Friday, December 27, 2013

UHURU KENYATTA NA WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA HAILEMARIAM DESALEGN WAIZURU SUDAN YA KUSINI KUTAFUTA AMANI

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Waziri Mkuu
wa Ethiopia Hailemariam Desalegn waliwasili
huko Juba Alhamisi hapo jana (tarehe 26 Disemba) kwa ajili
ya mazungumzo na rais wa Sudani Kusini Salva
Kiir yanayolenga kutatua hali ya kukosekana kwa
utulivu kunakoongezeka katika nchi hiyo,Afp iliripoti.

Viongozi hao walipigwa picha kabla ya kuingia
kwenye mazungumzo ya siri.

Ziara hiyo imekuja
katikati ya jitihada zinazoendelea zinazofanywa
na mataifa yenye nguvu ya kanda hiyo kuzuia
hali isiyo na utulivu kwa takribani wiki mbili.

Wajumbe kutoka Kenya na Ethiopia tayari
walishirikishwa katika jitihada za usuluhishi wiki
iliyopita, wakati mawaziri wa mambo ya nje wa
nchi husika walikuwa mojawapo wa ujumbe wa
kanda huko Juba.

Waziri wa nje wa Kenya Amina Mohammed
ameambatana na Kenyatta kwenda Juba, ofisi
yake ilisema.

Kenya imekuwa ikituma ndege kuhamisha raia
wake kutoka Sudani Kusini , ambapo wengi wana
biashara.

Watu elfu kadhaa wanaaminika waliuawa
tangumapambano yalipozuka Sudani ya Kusini ,
baina ya vikosi vinavyomtii Kiir dhidi ya wale
wanaomunga mkono mpinzani wake Riek
Machar, aliyekuwa makamu wa rais ambaye
alifukuzwa mwezi Julai.

Hali ya kukosekana kwa utulivu imechukua sura
ya kikabila, ikilenga kabila la Dinka la Kiir dhidi
ya Nuer la Machar.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga
kura Jumanne kutuma askari wa ziada karibia
6,000 na polisi kwenda Sudani Kusini, karibia
mara mbili ya kikosi cha Misheni ya Umoja wa
Mataifa huko Jamhuri ya Sudani Kusini hadi
vikosi 12,500 na polisi wa kiraia 1,323.

Umoja wa Afrika (AU) na Mamlaka baina ya
serikali za Maendeleo (IGAD) imeelezea kwa
uwazi wasiwasi juu ya kuongezeka kwa vurugu.

"AU na IGAD zimekuwa na wasiwasi mkubwa
kutokana na ripoti ya uhamasishaji wa
wanamgambo wa kikabila huko Sudani Kusini,
jambo ambalo linatishia kuongezeka zaidi kwa
mzozo na kuingia kwenye vurugu baina ya
kikabila zitakazosababisha uharibifu mkubwa
ambazo zingeweza kuhatarisha taifa liliundwa
hivi karibuni la Sudani Kusini," vikundi hivyo
vilisema katika taarifa.

IGAD inatarajia kufanya mkutano wa wakuu wa
nchi kuhusu mzozo wa Sudani Kusini hapa
Nairobi siku ya leo (ijumaa)

By Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score