Tuesday, November 12, 2013

Vyombo Mbalimbali Vyazidi Kuipinga Mswada Wa Sheria Kwa Vyombo Vya Habari Kenya, Uhuru Akataa Kuitia Saini.

Nairobi, Kenya

Sauti za kutoelewana zinaendelea kuongezeka
juu ya mswada wenye utata wa vyombo vya
habari ambao bunge la Kenya liliupitisha
mwishoni mwa mwezi uliopita, huku ikiripotiwa
kwamba rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
aliurudisha kwenye chombo cha kutunga sheria
kufanya mabadiliko.

Mswada wa Habari na Mawasiliano wa Kenya
(marekebisho) wa mwaka wa 2013, ambao
unahitaji saini ya Kenyatta kuwa sheria,
umeweka faini kubwa ya hadi shilingi milioni 1
(dola11,700) kwa mwandishi wa habari binafsi
na shilingi milioni 20 (dola 234,000) kwa chombo
cha habari kwa ukiukaji wa kanuni za maadili.
Waandishi wa habari pia wangepewa adhabu
kwa kufutiwa usajili na akaunti zao za benki
kufungwa.

Watunga sheria ambao walipitisha sheria hiyo
pia waliunda Mahakama ya Rufaa ya
Mawasiliano na Vyombo vya habari, iliyopewa
jukumu la kusikiliza malalamiko na kutoa
adhabu kwa waandishi wa habari
watakaogunduliwa kuvunja sheria.
Hivi sasa
Baraza la Vyombo vya habari la Kenya
hushughulikia malalamiko kama hayo.
Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia
iliteua wajumbe wa mahakama hiyo, ambayo
kazi yake ni kuunda kanuni za maadili kwa
waandishi wa habari na vyombo vya habari.

"Kwetu sisi, hii ni sheria ya uonevu ambayo
inarudisha nchi nyuma kwenye enzi za giza,"
alisema Sekou Owino, mkuu wa huduma za
kisheria wa kampuni ya Nation Media Group.
Ukweli kwamba mahakama imeundwa na
wateuliwa wa serikali, pasipo wawakilishi wa
waandishi wa habari, inalifanya lisiwe huru
hususani wakati serikali inapokuwa na maslahi
na suala hilo, aliteta.
:
Mswada huo pia unahitaji vyombo vya habari
kutumia asilimia 60 ya programu zake kwenye
"habari za ndani ya nchi", alisema. Hili ni suala
lenye ubishi kwa sababu mswada huo
haufafanui "habari za ndani ya nchi" na mahitaji
hayo yanaingilia uhuru wa vyombo vya habari,
aliongezea.
Kenyatta na Ruto wajibu kuhusiana na
wasiwasi
Wakati alipojitokeza katika Kaunti ya Kajiado
tarehe 2 Novemba, Kenyatta alisema hatasaini
mswada wa sheria hadi masuala yenye ubishi
yashughulikiwe.
"Tunakusudia kushawishi vyombo vya habari
kama hiki kuwa mstari wa mbele katika uhuru
wa kujieleza ambao wote tunaupigania," alisema
Kenyatta.

Siku ya Ijumaa (tarehe 8 Novemba), Makamu wa
Rais William Ruto alikariri kusudio la rais.
"Bunge letu lilipitisha mswada ambao tunakubali
una ubishi," aliliambia kusanyiko la viongozi wa
vyombo vya habari Afrika katika mji mkuu wa
Ethiopia Addis Ababa, kwa mujibu wa AFP.

"Rais wa Kenya amerejesha mswada kwa bunge
ili masuala haya yashughulikiwe," alisema,
akiongeza kwamba "mjadala unaandaliwa kati
ya wadau mbalimbali -- bunge la utendaji na
vyombo vya habari -- kutatua masuala yenye
ubishi."

"Uhusiano kati ya serikali na vyombo vya habari
hauhitaji ushindani," alisema Ruto.
Sheria ina lengo la 'kuwanyamazisha
waandishi wa habari'
Lakini wawakilishi wa vyombo vya habari na
wawakilishi na watetezi wanaendelea kuukosoa
mswada huo.

Kifungu cha 19, shirika la utetetezi wa haki za
binadamu lenye makao makuu huko London
ambalo linapambana na udhibiti wa habari na
kukuza uhuru wa kujieleza na wa habari.
aliielezea sheria hiyo kuwa ni ya "kizamani".
Muswada huo unakiuka vifungu vya katiba ya
Kenya na kuanzisha vifungu vya viwango vya
kimataifa vya habari, Mkurugenzi wa Kifungu
cha 19 Pembe ya Africa Henry Maina alisema.

