Saturday, September 6, 2014

Mwanaume Mmoja Afunga Ndoa Na Maiti..... Ni Wapi Fuatana Nami Mchimba Riziki Nikujuze


MWANAMUME alishangaza familia yake, marafiki na wanakijiji alipoamua 'kufunga’ ndoa na marehemu mkewe katika kijiji cha Kadzinuni, tarafa ya Kikambala, Kaunti ya Kilifi wakati wa mazishi yake.

Kiti Mwangudza Chilango aliamua kutimiza ahadi aliyokuwa amempatia mkewe miaka michache iliyopita kwamba wawili hao wangefunga ndoa rasmi.

Akiwa amevalia suti, Bw Chilango alisimama kando ya jeneza la mkewe akiwa pamoja na msafara wa wasimamizi wake sawa na jinsi inavyofanyika wakati wa harusi.

Pia kulikuwepo na keki ambayo aliikata na kisha ikagawanywa kwa waombolezaji kabla ya mwili kuzikwa.

Kulingana na rafiki wa karibu wa marehemu, Bi Mbeyu Mbura, Bw Chilango alikuwa amemuoa kwa kitamaduni lakini mkewe alikuwa akishinikiza wafanye harusi kanisani.

Bi Mbeyu alifichua kuwa marehemu ambaye alikuwa akiugua ugonjwa usiojulikana alikuwa amemtaka mumewe aape kuwa atamheshimu kwa kumfanyia harusi awe hai ama akiwa amekufa, na ndio sababu mumewe hakuwa na namna nyingine ila kutimiza ahadi hiyo.

“Tunahofia kuwa kitu kibaya huenda kikatokea kwa mumewe ama familia ikiwa ombi la marehemu halitatimizwa. Mumewe anaweza hata kufa,” alieleza Bi Mbeyu.

Mzee wa kijiji Kai Mwandeje alisema kuwa hakuna jambo kama hilo limewahi kutokea eneo hilo na kusema kuwa kitendo hicho huenda kikaleta matatizo mengine baadaye ikiwa mume ataamua kuwa anataka kuoa tena katika siku za usoni.

“Kuvalia mavazi ya harusi kunamaanisha kuwa roho ya mume tayari imeunganishwa na ya marehemu. Itakuwa vigumu kuoa tena isipokuwa kama ahadi hiyo itavunjwa,” alisema Bw Kai.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score