Friday, December 27, 2013

KENYA KUHAMA KUTOKA ANOLOJIA KWENDA DIJITALI VITUO VYA TELEVISION KUFUNGWA.

Kenya ilifunga ishara zote za matangazo ya
analojia saa sita ya usiku wa Alhamisi usiku wa jana (tarehe 26
Desemba) kufuatia uamuzi wa mahakama
mapema wiki hii, The Standard la Kenya liliripoti.

Nation Media Group, Standard Media Group na
Royal Media Services zilizima matangazo yao siku
ya Jumatatu katika kupinga kupuuzwa na
Mahakama Kuu kwa ombi lao la kucheleweshwa
kwa uhamaji kwenda dijitali.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia
Fred Matiang'i alisema kaya nyingi zilikuwa
zimejiandaa kuhamia huko dijitali.

"Kati ya TV zipatazo milioni 1.5 million ndani ya
eneo la awamu yetu ya kwanza kuzima, kiasi cha watu
500,000 tayari zimeshahama kwenda dijitali kwa
sababu wamejiunga na ama DSTV au GoTV,"
alisema. "Hilo linatuacha na kiasi cha watu  milioni na
wale wapatao 700,000 ambao tayari
wameshanunua vigamuzi."

Rufaa ya vikundi vya vyombo vya habari
inatarajiwa kusikilizwa mahakamani siku ya leo
Ijumaa.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score