Saturday, May 24, 2014

Hawa Ndio Wasamini Na Waanzilishi Wa Kundi Hatari La Boko Haramu..............

Chapa Za CIA na Boko Haramu
Randy Short mchambuzi wa masuala ya kisiasa wa nchini Marekani amelituhumu Shirika la Kijasusi la Marekani CIA kwa kuhusika na uundwaji wa kundi la Boko Haram la nchini Nigeria na uungaji mkono wa kifedha kwa kundi hilo linaloendesha ghasia na machafuko nchini humo.

 Randy Short ameongeza kuwa, lengo la Marekani la kuliunga mkono kundi la Boko Haram ni kutaka kuidhoofisha Nigeria na kupunguza ushawishi wa nchi hiyo magharibi mwa Afrika.

Mchambuzi huyo wa Kimarekani ameeleza kwamba, Marekani inadhamini mahitaji ya silaha na fedha ya kundi hilo kupitia Jenerali mstaafu Khalifa Haftar aliyesomea mafunzo ya kijeshi nchini Marekani ambaye hivi sasa anaendesha operesheni za kimapinduzi nchini Libya.

Randy Short ameongeza kuwa, hatua ya Marekani ya kutaka kushiriki kwenye operesheni za kutaka kuwaokoa wanafunzi wasichana wasiopungua 250 wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haram, ni njama za nchi hiyo za kutaka kupenya na hatimaye kulidhibiti eneo la Magharibi mwa Afrika.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score