Saturday, January 11, 2014

Al-shabab Yakanusha Taarifa Ya KDF

Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) lilisema siku ya Ijumaa (tarehe 10 Januari) kuwa ndege zake za
kivita zililenga kambi ya mafunzo ya al-Shabaab katika mkoa wa Gedo siku ya Alhamisi, na kuua
angalau wanamgambo 30 wa al-Shabaab, wakiwemo makamanda wa juu.

"Mamia ya wengine walikimbia wakiwa na
majeraha mengi.

Zaidi ya magari matano na
zana muhimu viliharibiwa," ilisema KDF kupitia Twitter.
Msemaji wa Al-Shabaab Abdiaziz Abu Musab alikanusha madai ya KDF.

"Hatuna majeshi yaliyopo hapa. Hakukuwa na wapiganaji wa al-Shabaab katika eneo hilo na
hakuna mtu wetu yeyote aliyeuawa," Abu
Musab alisema.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score