Friday, December 5, 2014

Kesi Ya Uhuru Kenyatta Imetupiliwa Mbali.

Wakenya Wakionyesha Furaha Baada Ya Uhuru Kufutiwa Kesi
Habari zilizofika mapema hivi leo zinasema mwendesha mashitaka wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC Fatou Bensouda, ametupilia mbali mashitaka dhidi ya Rais wa Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Mapema wiki hii mahakama ya kimataifa ya uhalifu  ICC ilimpa wiki moja mwendesha mashitaka huyo kuongeza  kasi ya uchunguzi ama kuyatupilia mbali mashitaka dhidi ya Rais Kenyatta.
Mh.Uhuru Kenyatta
Kesi hiyo iliahirishwa mara kadhaa na mahakama hiyo ya The Hague, na Jumatano ilisema kwamba kuchelewa zaidi kungeweza kuwa kinyume na maslahi ya haki katika mazingira yaliyokuwepo.
Rais Kenyatta alikabiliwa na mashitaka dhidi ya ubinadamu akishutumiwa kupanga ghasia za  baada ya uchaguzi mwishoni mwa mwaka 2007 na mapema 2008. Ghasia hizo zilisababisha vifo vya watu 1,100 huko Kenya na kuwakosesha makazi wengine zaidi ya nusu milioni.
Rais Kenyatta mara kadhaa amesema yeye hana hatia.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score