Monday, August 26, 2013

MESSI ; JERAHA LINALOMKABILI MSHAMBULIAJI HUYO MATATA WAITIA TUMBO JOTO BARCELONA

Wasiwasi umewakumba mabingwa hao wa Hispania Barcelona kufuatia jeraha linalomkabili mshambuliaji wao matata Lionel Messi.
Mshambuliaji huyo raia wa Argentina ambaye ndie injin ya klabu ya Barcelona aliumia katika mechi ya Spanish Super Cup dhidi ya vijana matata wa Atlatico Madrid jumanne ambayo walitoka sare ya 1-1 .
Katika mechi hiyo iliyochezwa katika uwanja wa Vicente Caldeton, Messi alitolewa na nafasi yake kichukuliwa na kiungo Cesc Fabrigas.

Nyota wa Brazil aliwaepusha Barcelona aibu baada ya kufunga bao moja la kusawazisha baada ya nyota wao wa zamani, kuwafunga na kuweka Atletico kifua mbele.
"Messi alitolewa nje akihisi maumivu katika mguu wake wa kushoto baada ya kugongana na mchezaji mwingine wa Atletico"klabu ya Barcelona ileipoti jana katika mtandao wake.
Staa huyo alipata jeraha dogo Wiki jana akifanya mazoezi lakini akapona na kuweza kucheza mechi dhidi ya Levante ambapo walishinda 7-0
Umuhimu wa Messi kwa Barcelona ulijulikana msimu uliopita alipokosa mechi za nusu fainali ya ligi ya mabingwa bara Ulaya dhidi ya Bayern Munich.
Barca walitwangwa jumla ya Mabao 7-0 nyumbani na ugenini.

Mchimba Riziki Sports


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score