Thursday, November 14, 2013

Washukiwa Wawili Wa Ugaidi Wauwa Eastleigh Nairobi.

Polisi ya Kenya hapo jana walifanikiwa  kuwapiga risasi na kuwauwa watu
wawili wanaoshukiwa kuhusika na mashambulizi
dhidi ya msikiti mmoja uliopo Jam Street
Eastleigh, jijini Nairobi, mwaka jana,

"Ni vijana na tumepata guruneti la mkono na
bastola moja kutoka kwao. Tunaamini walikuwa
sehemu ya genge kubwa ambalo limekuwa
likiwatisha watu," alisema Kamanda wa Polisi wa
Kaunti ya Nairobi, Benson Kibui.

Washukiwa hao waliuawa karibu na kituo cha
kurekebisha magari yaani Garrage  hapa Eastleigh.

Bado haifahamiki kama
walikuwa wanadhamiria kutumia bomu hilo
kufanya mashambulizi ya kigaidi.
Walikuwa wanasindikizwa na kijana wa tatu,
ambaye polisi sasa wanamtafuta, alisema Kibui,
kwa mujibu wa kituo cha Capital FM.

Wanaaminika kuwa sehemu ya kundi
linalohusika na mashambulizi dhidi ya waumini
waliokuwa wakitoka kwenye msikiti wa Al Hidaya
baada ya sala ya Ijumaa mwezi wa Disemba
2012, ambapo watu watano waliuawa na 16
kujeruhiwa, akiwemo mbunge wa Kamukunji,
Yussuf Hassan.

Mashambulizi dhidi ya raia hapa Eastleigh yalikithiri mwishoni  mwaka jana kwa kundi lisilojulikana kushambulia
Sehemu yenye mkusanyiko ya watu wengi lakini polisi wa kulinda raia walithibiti hali hiyo mpaka sasa hali ya usalama wa kutosha ipo katika mtaa huu.

Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score