Saturday, May 24, 2014

Chelsea Kama Ndio Timu Ya Dunia Vile...


RIO DE JANEIRO: Chelsea inaongoza kwa kuwa na wachezaji wengi zaidi katika vikosi vya timu za taifa zitakazoshiriki fainali za Kombe la Dunia.
Mashabiki Wa Chelsea Darajani.
Timu hiyo ina wachezaji 18 na kuzipiku timu nyingine kubwa kama Manchester United na Bayern Munich.

Hata Napoli ya Italia ina wachezaji wengi kuzipiku timu za Barcelona na Real Madrid.
Man United na Bayern kila mmoja ina wachezaji 16 katika vikosi mbalimbali vinavyojiandaa kwa michuano hiyo.
Brazil ambao ndio wenyeji wa fainali hizo wameita kikosini wachezaji wanne wa Chelsea ambao ni Oscar, Willian, Ramires na Davdi Luiz.
Wachezaji wengine wa Chelsea ni Frank Lampard na Gary Cahill walio katika timu ya Uingereza.
Uhispania ina Fernandos Torres na Cesar Azpilicueta wakati Ubelgiji ikiwa na Eden Hazard, Romelu Lukaku na Thibaut Courtois.
Mstaa wengine wa Chelsea kwenye vikosi vya taifa ni Samuel Eto’o (Cameroon), Andre Schurrle (Ujerumani) na Wanigeria -John Obi Mikel, Victor Moses na Kenneth Omeuro.
Kadhalika kuna Mghana Christian Atsu na Patrick van Aanholt wa Uholanzi.
Timu nyingine zenye wachezaji wengi ni pamoja na Barcelona, Real Madrid, Manchester City (13), Juventus, Arsenal, Liverpool (12), Atletico Madrid (11), Porto, Inter Milan, AC Milan, Zenit (10) na Borussia Dortmund, Paris Saint- Germain (8).


Kikosi Kamili Cha Chelsea Brazili Ndio Hiki Hapa Chini.
 Andre Schurrle
Cahill
Cesar
Christian Atsu
Eden
Samuel Etoo
Mikel Obi
Kenneth Omeuro

Lampard
Luis

Lukaku

Victor Mosess

Oscar

Patric van


Ramires


Thibaut Courtois.


Toress

Willian







0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score