Tuesday, November 12, 2013

Ligi Kuu Somalia Yashika Kazi.

Mchimba Riziki Michezo.

Ligi Kuu ya Somalia ilianza kwenye Uwanja wa
Michezo wa Benadir, Mogadishu, siku ya Ijumaa
(tarehe 8 Novemba), kwa mechi ya kwanza kati
ya timu za Heegan na Gaadiidka kumalizika kwa
ushindi wa 3-2 wa Heegan.

Ligi hiyo kuu inafanyika kwenye uwanja wa
kisasa ukiwa na nyasi bandia kwa mara ya
kwanza baada ya shirikisho la mpira la
kimataifa, FIFA, kuufanyia matengenezo Uwanja
wa Benadir .

Timu nane za mpira wa miguu za Somalia
kutoka mikoa ya Benadir, Shabelle ya Chini na
Shabelle ya Kati zitashiriki kwenye ligi hii, Katibu
Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la
Somalia, Abdiqani Said Arab, alidokeza.

"Uwanja wa Michezo wa Benadir ulijengwa
mwaka 1956, lakini ukakumbwa na maharibiko
makubwa [wakati wa vita vya wenyewe kwa
wenyewe]," alisema Arab. "Hata hivyo, baada ya
matengenezo yaliyofanyika miaka miwili iliyopita,
umeboreshwa na kuwa na viwango vya kisasa.
Matengenezo hayo yalimalizika tarehe 1
Novemba, na ligi kuu ilianza tarehe 8
Novemba."

"Naishukuru FIFA kwa kuweka nyasi za bandia
uwanjani hapo, ambazo zinakidhi viwango vya
kimataifa kwa kipimo na ubora wake,"
aliongeza.
Alisema matengenezo hayo ya uwanja
yanazifanya mechi ziwe bora zaidi.

"Kutakuwa na ongezeko la vipaji vya
wanariadha, hamasa ya mashabiki na uzuri wa
uwanja. Sasa tuko kama yalivyo mataifa
mengine duniani na tuna fursa sawa kama
walizonazo," alisema.

Arab alisema sasa wako kwenye mchakato wa
kupanga matengenezo ya viwanja vingine kwani
uwanja mmoja hautoshi kwa mechi za mpira wa
miguu nchini Somalia.
"Matengenezo ya uwanja huu yalipokamilika,
tuliiomba FIFA kutengeneza uwanja mwengine,"
alisema. "Walikubali na tunataka kuufanyia
matengenezo uwanja wa [Chuo Kikuu cha Taifa
cha Somalia]," alisema, akiongeza kwamba
watajaribu kuhakikisha matengenezo
yanafanyika kwenye viwanja vingine hadi wawe
wametengeneza viwanja kumi.

0 maoni:


Copyright © 2014. Mchimba Riziki- All Rights Reserved

Map

Live score