Tuesday, January 14, 2014

Simanzi Watu 200 wazama mto Nile S.Sudan

Zaidi ya watu 200 raia wa Sudan Kusini
wamezama katika ajali ya boti kwenye mto
Nile wakikimbia vita vinavyoendelea katika
mji wa Malakal.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Sudan Kusini.
Boti hiyo iliyozama, ilikuwa imewabeba watu wengi kupindukia.

Watu hao walikuwa wanatoroka vita vinavyotokota katika mji wa
Malakal.

Mapigano yalizuka Sudan Kusini mwezi Disemba mwaka jana baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa makamu wake wa Rais
Riek Machar, kwa kuwa na njama ya
kumpindua.

Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu
1,000 wameuawa tangu ghasia kuanza nchini

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score