Thursday, November 14, 2013

KAMA UNA MACHOZI YA KARIBU USISOME..!! SIMULIZI YA KWELI YA KUSISIMUA NA KUSIKITISHA YA MTOTO JANETH..!!

KAMA UNA MACHOZI YA KARIBU
USISOME..!! SIMULIZI YA KWELI
YA KUSISIMUA NA KUSIKITISHA
YA MTOTO JANETH..!!

Kengele ya kutoka darasani iligongwa,
wanafunzi wa shule ya msingi wakaanza
kutoka madarasani huku wakifukuzana
wengine wakipiga kelele ilimradi shwangwe
tu.

Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufundisha
shule za hatua hiyo.
Ilikuwa ni shule ya serikali.
Jicho langu liliangukia katika sura ya
msichana mdogo, nguo zake chafu. Alikuwa
analia.
Alikuwa peke yake na hakuwa na yeyote wa
kumbembeleza.
Mimi kama mwalimu sikutaka kujisogeza
karibu naye sana. Kwanza nilikuwa mgeni.
Nikaachana naye.

Siku iliyofuata tukio kama lile likajirudia.
Msichana yuleyule wakati ule uleule wa
kutawanyika, alikuwa analia sana.
Mwishowe aliondoka huku akiwa analia.
“Mbona mwenzenu analia?” nilimuuliza
mwanafunzi mmoja.
“Huyo ni mama kulialia..” alinijibu huku
anacheka.

Haikuniingia akilini hata kidogo kuwa yule
binti analia bila sababu.
Siku ya tatu nikaanza kujiweka karibu naye.
Muda wa mapumziko nilimwita
nikamnunulia chai, alikuwa ananiogopa na
hakutaka kuniangalia machoni.
Sikumuuliza lolote juu ya tabia yake ya kulia
lia kila anaporuhusiwa kurejea nyumbani.

Hata siku hiyo pia alilia vilevile. Wenzake
wakawa wanamzomea.
Akili yangu iligoma kuamini kuwa binti yule
analia bila sababu.
Kwanini alie wakati wa kutawanyika tu??
Hapana si bure.
Nikaendelea kujiweka karibu naye. Mkuu wa
shule akafikishiwa taarifa kuwa nina
mahusiano ya kimapenzi na yule mtoto.

Moyo wangu na Mungu pekee ndio walikuwa
mashahidi. Nilikosa cha kujibu.
Nilijaribu kujiweka mbali naye lakini moyo
ulinambia kuwa kuna jambo natakiwa
kulijua.

Nikaendelea kuwa karibu naye. Hatimaye
mkuu wa shule akanisimamisha kufundisha
pale kwa tabia yangu ya kufanya mapenzi na
mwanafunzi.
Nilijitetea lakini sikueleweka. Nikamwachia
Mungu……
Licha ya kusimamishwa kazi, niliendelea
kufuatilia nyendo za yule binti aliyeitwa
Janeth.
Kila alipotoka shule nilimvizia njiani na
kumnunulia chakula, kisha tunazungumza
kidogo.

Aliponiamini kama kaka yake ndipo
nikajieleza dukuduku langu.
“Janeth…” nilimuita.
“Bee kaka ….” Aliitika huku akinitazama.
“Nyumbani unaishi na wazazi.”
“Ndio naishi na mama..baba huwa anasafiri
safari.”

“Mama yako ana watoto wangapi?”
“Mama yangu alikufa….alikufa nikiwa mdogo
hata simkumbuki” Alijibu kwa sauti ya chini.
“Kwa hiyo unaishi na mama mdogo.”
“Ndio.”
“Unampenda mama mdogo?”
Swali hili likaikatisha furaha ya Janeth.
Akaanza kulia, alilia bila kukoma, Janeth
alilia kwa uchungu hadi nikajisikia vibaya.
Nilimbembeleza kisha sikumuuliza tena.

Siku zikaenda bila kumuuliza chochote..
Baada ya siku kumi, ilikuwa siku ya michezo
pale shuleni, hivyo hapakuwa na masomo.
Janeth alichelewa kuja shule, nilimngoja
uwanjani, hadi alipofika majira ya saa nne.
Nikamwambia twende kunywa chai.
Siku hiyo nilimpeleka mbali kidogo,
tukanywa chai, kisha tukakaa mahali
palipokuwa wazi.
Nikaleta tena mjadala mezani.
Ni kuhusu maisha ya Janeth.
Alikataa kabisa kusema lolote, nilimshawishi
sana.

