Thursday, March 13, 2014

Klabu Nyingi Za Bara La Afrika Zinatumia Uchawi Katika Soka..... Je unaamini Katika Nchi Yetu Kuna Timu Kubwa Inayotumia? Fuatilia Hapa ujue ni Timu gani.........

Klabu nyingi za Afrika zinatumia uchawi ili kung'ara katika Ligi ya Mabingwa Afrika, CAF Champions League, baadhi ya wanasoka maarufu barani humu wamesema.
Yanga Ya Tanzania
Uchawi umezungumziwa sana katika mijadala kuhusu soka ya bara na ingawa ilikuwa imepungua, kuna dalili kuwa matumizi ya ndumba unarejea katika mashindano makubwa.

Klabu maarufu ambazo zimefana katika ligi hii zimedaiwa kushiriki shughuli hiyo hata katika ligi za nyumbani.
Tukio la kwanza lilihusu klabu ya Morocco Raja Casablanca iliyocheza dhidi ya Horoya kutoka Guinea ambapo kipa wao alinaswa akipanga vifaa visivyojulikana katika lango lake.

Hata hivyo, Horoya ilishinda mechi hiyo 5-0 kwa njia ya penalti na kuondoa timu hiyo iliyoshiriki Kombe la Klabu Bingwa Duniani.

Katika hatua hiyo, kipa wa Yanga Deo Munish alionekana akifunga goli lake kwa uzi katika mechi dhidi ya Al Ahly jijini Alexandria, Misri lakini wenyeji wakaitoa.
SHUHUDA
“Niliona kipa wa Yanga akifanya vituko kabla ya mechi kuanza. Nilikuwa na jeraha na ilibidi nitizame mechi kwa nyumba na mara hiyo nilimpigia simu maafisa wa benchi la kiufundi kuwajulisha nilichoona. Mwanasoka mwenzangu alienda kwenye lango na kuuondoa uzi huo na hatimaye tulishinda mechi,” Walid Soliman aliambia supersport.com.

Kiungo wa Al Ahly Hossam Ashour amesema kuwa anaamini nguvu za uchawi katika ufanisi wa soka.
“Ndio nina imani na matumizi ya vitu hivyo na hatukufunga dhidi ya Yanga kwa kuwa tulikuwa na wasiwasi.”

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score