Saturday, March 9, 2013

HATIMAE RAIS WA NNE APATIKANA NCHINI KENYA


HABARI ZA KUAMINIKA NI KWAMBA LEO RAIS WAKENYA ATATANGAZWA RASMI..
NAE NI UHURU MOIGAE WA KENYATTA.
Kwa matokeo yaliyo tolewa na Tume ya IEBC sinaonyesha ya kwamba mgombea uris kwa mrengo wa Jubelee ameweza kufikisha idadi ya kura sinazotakiwa kikatiba..Bwana uhuru amefikisha kura 6,173,433 ambayo ni sawa na asilimia {50.03}ya kura yote ilopigwa mnamo march 4 2013.Jumla ya kura iliyopigwa ni kura 12,338,667.

Nae waziri mkuu wa kenya ambae alikuwa akigombea kiti hicho cha urais kwa awamu ya tatu sasa kupitia mrengo wa Cord aliweza kujizolea kura 5,340,667 kati ya kura 12,338,667 zilizopigwa na wakenya.Bwana Raila jana aliwaalika waandishi wa habari katika kambi iliyoko mjini Nairibi mtaa wa Karen lakini akaamua kuahirisha mkutano huo mpaka leo 09/03/2013..Kwa hiyo tunatarajia leo hii kuskia bwana Raila Odinga akihutubia waandishi wa habari.




 
IEBC leo itamtangaza rais wa jamhuri ya Kenya ailiye pita kikatiba saa 11am.Wakenya wengi walianza kusherehekea ushindi huo kuanzia mida ya saa kumi usiku katika mitaa tofauti katika jiji la Nairobi.Mavuvu zela yalipulizwa sana shwange na nderemo za kila aina zilikuwa katika mtaa huu wa Eastlegh wenye wafuasi wengi wa Jubelee coarlition.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score