Friday, December 27, 2013

MWALIMU WA DINI APIGWA RISASI MOMBASA

Ulamaa wa Kiislamu alipigwa risasi na kufariki
dunia na wanaume wenye silaha ambao
hawajafahamika usiku wa Jumatano (tarehe 25
Disemba) huko Ukunda, moja ya eneo muhimu
ya utalii nchini Kenya kandokando ya Bahari ya
Hindi, kusini mwa Mombasa, AFP iliripoti.

"Halikuonekana kuwa tukio la kawaida la
ujambazi," Jack Ekakoro, kamanda wa eneo hilo
alisema Alhamisi.
"Alionekana kuwa mlengwa wa
washambuliaji."

Salim Mwasalim, alivyokuwaa akijulikana
mwalimu huyo wa dini mwenye umri wa miaka
60, "alipigwa risasi wakati akitembea kurudi
nyumbani akitokea kwenye msikiti ulio karibu,"
Ekakoro alisema.

"Tunachunguza kujua sababu na kuwapata
washambuliaji," aliongezea, akisema wauaji
walitoroka kwa pikipiki.

Ulamaa mwingine wa Kiislamu Hassan Mwayuyu
alipigwa risasi kwenye mazingira kama hayo, pia
na wanaume wenye silaha waliokuwa kwenye
pikipiki, katika eneo hilo tarehe 6 Disemba.

Mwasalim alikuwa chini ya uchunguzi wa polisi
katika orodha ya wanaodaiwa kutoa mafunzo
kwa vijana kupambana pamoja na al-Shabaab,
chanzo cha polisi kiliiambia AFP.

By Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score