KOCHA wa Manchester City, Manuel
Pellegrini amesema timu yake itakosahuduma ya kiungo matata Samir Nasri.
Nasri atakuwa nje kwa wiki nane baada ya kuumia mshipa wa mguu katika goti lake la kushoto kutokana na rafu mbaya aliyochezewa na Mapou Yanga-Mbiwa wakati City ilipoizamisha Newcastle 2-0, Jumapili.
Mfaransa huyo amekuwa muhimu katika kikosi cha City ambayo kimecheza mechi 10 bila kupoteza katika Ligi Kuu ya England na kikiwa pointi moja nyuma ya vinara Arsenal.
Pellegrini ambaye kikosi chake jana kilicheza na Blackburn katika marudiano ya Kombe la FA, alisema Nasri atakumbukwa sana.
“Ni mchezaji muhimu kwetu. Pia alikuwa katika kiwango cha juu kwa sasa, kwa hiyo tuna matumaini atarejea haraka iwezekanavyo,” alisema kocha huyo raia wa
Chile.
“Lakini nafikiri kwamba wiki sita au saba (atakazokuwa nje Nasri) zitakuwa ngumu.”
Kikosi cha City kililazimishwa sare ya bao 1-1 na Blackburn iliyo Daraja la Kwanza na hivyo jana kurudiana kwenye Uwanja wa Etihad.
Pellegrini alizungumzia umuhimu wa Kombe la FA, akisema anataka kushinda kila taji msimu huu.
City hapo jana usiku iliweza kuizamisha Blackburn Rovers kwa magoli tano bila katika kinyaganyiro cha FA.
Magoli hayo yalifungwa na washambuliaji (Negredo 45+1' na 47', E.Dzeko 67' na 79' na Aguero 73').
Mchimba Riziki Michezo
Thursday, January 16, 2014
Nasri wiki 8 Nje kutokana na majeraha
Imechapishwa na
Unknown
kwa
Thursday, January 16, 2014
Email This
BlogThis!
Share to Twitter
Share to Facebook
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved
0 maoni:
Post a Comment