Tuesday, November 12, 2013

Wasomali Nusu Millioni Kurudishwa Somalia

Wakimbizi wa Kisomali nchini Kenya
wanalazimika tu kurudi nyumbani kwa hiari,
ulisema Umoja wa Mataifa siku ya Jumatatu
(tarehe 11 Novemba) baada ya kusaini makubali
yanayolainisha hofu ya kuwepo urudishwaji wa
lazima wa wakimbizi zaidi ya nusu milioni .

"Urejeshwaji wa wakimbizi lazima ufanyike kwa
usalama na heshima," alisema Raouf Mazou,
mwakilishi wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa
Mataifa (UNHCR) nchini Kenya, akiongeza
kwamba shirika hilo litasaidia katika kuandaa
uhamishwaji huo ikiwa tu "hali iko sahihi,"
liliripoti shirika la habari la AFP.
Makubaliano hayo ya pamoja - yaliyowekwa
saini siku ya Jumapili jijini Nairobi na Kenya,
Somalia na UNHCR - yanakuja kukiwa na hofu
za mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya
wakimbizi wa Kisomali kufuatia al-Shabaab
kulizingira jengo la maduka la Westgate mnamo
mwezi Septemba .
Tume yenye wawakilishi kutoka pande zote tatu
itaamua lini uhamishwaji huo uanze na kiasi gani
cha pesa anakachohitaji kila mkimbizi
atakayehamishwa ili kufanikisha kipindi cha
mpito.
"Serikali ya Somalia itaendelea kujenga
mazingira salama kwa wakimbizi kurudi nchini
Somalia ili kuwawezesha kujiimarisha kwa
wepesi na kujenga upya maisha yao, wakiwemo
wakimbizi milioni 1.8 wa ndani ya Somalia,"
alisema Waziri wa Mambo ya Nje wa Somalia,
Fowsiyo Yusuf Haji Aadan, wakati wa kuwekwa
saini kwa makubaliano hayo, kwa mujibu wa
gazeti la The Standard la Kenya.

By Mchimba Riziki

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score