Tuesday, January 21, 2014

Ribbery na Benzema Watupwa Mahakama Kwa Kosa La Kufanya Ngono Na Kahaba

Wacheza soka wawili mashuhuri duniani, wamefikishwa mahakamani mjini Paris Ufaransa kwa kosa la kufanya ngono na
kahaba aliyekuwa na umri mdogo.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 21 sasa hivi, alisema kwamba,Franck Ribery, mchezaji wa Bayern Munich , alimtumia kama zawadi
wakati wa sherehe za siku yake ya kuzaliwa mwaka 2009.
Inaarifiwa Ribbery alimlipia msichana huyo tiketi ya ndege aweze kusafiri kutoka Ujerumani Kuja Ufaransa kumtumbuiza Ribbery wakati wa sherehe hizo.
Alisema kuwa pia alilipwa ili afanye ngono na Karim Benzema anayecheza soka yake na klabu
ya, Real Madrid.
Kahaba huyo alisema kwamba, aliwaambia wawili, hao kuwa alikuwa mtu mzima wakati
huo.
Benzema amekanusha madai ya msichana huyo.
Wachezaji hao wanaweza kufungwa jela miaka mitatu kila mmoja ikiwa watapatikana na hatia.
Mchimba Riziki Michezo

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score