Thursday, November 28, 2013

Serikali Yatangaza Vita Ya Ukatili Wa Kijinsia na Watoto.

Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi
alitangaza mpango huo wakati wa Siku 16 za
kampeni ya Harakati Dhidi ya Unyanyasaji wa
Kijinsia, kampeni ya kimataifa inayolenga kuinua
uelewa kuhusu suala hili.

Takribani asilimia 45 ya wakina mama wenye
umri wa miaka kati ya miaka 15 hadi 49 waliripoti
kunyanyaswa kimwili au kijinsia katika maisha
yao, kwa mujibu wa Utafiti wa Demografia na
Afya nchini Tanzania wa mwaka 2010.

Watoto nao wako katika hatari kubwa, msichana
mmoja kati ya watatu na mvulana mmoja kati
ya saba wamenyanyaswa kijinsia, na zaidi ya
asilimia 70 walinyanyaswa kijinsia kabla ya
kufikisha umri wa miaka 18.

"Jeshi la polisi linawajibika kuboresha mwitikio
wake kwa manusura wa [ukatili wa kijinsia] na
unyanyasaji wa watoto," Inspekta Jenerali wa
Polisi Said Mwema alisema.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score