Thursday, November 14, 2013

Warioba Atoa Rambirambi kwa Familia Ya Dr Mvungi

Wakili wa Tanzania na mjumbe wa Tume ya
Kupitia Katiba (CRC) Sengondo Mvungi ,
aliyekuwa amejeruhiwa vibaya mapema mwezi
huu Alipovamiwa nyumbani kwake karibu
na jiji la  Dar es Salaam, alifariki siku ya Jumanne katika hospitali moja
nchini Afrika Kusini.

Kiasi cha watu sita wanaoshukiwa kuwa wezi
waliokuwa wamebeba mapanga walimshambulia
Mvungi nyumbani kwake siku ya tarehe 2
Novemba.

Alipelekewa kwa haraka kwenye
Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Muhimbili
jijini Dar es Salaam ambako alikuwa kwenye
chumba cha wagonjwa mahututi hadi tarehe 7
Novemba,
aliposafirishwa kwenda Hospitali ya
Milpark jijini Johannesburg kwa matibabu zaidi.
Polisi hadi sasa wamewakamata washukiwa tisa.

Mwenyekiti wa CRC, Jaji Joseph Warioba,
alipeleka salamu zake za rambirambi kwa
familia ya Mvungi. "Alikuwa mtafiti ambaye
daima alikuwa na hamu ya kile alichokifanya.

Nilimjua na kufanya naye kazi hata kabla ya
kuwa mjumbe wa CRC, hivyo kifo cake kwa kweli
kimeniumiza," alisema Warioba.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score