Katiba ya Kenya inahakikisha "uhuru na
kujitegemea kwa vyombo vya habari vya
kielektroniki, uchapishaji na aina nyengine za
habari".
"Taifa halitapaswa kutekeleza udhibiti au
kuingilia kati mtu yeyote anayajihusisha na
utangazaji, utoaji au usamabazaji wa chapisho
au usambazaji wa habari kwa njia yeyote; au
kuadhibu mtu yeyote kwa maoni au mtazamo
wa yaliyomo katika habari, chapisho au
usambazaji wa habari," inaeleza.
"Lakini kile ambacho bunge imepitisha ni jaribio
la makusudi la serikali na vyombo vyake
kudhibiti vyombo vya habari kinyume na katiba,"
Maina alisema.

"Kuna vitisho vya kutosha kwa jina la usalama
wa taifa, ambapo katika hali halisi serikali
inataka kufunga nafasi za kidemokrasia za
watu," Mwenyekiti wa Chama cha Sheria cha
Kenya Eric Mutua alisema. "Hili
linapaswa kupingwa na Wakenya wote."

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wahariri wa
Kenya David Ohito alisema ukali wa adhabu kwa
uvunjaji wa sheria unaweza kusabibisha vituo
vya redio na kampuni nyengine za vyombo
vyengine kufungwa kwa sababu vingi vyao
haviwezi kulipa faini hizo zinazotarajiwa.

"Kile ambacho sheria imetolewa ni
kuwanyamazisha waandishi wa habari na
vyombo vya habari, kumaanisha kwamba
wananchi hawatakuwa na uwanja wa kujielezea
kwa uhuru dhidi ya watawala wasiokuwa
wawajibikaji. Inamaanisha kwamba nchi nzima
itakuwa imenyimwa haki ya kuieleza uhuru,"
Ohito alisema.

"Nyingi ya kampuni zetu za habari zina bajeti ya
uendeshaji kwa mwaka chini ya shilingi milioni
40 [dola 468,000]," alisema. "Ikiwa utavitwanga
na angalau faini tatu kila mwaka, maana yake
utakuwa umekula bajeti yao yote. Hawatakuwa
na chaguo lingine zaidi ya kufunga."

Na, adhabu ambazo waandishi wa habari binafsi
wanazoweza kukabiliana nazo, pia zitakuwa
kubwa mno, alisema Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Maripota wa Kenya, William Oloo Janak.
"Faini hizi ni kubwa kupita kiasi," Janak alisema . "Hakuna sheria nyengine yeyote katika
nchi hii ambayo ina faini kubwa ya utovu wa
adabu kibinadamu inayoamuliwa na mahakama.
Kwa sisi, hili ni jaribio la serikali la
kuwanyanyasa waandishi wa habari."

'Hakuna chochote cha kibabe au kinyume
na katiba katika mswada'
Hata hivyo, Jamleck Kamau, mbunge ambaye
aliupeleka mswada huo katika Bunge la Taifa,
alivishutumu vyombo vya habari vya Kenya kwa
kupotosha ukweli.

"Suala hili limekuwa likitangazwa vibaya. Kwa sisi
hakuna chochote cha kibabe au kinyume na
katiba katika mswada huo," Kamau, ambaye pia
ni mwenyekiti wa kamati ya Mawasiliano na
Habari ya bunge alisema.

"Tunawaomba rais kutia saini iwe sheria kama
ilivyo kwa sababu vipengele vya vilivyomo humo
ni vizuri kwa nchi hii kwa kuwa vitavifanya
vyombo vyetu vya habari kuwajibika zaidi na
kuwa na malengo katika kazi yao ambazo kwa
upande mwengine utaibadilisha Kenya," alisema.
"Inapotosha kweli [kusema] kwamba Mahakama
ya Rufaa ya Mawasiliano na Vyombo vya habari
itakuwa na nguvu kupita kiasi za kuwatia
mbaroni waandishi wa habari na kuvamia ofisi
za vyombo vya habari. Lakini kama tulivyosema
kabla, suala hili limetatuliwa na mswada umo
njiani kuelekea kuwa sheria," alisema, na
kukataa kufafanua zaidi.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score