Wednesday, July 30, 2014

Hatimaye Mkenya Wa Pili Atua Ligi Kuu England.... Atashiriki Michuano Mikubwa Ya UEFA

Divork Origi Na Sakfu Ya Liverpool.

London: Hatimaye, klabu ya Liverpool imemsajili mshambuliaji wa chipukizi, Divock Origi Mkenya/Mbelgiji akitokea Klabu yake ya Lille aliyojiunga nayo akiwa na miaka 15.

Mchezaji huyo mwenye miaka 19 ameukubali mkataba wa miaka mitano lakini ataendelea kubaki kwenye klabu yake huko Ufaransa kwa mkopo katika msimu ujao kabla ya kuhamia Anfield mwaka ujao 2015.

“Ninayo furaha kwa klabu kubwa kama Liverpool imenisajili,” Origi alisema.
Origi alicheza mechi zote tano za Ubegiji katika fainali za Kombe la Dunia la mwaka huu wakati wakipigana kuelekea robo-fainali na kuifungia timu yake bao dhidi ya Urusi.
Mbali na Origi, Liverpool pia imewanunua Rickie Lambert, 32, akitokea Southamptom na kiungo wa wa kati Adam Lallana, 25,  kutoka Southampton.
Kadhalika imewanasa Emre Can, 20 akitokea Bayer Leverkusen na winga Lazar Markovic, 20, akitokea Benfica.
Mlinzi Dejan Lovren, 25 akitokea Southamptom pia amehamia Anfield.
“Najua hii ni klabu yenye historia kubwa, wachezaji wakubwa  na mashabiki wengi,” aliongeza.
“Kwangu Liverpoool ni moja ya vilabu bora kabisa duniani na ninayo furaha sana kuwa sehemu ya historia hii.
Origi ambaye asili yake ni Kenya alianzia katika klabu ya Genk alichochezea babake, Mike Okoth kabla ya kuhamia Lille.


TETESI ZA SOKA ULAYA

Beki was Aston Villa Ron Vlaar, 29, atakuwa
 na mazungumzo na meneja wake Paul Lambert kuhusiana na hatma yake licha ya Southampton kumwania (Daily Mirror), QPR wanafikiria kumchukua kiungo wa Colombia Carlos Sanchez, 28, kwa pauni milioni 4 kutoka Elche (Daily Mirror), West Ham na QPR wamepanda dau kwa Marseille kumchukua Matheiu Valbuena baada ya kiungo huyo Mfaransa kukataa kuhamia Dynamo Moscow (L'Equipe), Manchester United na Barcelona bado wanamfuatilia Juan Cuadrado, 26, wa Fiorentina lakini huenda wakatishwa na bei ya pauni milioni, 32, ya kiungo huyo kutoka Colombia (Marca), Manchester United wamefikia makubaliano "ya mdomo" na kiungo wa Juventus Arturo Vidal, 27, ya uhamisho wa pauni milioni 47 (Tuttosport), matumaini ya Manchester City kumsajili beki kutoka Morocco Mehdi Benatia, 27, yamefifia baada ya Roma kusema hakuna dalili za mchezaji huyo kuondoka (Le Figaro), meneja mpya wa Manchester United amewaonya mashabiki wake kuwa timu hiyo huenda ikasuasua katika miezi mitatu ya mwanzo wa msimu wakati wachezaji wakianza kuzoea mbinu zake (Times), Van Gaal amesema iwapo watashinda Ligi Kuu msimu ujao na kuwapiku majirani zao Manchester City, utakuwa ushindi "mtamu" zaidi (Manchester Evening News), kiungo wa Manchester City Yaya Toure, 31, amesema huenda akasalia katika timu hiyo hadi atakapoacha kucheza soka (Guardian), mshambuliaji mpya wa Barcelona Luis Suarez, 27, ambaye anatumikia adhabu ya miezi minne, amehamia katika mji wa Pyrenees kuanza mazoezi ya msimu mpya akiwa na mwalimu binafsi (Daily Mail), Didier Drogba, 36, amesema Diego Costa, 25, atakuwa mchezaji "mkali" katika Ligi Kuu ya England (Sun), AC Milan wanafanya mazungumzo wa mshambuliaji kutoka Brazil Robinho, 30 (Le Figaro), kiungo wa Arsenal Santi Cazorla,29, bado anasakwa na Atlètico Madrid. Atlètico pia wanamfuatilia Fernando Torres, 30, na winga wa PSV Eindhoven Zakaria Bakkali, 18 (AS.com), kiungo anayefuatiliwa na Liverpool, Xeridan Shaqiri, 22, huenda akaamua kubakia na klabu yake ya Bayern Munich (Tuttosport), Borussia Dortmund na Schalke wanamtaka mshambuliaji kutoka Serbia, Aden Ljajic, 22, kutoka AS Roma (Bild), Barcelona wametangaza kumsajili kiungo kutoka Brazil, Alex Varoneze Dione anayejulikana kama "Betri" kwa miaka mitatu (Mundodeportivo), Manchester United wameanza tena kumfuatilia beki wa kati wa Atletico Madrid Miranda, baada ya Atlètico kusema wapo tayari kupokea dau la pauni milioni 23 (Metro), AC Milan wanamtaka winga wa Newcastle Hatem Ben Arfa na huenda akauzwa kwa pauni milioni 12 (Daily Star), Bayern Munich wapo tayari kusubiri hadi Oktoba kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdez ambaye anauguza jeraha la goti, ingawa anaweza kusita kwenda kugombea namba na Manuel Neuer (Mundo Deportivo), QPR wanataka kumchukua Ronaldinho ambaye amemaliza mkataba wake na Atletico Mineiro (Globoesporte) na Chelsea wanakataa kutengeneza jezi zenye jina la kipa Thibaut Courtois, 22 na Romelu Lukaku, 22, kwa sababu wachezaji hao bado hawajapewa namba (Daily Star).

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score