Thursday, November 28, 2013

Uganda yateua naibu mpya wa kamanda wa kikosi cha AMISOM

Meja Jenerali Geoffrey Baraba Maheesi wa
Uganda, ambaye ameteuliwa kuwa naibu
kamanda wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini
Somalia (AMISOM), aliwasili nchini Somalia
Jumanne usiku (tarehe 26 Novemba), gazeti la
Daily Monitor la Uganda liliripoti.

Muheesi amechukua nafasi hiyo katika kipindi
ambacho wanajeshi 24 wa Uganda
walisimamishwa kwa muda mwezi Septemba
kwa kutuhumiwa kuuza chakula kilichokusudiwa
kwa ajili ya wanajeshi wa AMISOM .

Kamanda wa
kikosi cha Uganda Brigadia Michael Ondoga
alikuwa miongoni mwa wale waliosimamishwa.

"Nitapambana kwa kila hali kurejesha utu wa
[Jeshi la Ulinzi la Watu wa Uganda] nchini
Somalia, makosa yamefanywa lakini
tutayarekebisha," alisema Maheesi.

"Ninajua kazi inayotukabili ni ngumu lakini rekodi
za ufuatiliaji wangu ziko wazi na sihusiki na
makosa. Nitaiacha Somalia ikiwa vizuri kuliko
nilivyoikuta," alisema.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score