Friday, January 3, 2014

Mashambulizi mengine Mombasa yajeruhi 10

Mashambulizi mengine Mombasa yajeruhi 10

Nchini Kenya watu 10
wamejeruhiwa wakati
washambuliaji waliporusha
guruneti ndani ya mkahawa
mmoja katika mji wa pwani
wa Mombasa na kuzusha
hofu ya usalama katika
eneo hilo tete.

Mkuu wa polisi mjini Diani,
Jack Ekakuro, amesema
washambuliaji hao
waliilenga baa moja iitwayo
Tandoor mjini Diani
mapema leo, wakati
ilipokuwa bado imefurika
watu waliokuwa
wakiendelea kusherehekea
mwaka mpya.

Hii ni
sehemu ya mlolongo wa
mashambulizi, ikiwa ni
pamoja na lile la bomu
kwenye basi moja katika
mtaa wa Eastleigh mjini
Nairobi mwezi uliopita, hali
inayowatia wasiwasi
Wakenya wengi.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score