Monday, July 21, 2014

Mkenya Aliyecheza World Cup Kutua Liverpool

Liverpool inakaribia kufikia maafikiano na klabu za Southampton kumnunua beki Dejan Lovren na klabu ya Lille ili kupata saini ya mshambuliaji Mkenya Divock Origi.
Divorck Origi

Kulinganana BBC, The Reds ambao kwa wakati huu wako ziarani nchini Marekani wameripotiwa kufikia makubaliano na Lille kumsajili Origi raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Kenya kwa dau la Sh1.5 bilioni. Kwa wiki kadhaa sasa Liverpool imekuwa ikimsaka mshambuliaji huyo huku kukichapishwa ripoti kadhaa za maafikiano baina ya pande zote ila taarifa hizo hazijawahi kuwa rasmi.
Kumhusu mlinzi Lovren mwenye umri wa miaka 25, Liverpool waliwasilisha ofa ya Sh3 bilioni juma lililopita ila ilikakataliwa. Hata hivyo Lovren raia wa Croatia ameelezea nia yake ya kutaka kuhamia Liverpool hatua ambayo imeanza kuwafanya Southampton kuwaza mara mbili.
Mlinzi huyo amewasilisha barua kwa klabu hiyo ya kuwataka wamruhusu aondoke ikiwa ni baada ya kutumikia mwaka mmoja wa mkataba wake wa miaka minne nao.
Liverpool ambao watashiriki Ligi ya mabingwa msimu ujao kwa mara ya kwanza tangu 2009, wamekuwa wakikirutubisha kikosi chao na hadi kufikia sasa baada ya kuondoka kwa nyota wao Luis Suarez aliyetua Barcelona, wamefanikiwa kuwasajili wachezaji sita.

Mshambuliaji Loic Remy alijiunga nao Jumapili baada ya klbu ya QPR kukubali ofa yao ya Sh1.2 bilioni. Kando na mchezaji huyo, kocha Berndan Rodger ameanunua Adam Lallan, Rickie Lambert, Lazar Markovic na Emre Can...

Kwa tetezi nyingi za soka usikose kujiunga nasi kila mara....

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score