Friday, February 7, 2014

MABASHA WAZINDUA KITABU NAIROBI

MABASHA Jumatano walizindua kitabu chao kama hatua mojawapo ya kutaka kukubalika nchini Kenya; takriban wiki mbili tu baada ya mwandishi maarufu wa vitabu Bw Binyavanga Wainaina kujitokeza hadharani na kusema kuwa ni shoga.
Nakala Ya Kitabu Cha Mabasha Kilichozinduliwa Nairobi Jumatano. 
Kitabu hicho chenye kichwa: Wasioonekana - Hadithi za Jamii Fiche nchini Kenya, kimeandikwa na aliyekuwa mwanahabari na mwanaharakati wa kutetea haki za mashoga, Bw Kevin Mwachiro.

 Kitabu hicho chenye  kurasa 114 kinajumuisha mkusanyiko wa hadithi za watu ambao wanadaiwa kupitia hali ngumu baada ya kudhihirika kuwa ni mabasha katika maeneo yote nchini.

Kulingana na Bw  Mwachiro, 40, kuna Wakenya wengi ambao hawajaweka hadharani kuwa wana uhusiano na watu wenye jinsia moja kutokana na hofu ya kutengwa  na jamii.

Huku hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho, jijini Nairobi iliyohudhuriwa na wanaharakati mbalimbali wa kueteta haki za mabasha, Bw Mwachiro alisema mabasha wamenyimwa nafasi yao katika jamii nchini Kenya.

“Naamini kitabu hiki kitaifanya jamii kuamini kuwa mabasha wanapatikana katika maeneo yote nchini Kenya na wala sio Mombasa,”  akasema Bw Mwachiro ambaye alikuwa mwandishi wa habari wa Shirika la Habari la Uingereza (BBC).

Katiba
 “Kwenye Jarida la kitabu changu kuna mguu wa mtu ambaye huwezi ukatambua ikiwa ni mwanamke au mwanaume, hiyo ina maana kuwa watu unaokutana nao mitaani huwezi hukawatambua kuwa wana uhusiano wa aina gani,” akaeleza.

Kenya ni miongoni mataifa ya Kiafirika ambayo yameharamisha ndoa za jinsia moja. Hata hivyo, mabasha wanadai kuwa ushoga na usagaji vimejumuishwa katika katiba kwani katiba imempatia Wakenya haki ya kushirikiana na  mtu yeyote. Barani Afrika, nchi ya Afrika Kusini ndiyo ilikuwa ya kwanza kuhalalisha ndoa za jinsia moja mwaka wa 2006.

Bw Binyavanga ambaye alikuwepo katika uzinduzi huo aliwataka mabasha ambao wanaona haya kujitangaza wafanye hivyo huku bado wakiwa hai.

Bw Binyavanga alipasua mbarika kuwa ni shoga wiki mbili zilizopita jambo ambalo lilileta mjadala mkali nchini huku baadhi wakimtaja kama shujaa ilhali wengine wakishutumu hatua hiyo.


Chanzo Swahili Hub
Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score