Friday, November 29, 2013

MWANAUME AVUMANIWA AKIVUNJA AMRI YA SITA NA MBUZI NI HUKO MALINDI:


Mwanamume wa miaka 20 amepigwa na
kujeruhiwa vibaya na wananchi baada ya
kufumaniwa akishiriki kitendo cha ngono na
mbuzi kijijini Dabasom lokesheni ya Watamu
wilayani malindi.

MWANAMUME wa miaka 20 Alhamisi alipigwa na
kujeruhiwa vibaya na wananchi baada ya
kufumaniwa akishiriki kitendo cha ngonona
mbuzi kijijini Dabasom lokesheni ya Watamu
wilayani malindi.

Moses Katana alionekana na mwenye
mbuzi huyo ambaye alipiga mayowe
yaliyowavutia wanakijiji waliomkabili mshukiwa.

Baada ya kutandikwa vya
kutosha, mshukiwa
alikokotwa hadi ofisini
kwa chifu wa Dabaso Bw
Joseph Baya Maitha,
ambapo chifu aliwataka
maafisa wake wa polisi
wa utawala waingilie kati
na kumwokoa mshukiwa
aliyekuwa akiendelea kurushiwa makonde.

Baadaye mwanamume huyo alipelekwa katika
makao makuu ya polisi mjini Malindi na
kufunguliwa mashtaka ya kufanya kitendo cha
ngono na mnyama.

Chifu Baya alisema kwamba visa vya vijana
kupatikana wakishiriki vitendo vya ngono na
wanyama vimekuwa vikiongezeka mno katika
eneo hilo, na akawatahadharisha kwamba
watakabiliwa na mkono wa sheria iwapo
watapatikana.

Msomaji wangu kwa hayo yote nakuomba jaribu kuyapitia maandiko ya Mungu ili uweze kuyakemea mapepo kama haya.

Kumbukumbu La Torati 27:21 ama soma Kumbukumbu la Torati yote 27.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score