Saturday, January 18, 2014

TANZANIA: WILAYA MPYA 31 ZENYE MADINI

Dar es Salaam.Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema, tathimini iliyofanywa na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) imebaini kuwapo kwa madini ya aina mbalimbali katika wilaya 31 nchini.
Profesa Muhongo alisema jana kuwa, kubainika kuwapo kwa madini hayo kutachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa pato la taifa na malengo ya milenia ya nchi ifikapo mwaka 2025 yatafikiwa pasi na shaka.
Alisema katika bajeti ya mwaka huu, wametenga Sh6.3 bilioni ambazo zitakuwa chini ya Shirika la Madini Tanzania (Stamico) ili kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zao.
Alisema malengo ya Serikali kwa Sekta ya Madini kufikia mwaka 2025 ni ichangie asiliamia 10 ya pato la taifa ambapo sasa inachangia kwa asiliamia 3.3.
“Tunataka kufikia mwaka 2025 sekta ya madini ichangie zaidi ya asiliamia 10 katika pato la taifa, kubainika kwa madini katika wilaya hizo kutachangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla,” alisema Profesa Muhongo.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa GST, Profesa Abdulkarim Mruma alisema, nchi ikiwa na migodi mingi sehemu mbalimbali kutasaidia pia maendeleo ya mtu mmoja mmoja.
“Bila shaka pato la taifa nalo litaongezeka, wananchi watakuwa na fursa ya kutumia machimbo hayo kuboresha maisha yao na hiyo itafanikiwa ikiwa mipango ya Serikali ya kuwapa kipaumbele wachimbaji wadogo itafanyika,” alisema.
Baadhi ya wilaya ambazo zimebainika kuwa na madini hayo ni Igunga, Arumeru, Babati, Iramba, Kilosa, Manyara, Bagamoyo, Gairo, Nchemba, Chamwino, Handeni,Kiteto, Kongwa, Mbalali, Ikungi, Manyoni na Mbozi.
Mchimba riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score