“Usiogope mimi ni kaka yako.” Nilimpooza.
Janeth badala ya kusimulia akaanza kulia
tena.
“Ataniua mama nikisemaaaa” alilalamika.
Nikambembeleza hatimaye akanieleza jinsi
anavyonyanyaswa na mama yake.

“Mama hanipendi hata kidogo, ananipiga na
kuninyima chakula, hapendi nije shule,
vyombo tunavyotumia usiku hataki nivioshe
usiku na hataki niwahi kuamka asubuhi,
nikiamka natakiwa kufanya kazi zote,
kufagia uwanja, kudeki nyumba, kuosha
vyombo kisha ndipo nije shule. Baba
akiwepo anajidai kunijali sana…”
Alijieleza.
“Ni hayo tu Janeth….niambie kila kitu.”
“Akijua ananiua alisema….”
“Kwani amewahi kukutesa vipi..”
Ni hapa Janeth alivyozungumza huku analia
kilio ambacho hakitatoka masikioni mwangu
kamwe.

Siku moja, alichelewa kuamka, ilikuwa siku
ya mapumziko.
Mama yake alipomwamsha, aliitika na
kupitiwa usingizi tena.
Mama aliporejea mara ya pili, alikuwa na mti
mkavu, alimpiga nao kichwani na popote
pale katika mwili, alipoona hiyo haitoshi
akamvua nguo, akausokomeza katika sehemu
za siri, aliuigiza hovyohovyo, ukuni huo
ulikuwa wa moto.

Yeyote mwenye moyo wa nyama ajifikirie
ukuni wa moto ukazamishwa sehemu za siri
za mtoto wa darasa la sita.
Nilitokwa machozi.
Nikawahi kujifuta hakuona.
“Baba yeye alisemaje….”
“Baba ni mkali na hapendi kunisikiliza na
mama aliniambia nikiambia mtu ananiua
mara moja.” Alijibu kwa huzuni.
“Nikija na dada yangu tunaweza kukuona
ulivyounguzwa..”
“Ndio…” alinijibu.
Sikutaka kulaza damu nikampigia simu rafiki
yangu wa kike.
Nikamuuliza kama yupo kwake, alikuwepo.

Nikaongozana na Janeth.
Tukafika, Janeth akatoa nguo zote.
Ilihitaji moyo wa kiuaji sana kutazama mwili
wa Janeth mara mbilimbili.
Alitisha, hakika alikuwa ameunguzwa vibaya
na vidonda vilikuwa havijapona vizuri.

Dada yule alishindwa kujizuia alimlazimisha
Janeth twende kwa mama yake amkabiri na
kumpa kipigo. Nikamzuia.
Hata mimi nilikuwa na hasira kali. Lakini
sikutaka kuiruhusu ifanye kazi.
Nikachukua kamera, nikampiga picha Janeth
katika yale makovu.

Mbio mbio nikaenda polisi, kituo cha haki za
watoto nikaelezea mkasa ule huku
nikishindwa kujizuia machozi.
Nikawaonyesha na picha.
Tukaongozana nao hadi nyumbani kwao
Janeth.
Mama yule akakamatwa bila kutarajia.
Nilitamani kumrukia nimng’ate lakini
haikuruhusiwa.
Sheria ikafuata mkondo. Janeth akaanza
kupokea tiba.

Yule mama akahukumiwa kwenda jela miaka
sita..hadi sasa yupo jela.
Mume wake alitozwa faini kubwa kwa kosa
la kutofuatilia maendeleo ya mtoto wake
kiafya……..

Mimi nilirudishwa kazini, kwa heshima
kubwa. Heshima ya nkumkomboa mtoto.

***Akina JANETH wapo mtaani
kwako…..usiwaangalie na kuwaacha tu…
hebu jaribu KUWA SAUTI YAO… .hawawezi
kusema…hebu sema badala yao…….wanalia
kisikie kilio chao…….

KAMA UMEGUSWA NA MKASA HUU SHARE
NA NDUGU JAMAA NA
MARAFIKI ZAKO ILI WAONE.

SOURCE Kandilihuru Blog.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score