti la The
Citizen la Tanzania liliarifu hapo Jumatano
(tarehe 30 Oktoba).

Kitengo cha kupambana na ujangili,
kinachojumuisha polisi, jeshi na maafisa wa
kiintelijensia, kilidaiwa kumtia kizuizini Emaliana
Gasper Maro, mwenye umri wa miaka 46, siku
kadhaa baada ya kumkamata mume wake Elias
Kibuga, mwenye umri wa miaka 56. Kibuga
amekuwa haonekani tangu alipochukuliwa kwa
ajili ya kuhojiwa, lakini mwili wa Muro
ulionekana katika mochuari ya Hospitali ya
Mirara.
Watu wengine wengi wanaripotiwa kutoonekana,
na maafisa pia wanashukiwa kwa kuwachomea
moto nyumba zao.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara Akili
Mpwapwa alithibitisha ripoti hizo na kusema
uchunguzi ulikuwa unaendelea.
Joseph ole Parsambei wa Jukwaa la Wachungaji
Tanzania alisema kwamba kitengo cha
kupambana na ujangili pia kilikuwa
kinawashikilia wachungaji 27 na mifugo 2,169.
"Tutakwenda mahakamani kuzuia zoezi hili ikiwa
ukiukwaji wa haki za binadamu utaendelea,"
alisema.
Waziri wa Maliasili na Utalii Khamis Kagasheki,
ambaye aliripotiwa kuanzisha kampeni ya
kupambana na ujangili, alikataa kutoa maoni
yoyote.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score