Tuesday, December 31, 2013

BAADA YA OPARESHINI YA TOKOMEZA MAJANGILI KUSITISHWA, VIFO ZA TEMBO VYAONGEZEKA ZAIDI TANZANIA

Kiasi cha tembo 60 wameuawa nchini Tanzania
ndani ya miezi miezi tangu serikali
ilipolazimishwa kusitisha operesheni yenye utata
ya kupambana na ujangili, alisema Naibu Waziri
wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalangu siku ya
Jumapili (tarehe 29 Disemba).

Rais Jakaya Kikwete aliwafukuza kazi mawaziri
wanne mwezi huu kukiwa na tuhuma kwamba
operesheni hiyo ya nchi hiyo dhidi ya ujangili
ilipelekea vikosi vya usalama kufanya matendo
kadhaa yaliyovunja haki za binadamu ikiwemo
kuwauwa washukiwa, mateso na ubakaji.

Lakini Nyalandu alisema angalau operesheni
hiyo ilikuwa imepelekea kupungua kidogo kwa
ujangili. Chini ya operesheni hiyo ya kupambana
na ujangili, vikosi vya usalama vilifanya kazi kwa
sera ya "kupiga risasi na kuua" na kukamata
watu wengi.

"Ndani ya kipindi chote cha operesheni, tembo
wawili tu waliripotiwa kuuawa ambapo sasa
tembo 60 walichinjwa kati ya tarehe 1 Novemba
na 28 Disemba," alisema Nyalandu kwa mujibu
wa shirika la habari la AFP.

Alisema sasa Tanzania itaziomba serikali na
taasisi za mataifa mengine kwa msaada wa
namna gani ya kuendelea nayo.
"Wale watakaoombwa ni pamoja na Umoja wa
Ulaya na nchi za Asia.

Nchi za Asia zinaripotiwa
kuwa watumiaji wakubwa wa pembe za ndovu
na mambo yanatokanayo nazo," alisema
Nyalandu, akiongeza kwamba idara ya
wanyamapori ya Tanzania na shirika la ulinzi wa
wanyama hao vinapaswa kuimarishwa.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score